BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

NA,AMINA AHMED MOH'D.

JUMLA ya barabara 19  kutoka maeneo mbali mbali kusini na kaskazini Pemba ambazo zitakuwa na urefu kilo mita 99.4  zinatarajiwa  kujengwa  kwa kiwango cha lami  na kukamilika ujenzi wake mwezi Disemba mwaka huu 2024 .

Barabara  zenye  urefu tofauti ikiwemo   kubwa  yenye kilo mita  12  kutoka Konde  makangale mnarani  ni mkakati maalum uliowekwa na  serikali ya mapinduzi ya zanzibar kupitia mwaka mpya wa bajeti unaoanza  mwezi july   .

Akizungumza mara baada ya kumaliza ziara maalum  ya kuangalia  utekelezaji  wa sekta ya  barabara  na  bandari kisiwani humo  katibu mkuu wizara ya mawasiliano ujenzi  na uchukuzi Zanzibar  Dk Mngereza  Mzee Miraji  amesema kuwa  serikali imedhamiria kuzikamilisha kwa wakati  barabara hizo za kimkakati zilizowekwa na  wizara hiyo kupitia bajeti mpya  .
      KATIBU MKUU -WUMU           DK,MNGEREZA  MZEE  MIRAJI.
Amesema barabara nyingi kati ya hizo ni za muda mrefu na   ziliahidiwa kufanyiwa matengenezo  na serikali jambo ambalo limepelekea kuwekewa mikakati maalum katika ujenzi wake kutokana na  kuchelewa  kulikosababishwa na changamoto mbali mbali.

Aidha Mngereza amesema kuwa 
 ili  kuwaondolea usumbufu wananchi wake ambapo barabara hizo ziliahidiwa kufanyiwa matengenezo lakini kutokana na changamoto mbali mbali zimechelewa kufanyika kwa matengenezo hayo.
      KATIBU MKUU AKIZUNGUMZA NA WANANCH KUHUSU UJENZI WA BARABARA.
Barabara hizi ni za muda mrefu,kuna nyengine zimeahidiwa na serikali ya mapinduzi kwa takriban inafika miaka 10 sasa lakini kutokana na  changamoto mbilo tatu hazikuweza kukamilika kipindi icho lakimi serikali imedhamiria ndani ya miezi michache ijayo kuweza kukamilisha izi barabara.
Aidha Mngereza amewatoa hofu wananchi wa maeneo juu ya suala la uharibifu wa vipando pamoja na nyumba zitakazoathirika kutokana na kupisha ujenzi  wa barabara hizo ambapo amesema kuwa serikali italisimamia vyema suala hilo katika kuona kila muathirika anapata stahiki yake.

"Tunamshukuru mheshimiwa rais kwa sababu moja kati ya  vitu anavyohakikisha anavisisitiza ni pamoja na masuala haya ya kuhakikisha kuwa  hakuna mwananchi  ambae anakosa haki yake na sisi wizara tunalitekeleza hilo kwa umakini mkubwa  kuhakikisha kuwa wananchi hawatoondoshwa bila kupewa fidia kwanza kwa kushirikiana na wenzetu wa wizara ya ardhi pamoja na wizra ya fedha".

 Katika hatua nyengine katibu huyo amewataka wakandarasi  pamoja na washauri elekezi katika mradi wa  ujenzi wa bandari ya Shumba amemtaka mkandarasi mshauri  elekezi pamoja na watendaji  katika ujenzi huo kuongeza kasi ya ujenzi kwa kuzingatia ubora na wakati uliowekwa wa kukamilika ujenzi huo.
Kwa upande wake afisa mdhamini wizara ya mawasiliano na uchukuzi Ibrahim Saleh Juma amesema kuwa wizara hiyo itasimamia vyema suala la ujenzi wa barabara hizo zilizowekewa mkakati ili kuhakikisha zinawanufaisha wananchi katika shughuli zao kwa kukamilika kwa wakati uliowekwa na kusimamia vyema  ujenzi wenye ubora.
Wakizungumza baadhi ya wananchi katika maeneo tofauti  ya barabara hizo akiwemo Baraka Ali Mbwana kutoka Kinazini wameeleza shauku zao juu ya ujenzi wa barabaraza hizo  ambapo wameiomba wizara hiyo kusimamia  na kuzingatia mahitaji muhimu katika ujenzi wa barabara izo ikiwemo uwekwaji wa misingi ya kupitishiwa maji matuta pamoja na kalavati katika maeneo muhimu yanayitumika kwa shughuli mbali mbali.
Kwa upande wake Ramadhan Kiteri mshauri elekezi  Mkandarasi Allan Magoma pamoja na  Abdalla Salim kaim mkurugenzi  shirika la bandari Abdalla Salim Abdalla  wamesema kuwa wataendelea kusimamia vyema jukumu hilo la ujenzi wa bandari ya  Shumba ili likamilike kwa wakati . 

 Barabara hizo ambazo zinatarajiwa kujengwa na kampuni ya IRIS maeneo mbali mbali ni Wawi messi Mzambarau mboko ,Mchanga mdogo Mzambarau takao ,Pandani Pembeni ,Micheweni  Shumba mjini,Shumba bandarini ,Finya kicha ,Konde Makangale Mnarani ,Kizimbani Uzunguni,,Gando  Chaoni ,Gando Chokaani,Bwagamoyo Kele,Uondwe Nyali,Makongeni Kinazini,Barawa Mleteni,Ukutini Mtangani,Mgagadu kwa Otao,Mbuguani Tironi,pamoja na Wesha Mkumbuu.

Mwisho.






  

Comments

Popular posts from this blog

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI