Zijue Mbinu za Viongozi Wanawake walivyofanikisha maendeleo ya Elimu na udhibiti wa utoro kwa wanafunzi skuli za Msingi Na kupelekea kupata Mafanikio Bora katika ufaulu. .





Na Amina Ahmed Moh’d Pemba. 

 MIKAKATI  ya kudhibiti utoro skuli za msingi wilaya ya Micheweni imepelekea kuwepo kwa ufaulu mzuri miaka 4 Mfululizo  Zanzibar  ni kutokana na viongozi wa wilaya kufanya kazi kwa kushirikiana vyema na jamii . 

Wilaya Ya Micheweni  ipo katika Mkoa wa kaskazini ndani ya kisiwa cha  pemba ambayo ni moja kati ya wilaya kumi za Zanzibar . 

 Micheweni inaongoza kwa matokeo  ya darasa la nne Zanzibar sambamba na kuvuuka lengo  liliowekwa na wizara ya Elimu  juu ya kudhibiti tatizo la  utoro na kuwarejesha skuli wanafunzi wa skuli za msingi waliotoroka. 

 "Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu". Msemo huu umejidhihirisha mara  Mgeni khatib Yahya kuendeleza mikakati hiyo ni  pamoja na  kukemea   sherehe za mikusanyiko, ajira za watoto kuelimisha jamii  juu  ya umuhimu wa elimu jambo limefanikiwa kuwa bora matokeo  ya kitaifa . 

"Nilipokuja Katika wilaya hii   mwaka 2020 Tatizo la utoro lilikuwa lipo  linaumisha kichwa  na Lilishapigiwa  mbio na mwezangu aliepita  nilipofika nikaendeleza pale alipowacha".

ni maneno ya Mgeni Khatib Yahya ambae ni mkuu wa wilaya ya micheweni . 

SAbabu zilizopelekea utoro Wilaya ya Micheweni

Changamoto  kubwa zilizopelekea kuwepo kwa utoro kwa wanafunzi wa skuli za msingi wilayani  humo   .

"Wazazi walikuwa  hawataki Kutoa mashirikiano kudhibiti utoro, Ajira za watoto  zilikuwa kila sehemu wengine wanabanjishwa kokoto,  wanauzishwa samaki wanapara wengine wanaokota mwani pia wanakosa mda wa kuenda skuli  kutokana na kujishughulisha na mambo hayo ilikuwa". 

Mikakati  ya wilaya kudhibiti utoro baada ya kuwepo  kwa changamoto hizo ni ipi!. 

 Tumeweka mikakati maalum ambayo inasaidia  watoto walio na umri wa  kwenda  skuli wanaendelea na masomo  na   huo ulikuwa ni muendelezo tu kwangu  jitihada zilianza kwa kiongozi aliepita kabla yangu kupanga mikakati".

 "Tumepiga marufuku Ajira za watoto  maeneo yote mzazi atakaekiuka tunadili nae Jamii imeungana  kukemea utoro  kurekebisha maadili ya watoto kwa kuunda kamati maalum katika shehia zao" . 

" Tumefanya mikutano kuelimisha kila shehia umuhimu wa elimu  na malezi". 

Maneno ya Mgeni Khatib YahyaAmbae ni mkuu wa wilaya  Ya Micheweni. 
 Mkuu wa wilaya ya Micheweni Akiwa katika mkutano maalum waalim na wanafunzi Micheweni msingi. 

Baadhi ya wakaazi wa wilaya a micheweni Waeleza kuwa kushika nafasi ya kwanza   kitaifa  kwa mitihani ya darasa la nne  kwa miaka minne sasa zimetokana na jitihada za wakuu wa wilaya na kupelekea  wazazi waliowengi kubadilika. 

" Tuliwekewa mikutano  Tukaelimishwa  Tukaunda  kamati ya maadili   ya shehia,  na kufuatilia maendeleo ya wanafunzi  kusifiwa kwa mambo mema kama haya ni furaha kwetu  Hassani Ali Abdalla Mzazi shehia ya  Majenzi. 

Kwa mujibu wa   mkuu wa wilaya ya Micheweni  mwaka 2020 Wilaya hiyo ilikuwa  jumla ya wanafunzi watoro 7609 kw  ambao walikuwa nje ya skuli maeneo ambapo wanafunzi hao  3000 kati yao ni wanafunzi wa skuli za msingi . 

 Wanafunzi 1240 wamesharudishwa skuli rasmi wanaendelea vyema na masomo  wanawake ni 892 na 348 wakiwa ni wanaume.  ni maneno ya  Mgeni  kahtib Mkuu wa wilaya ya Micheweni. 

Anaendelea Kusema "Mpaka Mwaka 2021  Nilifanikiwa kuwarudisha Skuli Wanafunzi  1118    ambapo mapambano yaliendelea kwa kushirikiana na wizara husika  wazazi na  masheha  kufika mwezi September Idadi ya imeongezeka na  wengine  122 wamerudi skuli hao ni wanafunzi wa msingi kumbuka idadi niliokuambia ilikuwa ni pamoja na Sekondari . 

 Wilaya ya Micheweni Ina jumla ya skuli  za msingi 26   katika  maeneo  na shehia mbali mbali. 

 Wahusika wanaona juhudi hizi!. 

Asya Msellem Hassan ni Afisa elimu skuli za msingi  wilaya Ya Micheweni  Anasema  kuwa suala la utoro kwa sasa limepunguwa ukilinganisha na miaka iliyopita  na ufaulu kuongezeka kuanzia mwaka 2018 . 

"  Hali ya ufaulu ilibadilika  wilayani mwetu  baada ya kuongoza  wanawake kwa mfululizo  Bi salama halafu akaja bi Mgeni" 

" Salama Mbarouk Alikuja katika wilaya hii nakumbuka mwaka  2017 na  hapo mabadiliko ya  kudhibiti utoro  na kuongezeka  na kupanda kwa ufaulu kulianza kidogo kidogo"mwaka 2018 na  19 nakuendelea.
 
 Ongezeko la ufaulu wa wanafunzi skuli za msingi. 

Mwaka 2019  jumla  ya wanafunzi 107 walifaulu  kati ya wanafunzi 1632 ambao walifanya mitihani ya darasa la sita wilayani humo. 


ufaulu uliongezeka  zaidi mwaka 2020 ambapo   jumla ya wanafunzi 1919  waliofanya mitihani 167 kati yao  walifaulu   jambo ambalo  kabala halijawahi kutokea. 


Mwaka  2021  wanafunzi 257 walifaulu kati ya wanafunzi  3255 waliofanya mitihani skuli  za msingi wilaya hiyo.
 
 Takwimu hizo ni kwa niaba ya  Afisa elimu msingi wilaya ya micheweni Asya Msellem Hassan. 


Asya Msellem anadai  kuwa utoro uliobaki  wilaya ya Micheweni kwa sasa sio ule wa moja kwa moja  unatofautiana na ule wa miaka iliyopita   huku zaidi ukibaki katika maeneo ya ukanda wa pwani. 

"Upo ule utoro wa siku mbili siku moja bhasi na zaidi ni skuli ambazo zipo maeneo ya bahari Makangale, Tumbe, Shumba Maziwa ng'ombe hivyo sio ule wa mtoto kukatisha moja kwa moja  mkuu wa wilaya anatusaidia  kazo hii ya kumaliza utoro micheweni".

Jamii yaaswa  

" Wazazi kutengana, kuwatumikisha ajira zisizo lazima kwao endapo kufuatilia  mienendo yao  wazazi kuishi pamoja  tukiyadhibiti haya kwa pamoja hatutoshuka   katika ufaulu wala hatutowaangusha viongozi wetu   katika mapambano dhidi ya utoro." 

 Uongozi imara ni moja kati ya chachu ya maendeleo  Wanawake hawa ambao waliongoza kwa mfululizo katika wilaya  hiyo kumepelekea kuondoa tatizo la utoro lakini pia kusogeza mbele maendeleo ya elimu . 
 
"Zamani watoto walikuwa wanachelewa  kulala  wanazifuata ngoma  popote zinapopigwa  hawakataziki lakini aliekuwa mkuu wa wilaya alipotoa marufuku bhasi

Kidogo watoto walilegeza kamba  waliogopa wakaanza kutulia majumbani kusoma". Hassan Omar Mkaazi wa Majenzi."

Mara baada ya kuondoka wilayani humo mkuu wa   Tangu Mwaka 2017 wilaya ya Micheweni imebahatika kupata viongozi wanawake Salama Mbarouk khatib  mpaka kufikia sasa mwaka 2022 inaemdele kuongozwa na Mgeni khatib Yahya 
 
Wilaya yaweka mikakati  endelevu kudhibiti utoro  na kuendelea kubaki kileleni matokeo ya kitaifa  skuli za msingi. 

"Kwanza nitaendelea kusimamia suala hilo ili kuona  fursa ya upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi wa skuli za msingi inapatikana ipasavyo" 

"Kila ambae anawajibu wa kupata elimu ya msingi bhasi  nikiwa kama mama kama mlezi bhasi nitahakikisha anaipata  kwa gharama yeyote ile". 

"Nitahakikisha utoro hatokuwa sababu ya kukwamisha ufaulu nitaendeleza  vyema mashirikiano na wananchi wangu." 
Jengine " Nitahakikisha wazazi wa wanafunzi wanaendeleza utayari ambao wameanza kunionesha  kuhakikisha watoto wao wanaingia madarasani   kudhibiti kwa pamoja tatizo la utoro na kuweza kuendeleza  ufaulu mzuri . 


 Jee viongozi wa Shehia ambazo zinalalamikiwa  kuwepo kwa utoro zinamchango  gani juu ya hili la kidhibiti  na kuendeleza ufaulu! 

 Miongoni mwa shehia ambazo Asya Msellem afisa elimu msingi wilaya  ya micheweni alidai  kuwa ni moja kati Ya shehia ambazo bado utoro unaendelea ni  Makangale, Shumba  Tumbe  . 

"Utoro ulikiwepo kutokana na suala la maji wanafunzi walikuwa wanatumia mwanya huo kufuata maji ya bomba  ndio  sababu kushuka baharini" 

 kupara samaki  kuokota mwani na kufanya ucheza mwengine lakini kwa sasa  mashirikiano ya kamati  iliyoundwa  shehiani petu na wanakijiji  hasubutu mwanafunzi kutoroka wanagopa wakionekana watachukuliwa hatua". 

"Tunashukuru tatizo limepungua  sana  hata walimu wanatuambia na mkuu wetu wa wilaya anapita pita anatoa maelekezo  tunashirikiana nae bega kwa bega" 
Na sisi tumeweka sheria haswa mzazi atakaeonekana anamtumikisha mtoto  tutamchukulia hatua "
Ni maneno yaliotoka kinywani mwa  Said Kombo Said Sheha wa Makangale . 

 Rahila Ramadhan Juma Shehaw shehia Shumba Mjini alidokeza Hali ilivyokuwa awali kuhusu utoro lakini mikakati ya  kudhibiti suala hilo n maendeleo yaliofikiwa 

  " Suala hilo la utoro ilikuwa ni uelewa mdogo  wazazi juu ya umuhimu wa elimu  ndio  husababisha wanafunzi washindwe kudhibitiwa wanakuwa wapo majumbani mwao". 

"Halafu  kuna tatizo la waalimu Utakuta mwalimu mmoja anashghulikia darasa moja lenye wanafunzi pengine 70 wale atawadhibiti lakini  madarasa mengine huku hayana mwalimu hayasimamiwi wanatoroka   kwa vile vipindi zaidi ya vitatu darasa halijaingia mwalimu. "
 
"Wazazi walikuwa hawako tayari  kutoa mashirikiano kumaliza tatizo la utoro wala kusimamia wanafunzi wasome lakini  kiongozi wa wilaya hii amejitahidi kufanya vikao tunashirikiana na tumefanikiwa hilo utoro umepungua". 

"Hali ya ufaulu  mfano awali skuli yaa msingi  iliyopo shehiani mwangu skuli ya  karume  ilikuwa haitoi wanafunzi waliofaulu michipuo lakini  mwaka jana 2021 ilitoa ni jambo la faraja" .

Sheha wa shehia ya Micheweni Khadija Abdi Haji  Kuhusi masualahaya hakuwa nyuma kutoa ya moyoni. 

"Ni kiri utoro kwa wanafunzi wa skuli za msingi limefanikiwa kudhibitiwa ni  kutokana na kamati maalum ya kusimamia utoro wa wanafunzi   na tumefanikiwa juu ya hilo na leo hii limepungua kabisa. "


 Baadhi ya wanafunzi ambao walifanikiwa kurudishwa skuli na uongozi wa wilaya hiyo walitoa duku duku lao  walipokuwa nje ya  skuli  sababu wazitaja wadai ni kutokana na kukosa  sare kuumwa pamoja na kukosa ufahamu katika masomo yao.

Heri Omar "Nilijiona sifahamu masomo ya skuli nikawa nje ya skuli lakini kwa  sasa  nimesharudi nawaambia wanafunzi wengine ambao wametoroka warudi skuli tuje tusome.
 
" Nilikuwa sina sare kwa sasa nishapata  naawambia wanafunzi wenzangu warudi skuli waje tuje tusome elimu ni ufunguo wa maisha
 Alisema Mwanafunzi Time Makame. 

" Fatma Juma Ali ilikuwa naumwa na Kifua  nfio mana nikawa siji skuli kwa sasa nisharudi nawaambia wanafunzi wenzangu wasikae utoro waje skuli tusome tupate  kufanikiwa" . 


  Waalimu  kwa upande wao waeleza kuwa  jitihada za kudhibiti utoro kwa wanafunzi  zimetokana na vikao vya walimu wakuu  wa skuli zilizomo ndani ya wilaya kupanga mikakati ya pamoja  ili kuona tuna ufaulu haushuki. 


"Mikakati ikiwemo y walimu wakuu ikiwemo  kambi za kusoma muda wa ziada, kamati maalum za skuli kufuatilia watoro jambo ambalo tumefanikiwa kupunguza taatizo la utoro lakini  kuongeza ufaulu." 
 
Alisema  Mwalim Salum Mkadam Hamad Mwalimu Mkuu Skuli ya Mkanagale Msingi. 

  Kai Omar Haji kutoka skuli ya Micheweni B msingi aeleza kambi za kimasomo zina mchango  mkubwa na kuwa chachu ya maendeleo ya elimu na silaha ya kudhibiti utoro. 

"Yaani  lazima tujue mwenendo wa mwanafunzi   tunakuwa nao mda wote hilo linasababisha utoro usijitokeze kwa sana" . 

Wazazi nao watoa wito kwa Wizara 

 Haata hivvyo baadhi ya wazazi meiomba serikali ya wilaya hiyo kuzidisha mashirikiano katika kulimaliza suala la utoro ambalo kwa sasa limeanza kuleta matumaini ya kumalizika katika wilaya hiyo. 

 "Watoto wengine ni wasugu kiasi ambacho  unaweza ukamsemesha kuhusu skuli kama hakuskii lakini mikakati. yote inayochukuliwa imekuwa Dawa serikali naiomba iendeleze suala hili  wazazi tunafurahia kuskia wilaya inatajwa kwa wema  sio kwa ubaya" 

 Faki kombo Hamadi mzazi kutoka Shehia ya Majenzi wilaya ya micheweni. 

 Wizara ya Elimu ina mikakati gani nayo juu ya hili? 

 Wizara ya elimu na mafunzo Ya amali pemba Katika kulipatia ufumbuzi suala la utoro kwa wanafunzi wa  skuli za msingi  wilaya ya Micheweni pamoja na wilaya nyengine Ofisa mdhamini  anabainisha mikakati hiyo.

 "Upande  wa kaskazini pemba tumejenga zaidi ya madarasa  miamoja na nane, tumekarabati skuli  hata huko makangale tumejenga gorofa la vymba vya  madarasa  21 na madarasa haya mwngine ni mapya kabisa. 


" Tumeyapeleka  katika maeneo ya vijijini ambako kutokana na mazingira watoto hawasahawisahiki husoma, Lakini pia taasisis ya utumishi serikalini tayari imetangaza  nafasi za ajira kwa waalimu  na karibuni Serikali inakwenda kuajiri waalim  

" kwaio miundo mbinu inaimarishwa ajira zinatengenezwa  za waalimu na maslhi ya walimu yanaimarishwa ili ufaulu uengezeke sio Micheweni tu hata katika wilaya nyengine. 

"Mkakati wetu wizara ya elimu ni kuona tunaimarisha mfumo wa udhibiti wa wanafunzi maskulini Kwa sasa  upo lakini bado haujafikia vile ambavyo tunataka sisi wizara, 

hivyo tunaendelea kutoa mafunzo kwa waalimu wa madarasa ili waweke vizuri rikodi  nani kaja jana nani hakuja  nani kamaliza masomo,

 jengine tunawaita wazazi kuuliza kuhusu  mahudhurio kwanini fulani hakuja tutaweza kudhibiti utoro  moja kwa moja,

" Jengine ambalo ni kubwa zaidi tunatoa hamasa kwa wanafunzi ambao watafanya vizuri    kuwapa zawadi,  si hivyo tu wizara inampango wa kuboresha   na kufufu michezo mbali mbali ili iwe kivutio cha watoto kutokutoroka. 

Na mkakati mwengine ni kutumia mfumo shirikishi kushirikisha wazazi, walimu pamoja na wanafunzi wenyewe, tunatafuta msaada wa serikali za shehia wilaya mkoa jeshi la polisi pia ili kuona utoro unakoma na watoto wanapata haki yo ya msingi na mikakati yote hii imefanikiwa. 

"Aidha mdhamini huyo alisema kuwa  kwa sasa  kumekuwa na mabadiliko makubwa  kwa waalimu maskulini  jambo ambalo ambalo awali lilikuwa halipo. 

" Waalimu tuna mabadiliko makubwa kwa sasa  tunajitathmini  tunaandaa masomo ambayo hayatowachosha watoto, tunatumia mbinu mbadala ikiwemo ziara za kimasomo watoto wanatembea, 

Tunatumia  teaching aids  ambazo zitakuwa zimo ndani ya mazingira yao ili waweze kufurahia  masomo sababu wengine hutoroka kutokana na  njia mbovu za ufundishaji  zina wafanya kurudi nyuma tumewawekea komputa maskulini hiyo yote ni mikakati ya kuongeza ufaulu na kudhibiti utoro. 


 Hali ya utoro ipoje Zanzibar!. 

" Zanzibar nzima   ina watoto 35732 ambao wapo nje ya skuli na mikakati wa wizara ni  kuwarejesha wanafunzi hao  wote katika kipindi cha miaka mitatu" .  

"Baadhi ya wilaya imefanikiwa kuwarejesha  zaidi ya idadi iliyowekwa kwa mwaka   Micheweni ni miongoni mwao kutokana na  mashirikiano yao ni jambo la kujivunia" . 

Mashavu Ahmada Fakih Msimamizi mradi wa  Urejeshwaji skuli wanafunzi watoro skuli za msingi, sekondari  na madarasa ya elimu mbdala Zanzibar. 

 kwa mujibubwa  wa takwimu  kutoka kwa afisa elimu msingi  wilaya  micheweni Asya Msellem Hassan anasema hali ya  ufaulu awali kabla ya kuongozwa na viongozi wanawake  ilikuwahairidhishi  kwa miaka zaidi ya mitano. 

Hali ya ufaulu kabla ya miaka  minne ya viongozi  Wilaya ya Micheweni. 

  2013  Wanafunzi 1601 walifanya mitihani ya darasa la saba  wilayani  humo   801 wakiwa ni wanaume  na na wanawake 800 ambapo kati yao  Wanafunzi 13 pekee ndio waliopasi kuingia michipuo 

Mwaka 2014  Wanafunzi 1765 wanaume wakiwa ni 819 na wanawake 946  walifaulu walikuwa ni wanafunzi 63.

 Mwaka  215   wanafunzi 2443 walifanya mitihani  skuli za msingi wilaya ya Micheweni  1247 wanaume  1196 ni  wanawake  waliofaulu walikuwa ni jumla ya wanafunzi 35  pekee huku idadi ya wanafunzi watoro ikiongezeka. 
 
Kwa sasa Jamii ya Micheweni imehamasika katika suala la elimu na kudhibiti   tatizo la utoro ikiwa ni pamoja na  mashirikiano. 

Nguvu, ushawishi na uwajibikaji  waliono wanawake katika kuleta maendeleo ni kweli  Mama ni mama Popote " 

Mwisho. 













.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI