TRA MKOA WA KIKODI YATOA MSAADA WA VIFAA HOSPITALI YA WILAYA KINYASINI WETE, WIZARA YATOA UJUMBE HUU.

NA- AMINA AHMED, PEMBA. minnah1202@gmail. com. 
KAMISHNA wa Mamlaka ya  Mapato Tanzania TRA amewataka wananchi kisiwani Pemba Kuendeleza harakati za ulipaji  wa kodi ili kuisaidia serikali kutekeleza miradi  mbali mbali  itakayitumiwa kwa na wananchi pamoja na kusaidia kutekeleza huduma nyengine muhimu za kijamii.
 
     Wito  wa kamishna wa mamlaka hiyo umetolewa kwa niaba yake na  kaimu naibu kamishna wa huduma za kiufundi   wa mamlaka hiyo Venance alipokuwa akizungumza na wananchi pamoja na watendaji wa hospitali ya wilaya  kinyasini Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba  katika Ghaflaya kukabidhi vifaa tiba pamoja na Dawa kwa hospitali hiyo ikiwa ni muendelezo wa wiki ya kurejesha shukurani kwa mlipa kodi .

Amesema iwapo wananchi wataendelea kuwajibika  ipasavyo katika ulipaji kodi malengo yaliyowekwa na serikali  ya utowaji wa huduma bora kwa wananchi yataweza kufikiwa. 

Aidha amesema kuwa lengo la kukabidhi msaada huo wa vifaa tiba pamoja na dawa ni katika kuwashukuru  wananchi ambao  ndio walipa kodi  zinatumika kusaidia upatikanaji wa huduma pamoja na uimarishaji wa maendeleo. 

 Nae Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali ameishukuru mamlaka hiyo kwa kuendelea kuunga  mkono juhudi za serikali ambapo amesema kuwa  vifaa hivyo vilivyotolewa  vitatumika kwa walengwa na malengo yaliokusudiwa. 

Akitoa neno la shukurani   mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo  Daktari dhamana wa hospitali hiyo Ramadhan  Faki Ali ameziasa taasisi nawadau wengine kuendelea kuiga mfano wa kzalendo  ulioneshwa na TRA kwa kujitokeza kusaidia    vifaa tiba pamoja  na dawa kwa vile ni  jambo linalohitajika kila siku kwajili ya  matumizi yake kwa wananchi. 

Miongoni mwa vifaa vilivyokabidhiwa ni Pamoja na Mashuka 50, Nepi za watoto, na watu wazima, Nguo za Madaktari pamoja na Dawa mbali mbali.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI