DC WETE ATOA NENO HILI KWA MAMLAKA YA MAPATO TRA MKOA WA KIKODI PEMBA.

NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA.        0776 859184 


 MAMLAKA ya Mapato Tanzania  TRA imetakiwa kuandaa  mifumo imara  itakayosaidia kuongeza uelewa kwa wananchi  kisiwanibPemba  juu ya usahihi wa ulipaji kodi zinazokusanywa na mamlaka hiyo . 

Kauli hiyo ya mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib iliyotolewa kwa niaba yake na  mkuu wa  wilaya ya Wete  Hamad Omar Bakari   alipokuwa akizungumza na watendaji, na wafanya kazi wa mamlaka hiyo mkoa wa kikodi Pemba  mara baada ya kumalizika ghafla ya ufunguzi wa ofisi za mamlaka hiyo Wete  mapema Leo.

 Amesema bado ni wananchi wachache     hususan ni kisiwani Pemba ambao wanauelewa wa kutosha juu ya kulipa kodi kwa mamlaka hiyo na wengine kukwepa kwa makusudi kutokana na kutokuwepo kwa mifumo imara ya ukusanyaji wa kodi  jambo ambalo hupelekea kukosekana kwa mapato  ambayo yangeongeza ufanisi katika uimarishaji wa huduma mbali mbali za maendeleo. 

" Hayo  yote yataweza kutusadia kupiga hatua kubwa za kimaendeeo, iwapo mfumo  utaimarishwa  na elimu itatolewa kwa wananchi bado uhitaji wa mambo haya mawili hususan ni huku kisiwani Pemba yanahitajika " Alisema Hamad. 

Aidha amewataka wananchi  kuendeleza  uzalendo wa nchi kwa  kulipa kodi  kwa maslahi ya taifa  na kuongeza  zaidi maendeleo yanayoendelea kuletwa na viongozi wa nchi. 

" Nchi zote zilizoendelea wananchi ndio wanaolipa kodi wala hawazikwepi kadhalika na sisi tumuunge mkono rais wetu wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan lakini na Rais wetu Dk hussein Ali Mwinyi katika kulipa kodi kwa mamlaka zilizopewa dhamana ya kukusanya kodi ambazo ndizo ambazo zinatumika kwajili ya maendeleo mbali mbali".

 Akizungumza kwa niaba ya  kamishna mkuu wa TRA  Kaimu Naibu Kamishna wa huduma za  kiufundi  wa mamlaka  hiyo Venance Mshana   amesema kuwa   Kwa kipindi cha mwaka 2022 mamlaka hiyo imeupandisha Pemba   hadhi  kikodi  na  kuwa mkoa rasmi  wa kikodi   lengo  ni kusaidia kuongeza usimamizi    wa masuala yite yanayohusu kodi mbali mbali kuweza kufanyiwa kazi  bila usumbufu woqote wa kuzifata nje ya kisiwa hicho. 

Nae kwa upande wake Meneja wa  Mkoa kikodi Pemba Arif  Said  Amesema kuwa  dhamira ya kufungua ofisi hiyo kwa upande wa kaskazini Pemba ni  kusogeza karibu huduma za kikodi kwa wananchi ambao  awali walikuwa wanazifuata huduma hizo ofisi kuu  ya mkoa iliyopo Chake Mkoa Kusini  Pemba. 
 Ufunguzi wa ofisi hiyo ya  TRA wilaya ya Wete  imeambatana na burudani mbali mbali ikiwemo musiki wa kizazi kipya pamoja na ngoma ya msewe kutoka kambini kichokochwe. 
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI