UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI


Na Amina Ahmed Moh'd ,Pemba.


Pemba UONGOZI wa wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba umesema unaendelea kutambua na kuuthamini n a kuunga mkono mchango unaotolewa na Taasisi ya  
" Korea friends of hope international" KFHI   kwa wananchi katika shughuli mbali mbali ikiwemo Kuwawezesha kiuchumi na kuwapatia misaada muhimu inayiwasaidia katika maisha.
 Kauli hiyo imetolewa leo na mkuu wa Wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali alipokuwa akifungua mafunzo ya siku tatu  kwa  wakulima wakuu wa  mazao ya mboga mboga na matunda ikiwemo Tungule,Viazi lishe na matango kutoka mkoa wa kusini Pemba  yalioandaliwa na taasisi hiyo huko katika ukumbi wa Tasaf Chake Chake.

Amesema taasisi hiyo imekuwa mstari  wa mbele katika  kusaidia serikali  kuimarisha hali za wananchi ikiwemo kuwekeza katika elimu,kilimo na msaada  wa vyakula lishe   .

Mkuu wa wilaya huyo amewataka wakulima hao  kuyafanyia kazi mafunzo hayo ili yaweze kuwaletea tija katika kupata mazao bora yatakayowasaidia  kuwawezeaha kiuchumi na kupata lishe inayotokana na vyakula walivyolima.

 Katika hatua nyengine mkuu wa wilaya huyo amewataka wazazi na walezi  kuendelea kusimamia  maendeleo ya watoto katika elimu wanayopatiwa  kupitia msaada wa KFHI   ili iweze kuwasaidia katika masomo na kuwacha kuwatumia  kama nyenzo ya kujipatia kipato kwa kuwatumikisha katika ajira zisizo rasmi kwa maslahi yao.

Hata hivyo ameishukuru taasisi hiyo kwa kuendeleza utaratibu wa kuzisaidia familia  maskini msaada wa chakula lishe kila baada ya miezi 3 sambamba na  kusaidia gharama za masomo pamoja na matibabu yao.

 Aidha amewataka wazazi kuendelea kutoa mashirikiano na kutowavunja moyo  watendaji wa taasisi hiyo na kutoa mashirikiano kwa wanafunzi waliopata nafasi ya kwenda  Nchini korea kwajiki ya michezo ili waweze kurudi ja ushindi.

Kwa upande wake  Sylivia Albath kutoka KFHI amesema kuwa taasisi hiyo imekuwa ikisaidia kuleta faraja kwa wananchi wanaoishi katika hali ngumu za kimaisha ambapo jumla ya familia 800 zimefikiwa kutoka shehia mbali mbali ya wilaya hiyo.

Awali akizungumza katika mafunzo hayo afisa kilimo wilaya ya Chake Rashid Muhamed Wema amesema kuwa  mafunzo hayo yatasaidia kuleta mageuzi katika ukulima wa mboga mboga na matunda kwa wakulima wa  mkoa wa kusini Pemba.

Licha ya mafunzo hayo kwa wakulima zaidi ya 20 Taasisi hiyo ya Korea friends of hope international" KFHI  leo pia imekababidhi msaada wa  vipolo vya Mchele kwa familia 800 ambao wanaishi katika mazingira magumu.

Mwisho

Na Amina Ahmed Moh'd ,Pemba.


Pemba UONGOZI wa wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba umesema unaendelea kutambua na kuuthamini n a kuunga mkono mchango unaotolewa na Taasisi ya  
" Korea friends of hope international" KFHI   kwa wananchi katika shughuli mbali mbali ikiwemo Kuwawezesha kiuchumi na kuwapatia misaada muhimu inayiwasaidia katika maisha.

 Kauli hiyo imetolewa leo na mkuu wa Wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali alipokuwa akifungua mafunzo ya siku tatu  kwa  wakulima wakuu wa  mazao ya mboga mboga na matunda ikiwemo Tungule,Viazi lishe na matango kutoka mkoa wa kusini Pemba  yalioandaliwa na taasisi hiyo huko katika ukumbi wa Tasaf Chake Chake.

Amesema taasisi hiyo imekuwa mstari  wa mbele katika  kusaidia serikali  kuimarisha hali za wananchi ikiwemo kuwekeza katika elimu,kilimo na msaada  wa vyakula lishe   .

Mkuu wa wilaya huyo amewataka wakulima hao  kuyafanyia kazi mafunzo hayo ili yaweze kuwaletea tija katika kupata mazao bora yatakayowasaidia  kuwawezeaha kiuchumi na kupata lishe inayotokana na vyakula walivyolima.

 Katika hatua nyengine mkuu wa wilaya huyo amewataka wazazi na walezi  kuendelea kusimamia  maendeleo ya watoto katika elimu wanayopatiwa  kupitia msaada wa KFHI   ili iweze kuwasaidia katika masomo na kuwacha kuwatumia  kama nyenzo ya kujipatia kipato kwa kuwatumikisha katika ajira zisizo rasmi kwa maslahi yao.

Hata hivyo ameishukuru taasisi hiyo kwa kuendeleza utaratibu wa kuzisaidia familia  maskini msaada wa chakula lishe kila baada ya miezi 3 sambamba na  kusaidia gharama za masomo pamoja na matibabu yao.

 Aidha amewataka wazazi kuendelea kutoa mashirikiano na kutowavunja moyo  watendaji wa taasisi hiyo na kutoa mashirikiano kwa wanafunzi waliopata nafasi ya kwenda  Nchini korea kwajiki ya michezo ili waweze kurudi ja ushindi.

Kwa upande wake  Sylivia Albath kutoka KFHI amesema kuwa taasisi hiyo imekuwa ikisaidia kuleta faraja kwa wananchi wanaoishi katika hali ngumu za kimaisha ambapo jumla ya familia 800 zimefikiwa kutoka shehia mbali mbali ya wilaya hiyo.

Awali akizungumza katika mafunzo hayo afisa kilimo wilaya ya Chake Rashid Muhamed Wema amesema kuwa  mafunzo hayo yatasaidia kuleta mageuzi katika ukulima wa mboga mboga na matunda kwa wakulima wa  mkoa wa kusini Pemba.

Licha ya mafunzo hayo kwa wakulima zaidi ya 20 Taasisi hiyo ya Korea friends of hope international" KFHI  leo pia imekababidhi msaada wa  vipolo vya Mchele kwa familia 800 ambao wanaishi katika mazingira magumu.

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .