WANANCHI KISIWANI PEMBA WAASWA KUENDELEZA MASHIRIKIANO NA TRA KATIKA KULIPA KODI KWA HIARI.


NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA. 

WANANCHI  kisiwani Pemba  wametakiwa kuzidisha mashirikiano  katika  ulipaji wa kodi  kwa hiari mbali mbali   ili ziweze kutumika   katika shughuli za maendeleo ikiwemo uimarishaji wa huduma za afya ,elimu miundo mbinu na shughuli nyengine  za kijamii.
           ABDALLA RASHID ALI - DC, CHAKE CHAKE. 

 Ametoa wito huo mkuu wa wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid Ali   kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Matter Mahor Massoud alipokuwa akizungumza na wananchi huko katika uwanja wa gombani mara baada ya kumaliza   matembezi maalum yalioandaliwa na mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa kikodi kisiwani humo yalioanzia uwanja  wa Tibirinzi  ikiwa ni wiki maalum ya kurejesha shukurani kwa walipa kodi  .


Amesema    kodi zote zinazokusanywa na mamlaka  hiyo kwa upande wa Zanzibar Pamoja na mamlaka ya mapato Zanzibar   hutumika  kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa taifa  na kuondoa changamoto za kukosekana kwa huduma  muhimu  kwa jamii.

‘’ Tuendelee kushirikiana na mamlaka hii  ambayo imewekwa maalum katika kuisaidia serikali  na kuweza kupatikana mapato ambayo yatasaidia kuimarisha huduma  za  kijamii, kwani kwa  sasa serikali yetu haitegemei sana misaada kutoka  nje  kwa sasa tunategemea kodi zetu za ndani ambazo zinatolewa na wananchi‘’ .

Aidha mkuu huyo ameishukuru mamlaka hiyo kwa kuonesha uzalendo wa kurejesha shukurani kwa wananchi  ambapo amesema  kitendo hicho kitasaidia kuongeza hamasa kwa  jamii juu ya ulipaji wa kodi .

‘’ Walipaji kodi kwetu ni watu muhimu sana  katika kujenga   nchi  hivyo  kitendo hiki cha kurejesha  shukurani kwa kutoa misaada ya ujenzi na vifaa katika sekta mbali mbali  kutasaidia kuongeza hmasa kwa jamii  juu ya kulipa kodi  ‘’ alisema  mkuu huyo .

 Akizungumza  kaimu meneja wa mamlaka ya mapato Tanzania TRA  mkoa wa kikodi Pemba  Sleiman Nuhu  Sleiman amesema  lengo la kuandaa wiki maalum kwajili yamlipa kodi ni  kurudisha shukrani kwa wananchi pamoja na kuirudisha kodi hiyo  katika jamii .

 SLEIMAN NUHU  SLEIMAN, KAIMU MENEJA TRA PEMBA 

‘’ Kila ifikapo  mwezi wa 11 ni kawaida kwa mamlaka ya mapato  kuandaa wiki maalum kwajili ya  mlipa  kodi ikiwemo kugawa zawadi kwa waliofanya vizuri katika ulipaji kodi ,kujenga majengo na miundombinu ambay mazoezi kutoka maeneo mbali mbali ,viongozi wa serikali wafanya kazi  pamoja na watendaji wa TRA   meneja msaidizi  forodha mkoa wa kikodi  Pemba  Sleiman Abdalla Said  amesema mamlaka hiyo itaendelea kushirikiana na kuwa karibu na wananchi na kuifikia jamii  katika kutatua changamoto mbali mbali .kisiwani humo.


Wiki hiyo ya kurejesha shukurani kwa walipa kodi  Pamoja na bonanza hilo  pia  itaadhimisha wiki hiyo kwa kutoa msaada wa vifaa kwajili ya skuli ya Michenzani wilaya ya Mkoani, ufunguzi wa jengo la  ofisi ya TRA kaskazini, Pamoja na kutoa zawadi kwa washindi mbali mbali waliofanya vizuri katika ulipaji wa kodi  ambapo kauli mbiu ya wiki hiyo ni  ‘’Kodi Yetu Maendeleo yetu   Tuwajibike’’.


Mwisho.

 

 

 

 


Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI