MASAUNI AZUNGUMZA HAYA NA WANANCHI

NA OMAR HASSAN – UNGUJA                                                   
WAZIRI wa Mambo ya ndani ya Nchi Mhe. Hamad Yussuf Masauni amewataka Maafisa wa Jeshi la Polisi Kamisheni ya Zanzibar kuongeza nguvu katika kuzuia na kupambana na uhalifu ili Zanzibar iendelee kuwa salama kwa wananchi na wageni.
Akizungumza na Maafisa wa Jeshi hilo huko Makao Makuu ya Polisi Zanzibar amesema pamoja na kuwa takwimu zinaonesha  kupungua kwa baadhi ya Makosa ya jinai bado zipo changamoto za kiuhalifu ambazo zinawasumbua wananchi 

Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad ameeleza kuwa uchache na uchakafu wa magari pamoja na uchache wa Askari ni miongoni mwa changamoto zinazokwamisha utendaji wa Jeshi hilo.

Akitoa taarifa ya Uhalifu wa Makosa ya jinai kwa kipindi cha miezi tisa mwaka 2022 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2021, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, kamishna Msaidizi wa Polisi Zubeir Chembela amesema kuna upungufu wa matukio 64 ya Udhalilishaji wa Jinsia na watoto.
Mwisho 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI