TRA MKOA WA KIKODI PEMBA WATAKIWA KUONGEZA VYANZO VIPYA VYA UKUSANYAJI WA MAPATO KISIWANI HUMO .

NA - AMINA AHMED MOH’D PEMBA. 


NAIBU waziri wizara ya Fedha Tanzania Hamad Hassan Chande ameitaka mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa kikodi Pemba kufanya utafiti utakaosaidia kupata vyanzo  vipya vya mapato sambamba na kuzidisha uimarishaji wa mifumo ya ulipaji wa kodi mbali mbali zinazokusanywa na mamlaka hiyo .

 Ameyasema hayo  alipokuwa akizungumza na watendaji wa mamlaka hiyo, viongozi  wananchi, taasisi za serikali na binafsi  katika   kilele cha maadhimisho ya wiki ya  kurejesha shukurani kwa walipa kodi  iliyoandaliwa na mamlaka hiyo mkoa wa kikodi Pemba katika ukumbi wa Sun set Wesha Nje kidogo na mji wa Chake Chake.


Amesema licha ya kuvuka malengo ya makusanyo   yaliowekwa na mamlaka hiyo mkoa wa kikodi Pemba ipo haja ya kufanya utafiti maalumu wa kuongeza vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitasaidia kuongeza  kodi zitakazotumika kwajili  ya kuleta  zaidi maendeleo nchini, pamoja na kuweka  mifumo imara itakayosaidia walipa kodi kudai risiti za kielectoniki. 

Aidha  naibu huyo  amewataka watendaji wa mamlaka hiyo kuendelea kushirikiana na   taasisi, serikali pamoja na wananchi katika kuhakikisha wanaendelea  kufanya kazi ya ukusanyaji wa mapato bila kutumia  mabavu, wala kugombana na walipa kodi  wao ambao ni wananchi. 

Akizungumza  katika kilele hicho  kwa niaba ya kamishna wa TRA Tanzania meneja wa TRA  Zanzibar Saleh Haji Pandu amesema kuwa  kuvuka kwa malengo ya makusanyo mkoa wa kikodi Pemba kumetokana na kuongezeka hamasa  kwa wananchi ambao ni walipa kodi  ambapo amesema mamlaka hiyo  itaendelea kuiunga mkono serikali na kuonesha mafanikio ya kikazi kwa mamlaka hiyo katika makusanyo mbali mbali. 

 Nae kwa upande wake Meneja wa TRA  mkoa wa kikodi Pemba  Arif Said Amesema  kuwa mamlaka mkoa huo itaendelea kuhamasisha jamii ikiwa ni pamoja na kutoa elimu juu ya kodi kwa  kuzitumia fursa  mbali mbali. 

  Akitoa salam za mkoa wa Kusini na Kaskazini Pemba Mkuu wa mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud Ameipongeza mamlaka hiyo ya TRA kwa kuendelea kuisaidia serikali  kukusanya  kodi  kwa kutumia busara  bila kuwasumbua walipa kodi  ambao ni wananchi kwa namna yeyite ile ambapo amesema TRA mkoa wa kikodi Pemba ni miongoni mwa mamlaka pekee ambayo haijawahi  kulalamikiwa na wananchi  katika utendaji kazi wake. 

 Aidha Mattar amezitaka taasisi nyengine  kuiga mfano huo wa TRA katika kukusanya mapato kwajili ya maendeleo ya nchi bila kutumia nguvu  sambamba  na kukusanya kodi kwa misingi ya kistaarabu  kama inavyoelekezwa na viongozi wa nchi akiwemo Dk Samia Suluhu Hassan pamoja na Hussein Ali Mwinyi  rais wa Zanzibar ili kufikia malengo yaliokusudiwa. 

Katika kilele hicho  Naibu waziri huyo pia Alikabidhi zawadi  kwa walipa kodi waliofanya vizuri  mwaka 2023  huku Mamlaka hiyo mkoa wa kikodi Pemba ikiwa imevuuka lengo la makusanyo ya kodi na kufikia asilimia 100. 9 ukilinganisha na mwaka uliopita. 

Mwisho

 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI