WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

Na Amina Ahmed Muhamed Pemba.

WAZAZI na walezi  wameatakiwa kufuatilia kwa ukaribu nyenendo  na tabia za watoto  pamoja na  vijana  wao  ili kuwanusuru kujiingiza katika tabia hatarishi za kutumia madawa ya kulevya  .

Kauli hiyo imetolewa na  waziri wa nchi ofisi ya makamu wa kwanza wa rais zanzibar Harus Said Suleiman katika ufunguzi wa kongamano  la maadhimisho ya siku ya kupiga vita  matumizi  na  usafirishaji wa dawa za kulevya duniani lililoanadaliwa  na mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya zanzibar katika  ukumbi wa makonyo wawi chake chake mapema leo.

Amesema  bado kuna changamoto kubwa katika malezi na usimamizi wa watoto hususan ni kundi la vijana  jambo ambalo  linapelekea kuwa na idadi kubwa ya  vijana wanaotumia madawa ya kulevya na kupelekea kuharibu  maisha yao kwa kujiingiza katika vitendo viovu ikiwemo wizi .

  "Bado kuna tatizo katika kusimamia malezi hususan ni vijana wetu jambo hili limepelekea kuwa na idadi ya zaidi ya watumiaji wa madaa ya kulevya   wasiopungua elf 15   visiwani zanzibar hivyo wazazi tuzidishe umakini katika malezi ya vijana wetu. alisema.

Akizungumza katika kongamano hilo Kamishna mkuu wa mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya  Zanzibar  Kanalli Buruhan Zuberi Nasoro amesema kuwa mamlaka hiyo itaendelea kuchukua hatua kali kwa wauzaji na waingizaji wa dawa za kulevya ikiwemo kutaifisha mali zao kwa watakaobainika kuhusika na masuala hayo hatarishi kwa taifa.

"Tutaendelea kupambana  na suala hili  kwa dhamira ya kulikemea lisiweze kuendelea niwatake wananchi kuendelea kusaidiana na mamlaka  kwa kutoa taarifa  watakapoona viashiria vya biashara hii  ili jamii iweze kuwa salama ".

Kwa upande wake kaimu  katibu mkuu ofisi ya makamu wa kwanza wa rais  Iliyasa Pakacha Haji amesema kuwa licha ya jitihada  zinazoendelea kuchukuliwa katika mapambano hayo bado janga hili linaendelea kuathiri taifa ambapo madhara yake yanapelekea kuathiri taifa.

 Nao baadhi ya washiriki walioshiriki katika kongamano hilo akiwemo Othman kombo Ali pamoja na  wameiomba serikali na mamlaka hiyo  kuwashirikisha wataalamu wa  afya CHV  kutoa elimu kwa jamii juu ya athari za madawa ya kulevya pamoja na  Thani  Salim Said   mraibu alieacha madawa ya kulevya wameiomba mamlaka  hiyo kudhibiti  uingiaji wa pombe pamoja na  vilezi vilivyozagaa vinavyotumiwa na watoto .

Kongamani hilo lililowashirikisha wanafunzi  kutoka skuli  na vyuo mbali mbali, vijana kutoka mabaraza ya vijana ,viongozi wa ulinzi na usalama ,wanasheria ,waath usala,viongozi wa serikali  watumiaji  waliocha madawa ya kulevya,waandishi wa habari Watendaji wa mahakama  pamoja na wanachi  na wadau mbali mbali .

Aidha  katika kongamano hilo mada mbali mbali zimewasilishwa ikiwemo athari za madawa ya kulevya na afya ya akili Uhalifu wa madawa ya kulevya na hatua za kukabiliana nazo  Sheria namba 8 ya mwaka 2021  ya mamla kudhibiti na kupambana na madawa ya kulevya ambapo kauli mbiu   katika maashimisho hayo ni Ushahidi upo wazi tuwekeze katika  kukinga.

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI