CHANGAMOTO YA MADARASA MBIONI KUPATA UFUMBUZI , WIZARA YAPONGEZA SERIKALI, MAJENGO YA GHOROFA YAENDELEA KUJENGWA KILA KONA ZANZIBAR, MAKAMU WA PILI AFANYA ZIARA KUKAGUA.

AMINA AHMED MOH’D, PEMBA   - 0776859184 

MAKAMU  wa Pili wa  rais Hemed Suleiman Abdulla Amefanya ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa Skuli za ghorofa am zinaendelea kujengwa katika maeneo mbali mbali Kusini na Kaskazini mwa kisiwa cha Pemba zilizopo chini ya  wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar.

 Akizungmza  kwa nyakati tofauti   Hemed amewataka wasimamizi wa  ujenzi wa skuli hizo kuhakikisha majengo hayo yanakamilika na kukabidhiwa kwa serikali kwa wakati  uliowekwa wa makabidhiano.

 Amesema lengo la serikali ni kuondoa  msongamano wa wanafunzi  madarasani kwa kutatuanchangamoto ya  madarasa  hivyo kukamilika kwa wakati majengo hayo kutasaidia kuondoa changamoto hiyo na kuongeza kasi ya ufaulu. 

" Niwaombe wasimamizi na wakandarasi mfaanye kazi ikibidi usiku na mchana kwavile vifaa vipo  kuhakikisha majengo haya yanakabidhiwa kwa serikali kwa wakati uliokusudiwa" . 

"Dhamira ya serikali ni kuona majengo haya yanakabidhiwa yakiwa yamekamilika   mwishoni mwa mwezi  wa mwaka huu  na mengine mwanzoni mwa mwaka 2024". 


 "Nia njema ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  ni kuona kila mwananchi anafurahia maendeleo   mh rais anataka kuona  changamoto ya madarasa  inamalizika kabisa  ndio mana  akaona ipo haja  ya kujenga majengo nane ya skuli za ghorofa ambazo zitakuwa na vyumba visivyopungua 40  na tutaendelea ili kuona wanafunzi wanasoma bila usumbufu na kupata matokeo mazuri".
 
Katika hatua nyengine Hemed amewataka wakandarasi na washauri elekezi kutoa fursa za ajira za muda zinazopatikana katika ujenzi wa majengo hayo kwa wazawa ili kuweza kunufaika "

 Akizungumza katika ziara hiyo waziri wa elimu na mafunzo ya amali Zanzibar Leila Muhammed Mussa ameishukuru serikali ya awamu ya nane  kwa kusimamia  vyema changamoto za elimu ikiwemo uhaba wa madarasa. 

" Baada ya  kuona  bado kuna changamoto ya uhaba wa madarasa  kwa wanafunzi wetu wizara ya elimu tulipeleka ombi kwa mh rais tunashukuru hakusema tusubiri wahisani alisema tutatatua changamoto hii sisi wejyeqe serikali na ni kweli tunaona majengo haya yakiendelea kila kona tunatoanpongezi zeru za dhati "
 
" Tunashukuru Kupitia fedha za serikali wizara ya elimu imepata majengo kama haya yanaoyoendelea ujenzi wake kila kona   8 kwa kwa hapa kisiwani Pemba lakini 13 kwankisiwani unguja ambayo ni sawa na 21 ni hatua kubwa sana".

 Jumla ya majengo sita   ya skuli za ghorofa yanayoendelea  ujenzi wake zimetembelewa  kupitia ziara hiyo ikiwemo  Mwambe, Kiwani, Michakaeni, Ole, Utaani, Konde Pamoja na Maziwa ngombe Micheweni ambapo changamoto  zilizobainika katika ujenzi huo wkamadarasi wameahidi kuzifanyia kazi  huku  zinazohusu serikali makamu huyo akiahidi kuzipatia ufumbuzi ikiwemo ujenzi wa barabara ya ndani  skuli mpya ya Mwambe. 

Mwisho 
 


 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI