Posts

Showing posts from November, 2023

WIZARA YA AFYA PEMBA YATOA NENO KWA WANAOSAMBAZA UVUMI KUHUSU MAGONJWA YA MIRIPUKO.

Image
NA AMINA AHMED MOH'D, PEMBA.  WIZARA ya Afya Zanzibar imewataka  waandishi wa habari pamoja na wahudumu wa Afya ya jamii CHV kungana  pamoja  katika kuiweka salama jamii  juu ya majanga ya miripuko  mbali mbali  kwa kuelimisha na kutoa taarifa  kutoka kwa  vyanzo vyenye usahihi  ili kuepusha mitafaruku inayowapata wananchi kutokana na uvumi hususan katika msimu wa mvua zinazoendelea  kunyesha.   Kauli hiyo imetolewa na  Afisa Mdhamini Wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali alipokuwa  akizungumza na baadhi ya wanahabari   wa vyombo mbali mbali pamoja na wahudumu wa Afya jamii CHV kiswani Pemba  katika mafunzo maalumu juu ya kudhibiti kusambaa kwa uvumi na maneno mbali mbali katika vipindi vya majanga  huko Samail Gombani Chake.  Amesema  makundi hayo yanayonafasi kubwa katika kusaidia jamii kuwa na uwelewa wa kutofautisha uvumi   na taarifa potofu kwa kuweka usah...

WAANDIKISHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WAASWA UADILIFU.

Image
Amina Ahmed Moh’d Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC  inaendelea na mafunzo ya siku mbili   kwa Wakuu wa vituo na Makarani  wapya waliochaguliwa kusimamia  zoezi la uandikishaji wa daftari la wapiga kura wapya  linalotarajiwa kuanza rasmi  tarehe tarehe 2 /12/ mwaka 2023 kwa awamu ya kwanza katika wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Mpango huo wa matayarisho ya uendelezaji wa  uandikishaji wa daftari la  kudumu la wapiga kura kwa wapiga kura wapya wapya kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2025 ni miongoni mwa utekelezaji wa majukumu ya msingi  ya Tume ya Uchaguzi.  Akizungumza na  na watendaji hao  mkuu  wa kurugenzi ya mifumo ya uchaguzi Tume ya Uchaguzi Zanzibar  ZEC  Mwanakombo Machano Abuu  amewataka kufanya kazi hiyo kwa mujibu wa haki   na malengo yaliokusudiwa.  Amesema  watendaji wanapaswa kutambua kuwa jukumu hilo wanalokwenda kulisimamia ni jukumu la kitaifa linalohitaji ...

UDHALILISHAJI UNAVYOSABASISHA WATOTO KUATHIRIKA KISAIKOLOJIA KATIKA JAMII HAPA ZANZIBAR

Image
  NA SALMA AMOUR, UNGUJA.  KWA MIAKA mingi, tunashuhudia watoto ndio waathirika wakubwa wa vitendo cya ukatil wa kijinsia, hali inayoleta taswira ya kupata idadi kubwa ya watoto walioatharika kisaikolojia kwenye Jamii na hata katika Taifa Kwa ujumla    Wataalamu wa afya ya akili wamekiri kuwa, tatizo la udhalilishaji kwa watoto linaweza kusababishia msongo wa mawazo hivyo kukabiliwa na tatizo la afya ya akili. Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar ni moja ya taasisi inayotoa elimu ya saikolojia kwa familia zinazokabiliwa na tatizo la udhalilishaji wa kijinsia.   Kwa mujibu wa takwimu kutoka mtatwimu mkuu wa serikali takwimu za ukatili na udhalilisha wa kijinsia hutoa taarifa za idadi ya matukio yaliyotolewa aina ya waathirika na hali ya waathirika Baada ya ukatili na udhalilisha wa kijinsia muda wa matukio yalipotokea na wafanyakazi wa matukio.takwimu hizo hutoa taarifa  kuhusu matukio amvbayo yameainishwa . Idadi ya watoto w...

TRA MKOA WA KIKODI PEMBA WATAKIWA KUONGEZA VYANZO VIPYA VYA UKUSANYAJI WA MAPATO KISIWANI HUMO .

Image
NA - AMINA AHMED MOH’D PEMBA.  NAIBU waziri wizara ya Fedha Tanzania Hamad Hassan Chande ameitaka mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa kikodi Pemba kufanya utafiti utakaosaidia kupata vyanzo  vipya vya mapato sambamba na kuzidisha uimarishaji wa mifumo ya ulipaji wa kodi mbali mbali zinazokusanywa na mamlaka hiyo .  Ameyasema hayo  alipokuwa akizungumza na watendaji wa mamlaka hiyo, viongozi  wananchi, taasisi za serikali na binafsi  katika   kilele cha maadhimisho ya wiki ya  kurejesha shukurani kwa walipa kodi  iliyoandaliwa na mamlaka hiyo mkoa wa kikodi Pemba katika ukumbi wa Sun set Wesha Nje kidogo na mji wa Chake Chake. Amesema licha ya kuvuka malengo ya makusanyo   yaliowekwa na mamlaka hiyo mkoa wa kikodi Pemba ipo haja ya kufanya utafiti maalumu wa kuongeza vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitasaidia kuongeza  kodi zitakazotumika kwajili  ya kuleta  zaidi maendeleo nchini, pamoja na kuweka  mifumo...

TRA MKOA WA KIKODI YATOA MSAADA WA VIFAA HOSPITALI YA WILAYA KINYASINI WETE, WIZARA YATOA UJUMBE HUU.

Image
NA- AMINA AHMED, PEMBA. minnah1202@gmail. com.  KAMISHNA wa Mamlaka ya  Mapato Tanzania TRA amewataka wananchi kisiwani Pemba Kuendeleza harakati za ulipaji  wa kodi ili kuisaidia serikali kutekeleza miradi  mbali mbali  itakayitumiwa kwa na wananchi pamoja na kusaidia kutekeleza huduma nyengine muhimu za kijamii.         Wito  wa kamishna wa mamlaka hiyo umetolewa kwa niaba yake na  kaimu naibu kamishna wa huduma za kiufundi   wa mamlaka hiyo Venance alipokuwa akizungumza na wananchi pamoja na watendaji wa hospitali ya wilaya  kinyasini Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba  katika Ghaflaya kukabidhi vifaa tiba pamoja na Dawa kwa hospitali hiyo ikiwa ni muendelezo wa wiki ya kurejesha shukurani kwa mlipa kodi . Amesema iwapo wananchi wataendelea kuwajibika  ipasavyo katika ulipaji kodi malengo yaliyowekwa na serikali  ya utowaji wa huduma bora kwa wananchi yataweza kufikiwa.  Aidha ...

DC WETE ATOA NENO HILI KWA MAMLAKA YA MAPATO TRA MKOA WA KIKODI PEMBA.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA.        0776 859184    MAMLAKA ya Mapato Tanzania  TRA imetakiwa kuandaa  mifumo imara  itakayosaidia kuongeza uelewa kwa wananchi  kisiwanibPemba  juu ya usahihi wa ulipaji kodi zinazokusanywa na mamlaka hiyo .  Kauli hiyo ya mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib iliyotolewa kwa niaba yake na  mkuu wa  wilaya ya Wete  Hamad Omar Bakari   alipokuwa akizungumza na watendaji, na wafanya kazi wa mamlaka hiyo mkoa wa kikodi Pemba  mara baada ya kumalizika ghafla ya ufunguzi wa ofisi za mamlaka hiyo Wete  mapema Leo.  Amesema bado ni wananchi wachache     hususan ni kisiwani Pemba ambao wanauelewa wa kutosha juu ya kulipa kodi kwa mamlaka hiyo na wengine kukwepa kwa makusudi kutokana na kutokuwepo kwa mifumo imara ya ukusanyaji wa kodi  jambo ambalo hupelekea kukosekana kwa mapato  ambayo yangeongeza ufanisi katika...

WANANCHI KISIWANI PEMBA WAASWA KUENDELEZA MASHIRIKIANO NA TRA KATIKA KULIPA KODI KWA HIARI.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA.  WANANCHI  kisiwani Pemba  wametakiwa kuzidisha mashirikiano  katika  ulipaji wa kodi  kwa hiari mbali mbali   ili ziweze kutumika   katika shughuli za maendeleo ikiwemo uimarishaji wa huduma za afya ,elimu miundo mbinu na shughuli nyengine  za kijamii.            ABDALLA RASHID ALI - DC, CHAKE CHAKE.   Ametoa wito huo mkuu wa wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali   kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Matter Mahor Massoud alipokuwa akizungumza na wananchi huko katika uwanja wa gombani mara baada ya kumaliza   matembezi maalum yalioandaliwa na mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa kikodi kisiwani humo yalioanzia uwanja  wa Tibirinzi  ikiwa ni wiki maalum ya kurejesha shukurani kwa walipa kodi  . Amesema    kodi zote zinazokusanywa n...

CHUO CHA UFUNDI WENI NI FURSA KWA VIJANA KUJIAJIRI YOTE NI MATUNDA YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Image
  NA THUREYA GHALIB, PEMBA.  Wakwezi na Wakulima ,hapo walipokutana ,maneno waliyosema ,tutashindaa kwa nguvu zake karima,hii ni wimbo maarufu sana ya mashujaa wetu wa Mapinduzi ambao hautaweza kusahaulika katika akili za Mzalendo na Mpenzi wa Nchi  yake ya Zanzibar. Wimboo huu unakumbusha jinsi mashujaa walivojipanga na kufanya mapinduzi huku wakiwa na ujasiri wa hali ya juu huku wakielekeza matumaini yao kwa Mungu na kuamini Mapinduzi watashinda lazima.   Mapinduzi ya Zanzibar yalitokea mwaka 1964 ili kumuondoa madarakani Sultani wa Zanzibar na serikali yake, iliyoundwa hasa na Waarabu, na hatimaye kuweka uongozi mikononi mwa Waafrika chini ya Kiongozi wake Rais wa Kwanza wa Zanzibar Jemedar Hayati Abedi Amani Karume. Kwa mujibu wa historia zinasema haikuwa kazi rahisi kufanyika kwa mapinduzi hayo,zilitumika jitihada kubwa na mioyo ya kizalendo hadi kufanikisha azma yao . Wazanzibar  waliteswa na kunyanyaswa huku wakinyimwa haki zao muhimu ikiwemo ...

VIONGOZI CHUO CHA AMALI WAASWA MASHIRIKIANO KUTATUA CHANGAMOTO MBALI MBALI.

Image
Na, Thureya Ghalib - PEMBA.                               UONGOZI wa Chuo cha amali vitongoji umetakiwa kutoa mashirikiano kwa Kamati ya ushauri wa Chuo hicho katika kufanya mamuzi sahihi na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili . Wito huo  umetolewa Mratibu wa chuo cha mafunzo ya amali Pemba Othaman Said Othaman Kwa niaba ya Ofisa Mdhamini Wizara ya Elimu Na mafunzo ya mali katika uzinduzi wa Kamati  hio  Vitongoji Wilaya ya Chake Mkoa wa Kusini Pemba Alisema ni vyema Kamati hio wakaitumia  vizuri kwa kupokea na kusikiliza  ushauri utakaojadiliwa katika vikao vya kamati hio  na kuifanyia kazi katika  kuleta mafanikio na kukizogeza mbele chuo hicho . "Kutokana na Nafasi zenu mulizonazo nina uhakika muna uwezo mkubwa wa kusaidia kutatua changamoto na kufanya maamuzi yaliyo sahihi " Alisema Mratibu huyo . Aidha ame...

CHANGAMOTO YA ULIPWAJI WA FIDIA KWA WAHANGA WA UDHALILISHAJI BADO TATIZO SUGU

Image
NA THUREYA GHALIB PEMBA. KUNA Msemo usemao Adhabu ya kaburi aijuaje maiti  huu ni msemo unaofahamisha kuwa aliyefikwa na shida fulani ndiye  anaejua na kufahamu shida ya ilo jambo. Au pia  kuna usemao unasema  aisifuye mvua imemnyeshea,msemo huu unamana kuwa  kila jambo ambalo mtu analizingumzia atakuwa aidha  ana uzoefu nalo au kwa namna moja au nyengine analifahamu.  Hii ni misemo inayonesha ni jisi gani Mtu anapopata matatizo unatakiwa umskilize na kumpa faraja maana yeye ndie mtu pekee anaehisi uchungu wa Jambo hilo. Leo Katika Makala haya nimelenga kuzungumzia ni kwa namna Gani ukosekanaji wa Fidia  kwa Wahanga wa Kesi za udhalilishaji unavosokota mioyo yao .                                               ...

UHABA MAAFISA USTAWI JAMII WALALAMIKIWA WADAU WALIA NA SERIKALI.

Image
NA AMINA AHMED MOH'D PEMBA.  WADAU wa kupinga vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kisiwani Pemba Wameiomba  Serikali kuongeza idadi ya maafisa ustawi jamii  katika wilaya  ili kusaidia kuongeza kasi ya kupambana na changamotoza  vitendo vya Udhalilishaji wa kijinsia kwa watoto.  Wakizungumza kwa nyakati  tofauti baadhi ya wadau hao wamesema kuwa kutokana na uhitaji wa watu hao katika kusaidia kupambana  na vitendo hivyo  utaratibu wa Afisa mmoja katika kila wilaya ni miongoni mwa changamoto  inayopelekea  kuongezeka kwa changamoto katika kesi za udhalilishaji. "Wilaya  mfano wilaya ya mkoani ina  shehia 32 ambazo shehia zote hizo vitendo na kadhia za udhalilishaji kwa watoto zinajitokeza  Afisa mmoja tu ndie analazimika kushuhulika  haisaidii kuondoa changamoto", Fathiya Mussa Said.   Serikali iliangalie suala hili kuona kwamba ipo haja ya kuongeza idadi ya hawa watu katika wilaya ikiwezekana iwaweke...

WADAU WA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA WALIA NA UFANISI WA VITUO VYA MKONO KWA MKONO PEMBA.

Image
NA AMINA AHMED MOH'D PEMBA.  UHABA wa wafanya kazi ni miongoni mwa changamoto kubwa inayovikabili vituo vya mkono kwa mkono kisiwani Pemba jambo ambalo hupelekea kupungua kwa ufanisi wa vituo hivyo ambavyo kazi yake kubwa ni kusaidia kwa kiasi kikubwa mapambano dhidi ya vitendo vya udhalilishaji kwa watoto na wanawake katika kusaidia kupatikana kwa ushahidi wa moja kwa moja.  Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wadau wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji  kisiwani Pemba wamesema  miongoni mwa changamoto walizozibaini ni kutokuwepo kwa idadi kubwa  ya watendaji katika Vituo hivyo  jambo ambalo hupelekea kurudisha nyuma mapambano dhidi vitendo hivyo. Fat hiya Mussa Said Mratibu wa Tamwa Zanzibar kwa upande wa kisiwani Pemba  alisema kuwa  huenda hakuna usimamizi  wa vituo vya mkono kwa mkono  jambo ambalo hupelekea kupungua kasi ya ufanisi katika vituo hivyo. "Tulio wengi katika taasisi tumezoea  kusimamiwa ndio...