WAANDIKISHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA WAASWA UADILIFU.


Amina Ahmed Moh’d

Tume ya Uchaguzi Zanzibar ZEC  inaendelea na mafunzo ya siku mbili   kwa Wakuu wa vituo na Makarani  wapya waliochaguliwa kusimamia  zoezi la uandikishaji wa daftari la wapiga kura wapya  linalotarajiwa kuanza rasmi  tarehe tarehe 2 /12/ mwaka 2023 kwa awamu ya kwanza katika wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Mpango huo wa matayarisho ya uendelezaji wa  uandikishaji wa daftari la  kudumu la wapiga kura kwa wapiga kura wapya wapya kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2025 ni miongoni mwa utekelezaji wa majukumu ya msingi  ya Tume ya Uchaguzi. 

Akizungumza na  na watendaji hao  mkuu  wa kurugenzi ya mifumo ya uchaguzi Tume ya Uchaguzi Zanzibar  ZEC  Mwanakombo Machano Abuu  amewataka kufanya kazi hiyo kwa mujibu wa haki   na malengo yaliokusudiwa.
 Amesema  watendaji wanapaswa kutambua kuwa jukumu hilo wanalokwenda kulisimamia ni jukumu la kitaifa linalohitaji kuendeshwa kwa uweledi  na kutimiza malengo ya  taifa kupitia mfumo wa kidemocrasia. 

"Zoezi la uandikishaji halihitaji ushabiki wa kisiasa, niwaombe sana  jiepusheni kushabikia vyama wakati wa uandikishaji kwani kufanya hivyo kutaweza kupelekea kutia dosari zoezi zima la uandikishaji, niwatake kila mmoja wenu aelekeze akili yake katika kazi hiyo  kwa kuzingatia haki   na sheria bila kujali mtu anatokea chama gani". 

 
Aidha amewataka kutoa vipaumbele kwa watu wenye mahitaji maalum ikiwemo wazee, wajawazito, watu wenyw ulemavu , ili kuweza kuipata haki hiyo bila usumbufu. 
 
 Nae kwa upande wake mkuu wa wakurugenzi huduma kwa wapiga kura kutoka Tume ya Uchaguzi Salum Juma amewataka watendaji hao kuwa makini katika suala la utunzaji wa vifaa   vya uandikishaji, sambamba na kuepuka kuchezea  mifumo ya kuandikia.

 Kama tunavyojua zoezi hili la uandikishaji mara hii ni la kidigitali zaidi kwahiyo tunatakiwa  vifaa tuvitunze  vizuri ili  vitumike mara nyingi zaidi katika uandikishaji".

Kwa Upande wake   Afisa uandikishaji  Tume ya Uchaguzi, wilaya ya mkoani  Juma Fumu Makame  amesema  lengo la mafunzo  hayo kwa wakuu wa vituo na makarani hao ni kuwafundisha  na ujuzi utakaosaidia kufanikisha zoezi hilo kwa umakini zaidi. 

Mafunzo hayo  ya  siku mbili juu ya mfumo wa uandikishaji kwa makarani na wakuu wa vituo  yamefanyika katika ukumbi wa Kiwanda cha makonyo wawi Chake Chake ambapo Zoezi hilo linatarajiwa kuanza kesho Tarehe 2 katika wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI