SOKO LA OLE LA ZINDULIWA

Na Fatma Suleiman. 

MWAKILISHI wa jimbo la Ole Masoud  Ali Muhammed amewataka wafanya biashara wa jimbo la ole kulitumia ipasavyo soko la mboga mboga  lililopo olee kianga  bila ya kuingiza  itikadi za kisiasa ili kuendelea kujipatia rizki za halali .

Akizungumza na wana jimbo  mara baada ya uzinduzi wa soko hilo mh Massoud ambae ni waziri wanchi Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ amesema soko hilo amelijenga kwa ajili ya wanachi wote na sio la mtu binafsi hivyo ni vyema litumike kama lilivyo kusudiwa.


Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya chake chake Abdala Rashid Ali amewataka wanachi wa ole kuthamini jitihada za viongozi wao pamoja na kulitunza ili liweze kutumika kwa muda mrefu .

Akitoa maelezo juu ya matumizi ya soko  msimamizi wa ujenzi wa mradi huo Thabit Othman Abdalla  amesema soko hilo litatumika na wauzaji zaidi ya 20 ambapo  watauza biashara zao katika mazingira rafiki na salama.

Wakitoa neno la shukurani kwa niaba ya wafanya biashara wengine Hamad Salum amesema awali ilikua wakiteseka wao na hata wateja lakini kwa sasa mwakilishi amewakomboa kutoka kwenye kilio . 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI