Posts

Showing posts from September, 2023

SERIKALI YAAHIDI KUKIFUNGUA ZAIDI KISIWA CHA KOJANI KWA KUTATUA CHANGAMOTO MBALI MBALI ZINAZORUDISHA NYUMA MAENDELEO KISIWANI HUMO.

Image
NA AMINA AHMED MOH'D, PEMBA ZIARA ya makamu wa pili wa rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla kuendelea kukagua  ujenzi wa skuli za ghorofa maeneo mbali mbali kisiwani Pemba leo   hii imefika katika  wilaya ndogo ya Kojani mkoa wa kaskazini kukagua mradi  huo pamoja  kuzungumza na wananchi na kuweza kusikiliza changamoto zinazowakabili .   Akizungumza na wanachi katika  kijiji cha Kipata  Kojani    eneo ambalo linajengwa skuli hiyo kwajili ya Wanafunzi wa Msingi  makamu huyo amesema  kuwa  serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuboresha maenedeleo ya elimu kisiwani humo  ili kupata Viongozi bora watakoasimamia taifa katika nyanja mbali mbali.    " Tunataka tutoe wasomi zaidi na zaidi katika kisiwa hichi, ambao watakuwa wasaidizi na viongozi katika sekta mbali mbali, lengo la serikali ni kuona kojani inabadilika na kuwa kojani yenye maendeleo zaidi lakini pia kuona wasomi wa fani mbalo mbali wa...

POLISI NA RAIA MUWE NA MFUMO NA UTARATIBU MZURI WA ULINZI SHIRIKISHI

Image
 HASSAN – ZANZIBAR                                                             25/06/2023 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi MHE, MHANDISI HAMAD YUSSUF MASAUNI amesema kuna haja ya kuwekwa mfumo mzuri wa mashirikiano kati ya Jeshi la Polisi na wananchi katika kutekeleza sera ya Polisi Jamii ili lengo la kuondoa uhalifu katika jamii lifanikiwe. Akizungumza na wananchi wa Jimbo la Bububu, katika Wilaya ya Magharibi A, Mkoa wa Mjini Magharibi amesema japo kuwa yapo mafanikio katika usimamizi wa ulinzi na usalama lakini bado zipo changamoto baina ya pande hizo mbili katika utekelezaji wa ulinzi shirikishi mambo ambayo yanahitaji kurekebishwa. Kamishna wa Polisi Zanzibar CP. HAMAD KHAMIS HAMAD amesema Jeshi la Polisi linaendelea kuchukuwa hatua mbalimbali za kutatua changamoto katika utekelezaji ulinzi shirikishi...

CHANGAMOTO YA MADARASA MBIONI KUPATA UFUMBUZI , WIZARA YAPONGEZA SERIKALI, MAJENGO YA GHOROFA YAENDELEA KUJENGWA KILA KONA ZANZIBAR, MAKAMU WA PILI AFANYA ZIARA KUKAGUA.

Image
AMINA AHMED MOH’D, PEMBA   - 0776859184  MAKAMU  wa Pili wa  rais Hemed Suleiman Abdulla Amefanya ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa Skuli za ghorofa am zinaendelea kujengwa katika maeneo mbali mbali Kusini na Kaskazini mwa kisiwa cha Pemba zilizopo chini ya  wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar.  Akizungmza  kwa nyakati tofauti   Hemed amewataka wasimamizi wa  ujenzi wa skuli hizo kuhakikisha majengo hayo yanakamilika na kukabidhiwa kwa serikali kwa wakati  uliowekwa wa makabidhiano.  Amesema lengo la serikali ni kuondoa  msongamano wa wanafunzi  madarasani kwa kutatuanchangamoto ya  madarasa  hivyo kukamilika kwa wakati majengo hayo kutasaidia kuondoa changamoto hiyo na kuongeza kasi ya ufaulu.  " Niwaombe wasimamizi na wakandarasi mfaanye kazi ikibidi usiku na mchana kwavile vifaa vipo  kuhakikisha majengo haya yanakabidhiwa kwa serikali kwa wakati uliokusudiwa" ....

ZAN MALIPO YADAIWA KUZOROTESHA HUDUMA ZA VYETI VYA KUZALIWA WANANCHI WAIOMBA SERIKALI KULIANGALIA VYEMA SUALA HILI.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA.  BAADHI ya Wazazi wamelalamikia   kukosa huduma zavyeti vya  kuzaiwa vya watoto wao  kwa wakati katika kituo cha  utolewaji wa huduma  hizo wilaya  ya Chake chake  kwa zaidi ya siku 5 kwa  kile wanachojibiwa na watoa huduma kuwa ni  kukosekana kwa huduma ya kimtandao katika ofisi ya wakala wa usajili wa  matukio ya huduma za kijamii.   Wamesema  suala hilo limekuwalikisababisha hasara kwao kutokana na kutoka masafa ya mbali  huku mchezo huo wa nenda rudi   ukikosa 40 kwa zaidi ya siku nne sasa  ambao  wanasema hifu yao ni kucheleweshewa na  baadae kuonhezew malipo katika huduma hiyo kwa kosa la kuchelewesha.  Aidha wanachoendelea kulalamikia baadhi ya wananchi hao  wamesema ni kukosa taarifa maalum juu ya tatizo hilo  ili kuweza kupumzika mpka yatakapokuwa sawa.  Wananchi hao ambao wengi wao ni akina mama na watoto wameiomba Serikali k...

UTAMADUNI WA KUSAMEHEANA WATAJWA KUWA KICHOCHEO CHA VITENDO VYA UDHALILISHAJI TANZANIA.

Image
Na Asha Ahmed Maumivu huwa makubwa sana kwa wahanga na wazee wa wahanga wa vitendo vya udhalilishaji, watoto ambao wanaharibiwa kwa kubakwa na kulawitiwa, lakini mara nyingi huonekana baadhi ya familia kuacha kufuatilia mwenendo wa kesi zao na wengine kuzifuta kabisa.  Wadau wa kupinga vitendo vya udhalilishaji wanasema kuwa utamaduni wa kusameheana na kuoneana muhali ndio husababisha zaidi kutoendelea kwa kesi na hivyo watuhumiwa kuendelea kukaa mitaani na kufanya vitendo vya udhalilishaji kwa watu wengiine. Vitendo vya ukatili dhidi ya watoto, hususan ubakaji na ulawiti, vimekua ni kama janga la taifa hapa nchini, hali ambayo imeendelea kuumiza vichwa vya watendaji wa Serikali, mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGOs), taasisi za dini na wadau wengine juu ya namna gani vitendo hivyo vinaweza kukomeshwa. Kwa mujibu wa takwimu kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, kati ya mwaka 2017 mpaka Mei 2022, Tanzania ilirikodi jumla ya matukio 75,7...

WADAU WAHIMIZA ELIMU YA SAIKOLOJIA KWA WAHANGA WA VITENDO VYA UDHALILISHAJI

Image
NA, MASSOUD JUMA .  SUALA la udhalilishaji wa kijinsia limekuwa likiitia doa sana nchi yetu ya Tanzania, khasa kwa upande wa Zanzibar. Vitendo hivi vya udhalilishaji vimeshika kasi na vinaonekana kukithiri na hasa waathirika wakubwa wakiwa ni watoto na wanawake . Unyanyasaji dhidi ya wanawake na watoto unatajwa kuwa ni jambo la kila siku visiwani hapa, huku asilimia 14 ya wanawake wakiripotiwa kukumbana na vitendo hivi. Vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia vimeripotiwa kuendelea kuongezeka visiwani hapa ambapo Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaonesha kuripotiwa kwa matukio 1,222 mwaka 2021 na kuongezeka hadi matukio 1,360 mwaka 2022, ongezeko ambalo ni la matukio 138. Takwimu hizo zilizotolewa  Januari 2023, zinaonesha kwamba kwenye matukio 1,361 yaliyotokea mwaka 2022, matukio 1,173 yalijumuisha watoto, 185 yalihusu wanawake na matatu yalihusu wanaume ambapo kwenye matukio 1,173 ya watoto, 889 walikuwa ni wasichana, huku 284 walik...

UTAMADUNI WA KUSAMEHEANA WATAJWA KUWA KICHOCHEO CHA VITENDO VYA UDHALILISHAJI TANZANIA.

WADAU WA SHERIA PEMBA WATOA MAONINRASIMU YA SHERIA YA KUANZISHWA MAHAKAMA MAALUMU YA RUSHWA NA UHUJUMU WA UCHUMI.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA.  WADAU wa sheria kutoka Taassisi mbali mbali za Serikali pamoja na taasisi binafsi  kisiwani Pemba  Wameshiriki katika  mkutano maalumu wa kujadili na  kutoa Maoni  katika  rasimu ya sheria ya kuanzishwa mahakama maalum  ya rushwa  na uhujumu uchumi   uliondaliwa na  ofisi ya mwanasheria mkuu Zanzibar   wenye lengo la kuboresha na  kupatikana kwa sheria  bora  itakayosimamia masuala hayo.  Wakitoa maoni yao mara baada ya kufanyiwa mapitio ya rasimu hiyo  baadhi ya wadau hao  akiwemo Muhammed  Ali  Muhammed   kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka,  Simba Khamis Simba  kutoka  kikosi cha kuzuia magendo Zanzibar   (KMKM)  wameiomba kamati  inayosimamia   rasimu hiyo kuongeza Vifungu vya sheria  ambavyo vitaweza kusimamia suala la usafirishaji haram wa magendo ya karafuu, mazao ya b...

KADUARA ATOA AGIZO HILI KWA WATENDAJI WA IDARA ZAKE KUHUSU KUIMARISHA HUDUMA KWA WANANCHI.

Image
NA, FATMA ABRAHMAN, PEMBA.  WAZIRI wa Maji Nishati na Madini Shaibu Hassan Kaduara amezitaka idara zote za serekali kushirikiana kwa pamoja katika kuboresha miundombinu  kwa lengo lakuleta maendeeleo Bora kwa wananchi. Waziri huyo ameyasema hayo wakati akiwa katika ziara yake yakagua miradi ya matangi ya maji ikiwemo la chanjaani , pujini na kendwa kwa lengo la kuangalia miundombinu na kutaka kufahamu changamoto zinazojitokeza katika maeneo hayo . Amesema kwa sasa wananchi hawataki tena maneno bali wanataka vitendo Ili kuona huduma Bora za maendeeleo zinafanikiwa kwa lengo la kuimarisha shuhuli zao huku wakiinua Pato la taifa. Mapema kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya maji zawa Hamad Mussa Rashid amesema serekali Ina nia ya kuboresha huduma ya maji safi na salama mjini na vijijini hivyo kuwataka wananchi kuchangia huduma hio kwa lengo la kumudu gharama za kutatua changamoto mbali mbali zinazoweza kujitokeza . Katika ziara hio waziri kaduwara pia alitembelea visima vya maji vya kiw...

KAMATI YA S JIMBO CHAMBANI YATOA MSAADA WA CHAKULA KWA WANAFUNZI WANAOKAA KAMBI , LENGO KUIMARISHA ELIMU.

Image
Na Fatma  Suleiman, Pemba MWENYEKITI   wa CCM wilaya ya Mkoani Pemba Ali Juma Nassor  amewataka walimu wazee na kamati za Skuli wa skuli za Jimbo la Chambani kuhakikisha wanatoa mashirikiano ya pamoja katika kuwapatia elimu na malezi bora Ili kupata kizazi kinachojielewa na kitakacholeta maslahi endelevu nchini . Mwenyekiti  ameyasema hayo mara baada ya kukabidhi chakula kwa wanafunzi wanaokaa kambi katika Jimbo la chambani mkoani na kusini Pemba. Amesema suala la elimu ni la wote hivyo ni vyema kulifanyia kazi kwa kina katika kuwaandaa ziongozi Bora vya baadae . Aidha amesema Viongozi wao wa Jimbo akiwemo mbunge , Mwakilishi na madiwani wamekua na mchango mkubwa katika kuliinua suala la elimu ndani ya Jimbo Hilo hivyo kuwaomba kuendelea kujitoa kwa ajili Yao Ili kufikia malengo ya serekali ya kuiboresha sekta ya elimu nchini . Akizungumza kwa niaba ya kamati ya Jimbo la chambani mbunge wa Jimbo Hilo Muhammad Abrahman Mwinyi amesema ni vyema walimu kujikita kati...

WAZAZI WAASWA MAADILI YA WATOTO

Image
NA OFISI YA MAKAMU WA  PILI  WAZAZI na walezi wametakiwa kuwasimamia vyema watoto wao katika kuwapatia elimu iliyo bora itakayowasaidia katika maisha yao ya sasa na baadae. Akiwasalimia Waumini wa Masjid Kheir iliyoko Nyamanzi wakati wa Ibada ya Sala ya Ijumaa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amesema ili watoto wafikie lengo la kutafuta elimu jitihada za wazazi zinahitajika ikiwemo kuwafuatilia na kujua mienendo ya watoto hao. Alhajj Hemed ameeleza kuwa Serikali inachukua jitihada mbali mbali katika kuimarisha sekta ya Elimu nchini hivyo, ushirikiano wa wazazi utasaidia kwa kiasi kikubwa watoto kupata elimu kwa urahisi. Ameeleza kuwa Taifa linahitaji wasomi waliobobea katika fani mbali mbali, wenye nidhamu na Maadili mema ambao watasaidia kutoa mawazo ya kuliletea Taifa maendeleo. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema elimu bora inapelekea kupunguza mmong'onyoko wa maadili, vitendo viovu na kusaidia kurejesha hadhi ya Zanzibar i...

WANANCHI WAHIMIZWA KUTUMIA VYANDARUA KWA USAHIHI KUMALIZA MALARIA PEMBA

Image
NA AMINA AHMED MOH’D.        Massoud Suleiman Abdulla, Mkuu kitengo Idara ya Tiba Pemba.  WANANCHI wametakiwa kuvitumia  kwa  Usahihi vyanadarua vinavyotolewa na  na Wizara ya Afya  ili lengo la kumaliza Malaria Zanzibar  liweze kufikiwa. Ametoa  Ombi hilo mkuu wa Idara ya Tiba Massoud Suleiman Abdulla kwa niaba ya Afisa mdhamini wizara ya Afya  Pemba   Khamis Bilali Ali wakati wa mkutano maalumu  wa  kutoa taarifa  kwa wananchi  kupitia waandishi wa habari juu ya hali ya malaria na ufuatiliaji wa ugonjwa huo  kisiwani humo.  Amesema  ili lengo la kumaliza Malaria Zanzibar liweze kufikiwa na kuwa asilimia 0  ni vyrma wananchi kufuata taratibu zilizowekwa  juu ya matumizi sahihi ya vyandarua vinavyoendelea kutolewa bure kwa mama wajawazito na watoto wanapofika hospitali. "Serikali inafanya kila jitihada kuona hiyo asilimia 0.4  ya ugonjwa wa Malaria uliopo i...

WAKULIMA WA MBOGA A MBOGA PEMBA WAPEWA ELIMU JUU YA KUTAMBUA UDONGO WENYE AFYA KWA KILIMO, LENGO KUPATA TIJA NA MAENDELEO

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA.  ZAIDI ya Wakulima 120  wa Mboga mboga na Matunda   Kutoka maeneo mbali mbali ya  kisiwa cha Pemba  wamepatiwa mafunzo maalumu   juu ya Afya Bora ya Udongo  na usimamizi Wa rutuba kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Zanzibar.  Akitoa elimu   elekezi  katika mafunzo hayo mkuu wa division ya Utafiti wa udongo na mimea  Zanzibar Ali Hamad Ali alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni  kuwasaidia  wakulima kuweza kuchunguza  afya ya Udongo kabla ya kulima mazao yao  kuepuka hasara na kujipatia faida kupitia kilimo chao.   "Udongo ndio tegemeo kubwa la wakulima katika masuala ya kilimo tumeona ni vyema kufikisha elimu hii kwa wakulima   kutokana na waliowengi kukosa elimu hii na kupata hasara mbali mbali ikiwemo mazao kuharibika pamoja na miche" . Alisema  Kutokana na wakulima wengi kuendelea kutumia mashamba ambayo yalishatumika  kwa muda mr...