SERIKALI YAAHIDI KUKIFUNGUA ZAIDI KISIWA CHA KOJANI KWA KUTATUA CHANGAMOTO MBALI MBALI ZINAZORUDISHA NYUMA MAENDELEO KISIWANI HUMO.

NA AMINA AHMED MOH'D, PEMBA



ZIARA ya makamu wa pili wa rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla kuendelea kukagua  ujenzi wa skuli za ghorofa maeneo mbali mbali kisiwani Pemba leo   hii imefika katika  wilaya ndogo ya Kojani mkoa wa kaskazini kukagua mradi  huo pamoja  kuzungumza na wananchi na kuweza kusikiliza changamoto zinazowakabili .  

Akizungumza na wanachi katika  kijiji cha Kipata  Kojani    eneo ambalo linajengwa skuli hiyo kwajili ya Wanafunzi wa Msingi  makamu huyo amesema  kuwa  serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuboresha maenedeleo ya elimu kisiwani humo  ili kupata Viongozi bora watakoasimamia taifa katika nyanja mbali mbali.
 
 " Tunataka tutoe wasomi zaidi na zaidi katika kisiwa hichi, ambao watakuwa wasaidizi na viongozi katika sekta mbali mbali, lengo la serikali ni kuona kojani inabadilika na kuwa kojani yenye maendeleo zaidi lakini pia kuona wasomi wa fani mbalo mbali wanaendelea kutoka huku   . 

  Aidha Makamu huyo amewataka wanachi wa kojani kutoa mashirikiano  kwa wasimamizi wa jengo hilo ili kuona linakamlika kwa wakati  lna kuanza kutumiwa na wanachi. 

 Katika hatua nyengine  makamu  huyo amesema serikali itaendelea kulipatia ufumbuzi   suala la kituo cha afya  ambacho kwa sasa hakikidhi mahitaji  kwa wananchi kisiwani humo   kutokana na udogo wake. 

 "Salam  kutoka kwa  mh rais kaniambia serikali ipo mbioni  kuzipatia ufumbuzi changamoto zote zinazorudisha nyuma maendeleo ya kojani  ikiwemo kuongeza kituo cha Afya amabacho kitasaidia wananchi kuondoa changamoto zinazowakabili". 

 "Jumla ya shilingi bilioni 20 mh rais ameshazitenga kwajili ya kuleta maendeleo ikiwemo kisiwa cha kojani  maendeleo ya elimu, afya maji na mengineyo, na ifikapo 2030 kojani itakuwa kojani nyengine. 

 Sambamba na hayo Hemed amewataka wananchi kuendelea kuhamasishana  maendeleo na kuacha mambo yasio na maana yanayirudisha nyuma  harakati za kufikiamaendeleo. 

 Awali akizungumza   katika mkutano huo waziri wa elimu na mafunzo ya amali  Zanzibar leila  Muhammed Mussa amesema utakapokamilika ujenzi wa ghorofa hiyo  kutasaidia    kutatua changamoto ya uhaba wa madarasa kisiwani humo na kuwaondoshea usumbufu. 

" Miongoni mwa  changamoto kubwa  katika elimu kisiwa cha Kojani ilikuwa ni skuli ya msingi kutokana na  iliyopo kuwa haikidhi  matakwa    ya    wanafunzi,  ni wengi madarasa hayatoshi kukamilika kwa ujenzi kutasaidia kuondoa changamoto hiyo. 


 Kwa Upande wake mkandarasi wa kampuni  hiyo  Sinic construction  Hawa Abdalla Said amesema   itasimamia ujenzi huo kukamilika  mapema kabla ya muda uliowekwa  kwa ubora. 


 Mwisho 

 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI