Taasisi Zapaza sauti kuelekea sikiu 16 za kupinga udhalilishaji.






Na Amina Ahmed Moh’d. 

TAASISI  zinazoshughulika na kupinga vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto kisiwani pemba  zimeiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuimarisha vyema mfumo wa upatikanaji wa takwimu  za matukio ya udhalilishaji  wa kijinsia ili kuonesha jamii   maendeleo yaliofikiwa  katika mapambano dhidi ya vitendo hivyo. 


Akizungumza  katika Mkutano maalum na waandishi wa habari  wa vyombo mbai mbali uliofanyika  katika ofisi za Tamwa  Mkanjuni Chake Chake Pemba  Mwenyekiti wa  asasi za kiraia zinazoshughulika na Mambo ya udhalilishji Nassor Bilal Ali alisema kuimarika kwa mifumo  hiyo kutaweza kuonesha  jitihada zinazochukuliwa na serikali pamoja na Asasi hizo katika mapambano   hayo ya kupinga vitendo hivyo. 

Aidha  Wanaasasi hao waliwataka waandishi wa habari Kuzidisha mashirikiano katika kutoa taarifa za ufuatiliaji na uendeshwaji wa  kesi za udhalilishaji   katika Mahakama mbali mbali  . 

Aidha asasi  hizo zimempngeza rais  wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi kwa kuanzisha mahakam maalum za udhalilishaji ambapo  wamesema  maahakam hizo zimekuwa zikifanya kazi vyema katikaa kusimamioa kesi za

udhalilishaji. 

 Akizungumza katika Mkutwno huo Tatu Abdalla Msellem, Mkurugenzi wa jumuiya Tumaini Jipya Pemba (TUJIPE) amesema katika kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia na udhalilishaji wanashirikiana na wadau mbali mbali ikiwemo viongozi wa dini ili kila mdau aweze kushiriki katika mapambano hayo.

 

Nae kwa upande wake Hafidh Abdi Said ni Mkurugenzi wa jumuiya ya Kupunguza Umaskini na Kuboresha Hali za Wananchi (KUKHAWA)Amesema kutokana na uzito wa tatizo la  udhalilishji wa kijinsia na udhalilishaji jumuiya hiyo imechukua jitihada za kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananmchi maeneo mbali mbali. 


Mkutano huo wa waandishi wa habari  kisiwani Pemba  uliikuwwa na lengo laa kutoa taarifa maalum  kuelekea  kilele cha siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili wa wanawake na watoto wa kike duniani,  ambayo huazimishwa  kila ifikapo Diosemba 10  ambapo kaulimbiu ya kimaitaifa ya mwaka huu 2022 inasema “KUUNGANISHA UANAHARAKATI KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANWAKE NA WASICHANA. 

Ambapo Taasisi hizo ni Chama  cha waandishi wa habari  wanawake Tanzania ( Tamwa Zanzibar) ,  Jumuia  za wasaidizi wa sheria wilaya 4 za pemba   Pegapo, Kukhawa,, Zayco, jumuia  ya watu wenyer ulemavu wa akili Zanzibar, ZAPDD, Blog ya Pemba Today pamoja na wizara inayosimamia    haki za watoto.

Mwisho. 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI