Wakandarasi Miradi ya Elimu Pemba wapewa Neno



NA FATMA SULEIMAN-PEMBA 

KATIBU  mkuu wizara ya Elimu na mafunzo ya amali Zanzibar  Khamis Abdalah Said amewataka wasimamizi  wakuu wa   ujenzi  wa miradi ya Elimu kusimamia na kutekeleza kwa wakati ujenzi wa  skuli na madarasa mbali mbali    Ili kutimiza lengo la Serekali la kuimarisha Majengo  Ili kutoa eElimu bora  kwa wanafunzi .

  Said Ameyasema hayo kwa  nyakati  tofauti katika ziara ya ya siku Moja ya kutembea miradi ya elimu inayoendelea kujengewa kisiwani Pemba.

Amesema ni vyema  wakandarasi kuongeza Kasi ya utendaji kazi kwa  wafanya kazi wao ili waweze  kukabidhi miradi hiyo kwa wakati husika ikiwa imekamilika na kwa ubora uliotarajiwa.

Katika hatua nyengine Katibu Mkuu amewataka walimu kutoa ushirikiano wa dhati katika kueka msingi nzuri kwa wanafunzi utakaowezesha kupata Viongozi Bora wa baadae.

Kwa upande wao wakandarasi wa miradi hiyo wameelezea baadhi ya changamoto zinazowakabili hatahivyo wameahidi kumalizia ujenzi huo kwa wakati husika na kwa viwango vya ubora vinavyohitajika licha ya changamoto hizo.

Katika ziara yake hio Katibu Mkuu alitembelea kituo Cha Wakorea kilichopo Madungu, Skuli  ya Wanafunzi wenye mahitaji maalum Pujini  ,pamoja na Sekondari  ambazo zinazoendelea na ujenzi, pia ametembelea Skuli ya Mwambe ,  Kwale , pamoja na kuzungumza na Walimu Wakuu wa Skuli za Sekondari kisiwani Pemba.

Hii ni ziara yake ya kwanza ya kikazi kisiwani Pemba tokea kuapishwa kukamata nyadhifa hio  kufuatia mabadiliko yaliyofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi.

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI