UHABA MAAFISA USTAWI JAMII WALALAMIKIWA WADAU WALIA NA SERIKALI.

NA AMINA AHMED MOH'D PEMBA. 

WADAU wa kupinga vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kisiwani Pemba Wameiomba  Serikali kuongeza idadi ya maafisa ustawi jamii  katika wilaya  ili kusaidia kuongeza kasi ya kupambana na changamotoza  vitendo vya Udhalilishaji wa kijinsia kwa watoto.

 Wakizungumza kwa nyakati  tofauti baadhi ya wadau hao wamesema kuwa kutokana na uhitaji wa watu hao katika kusaidia kupambana  na vitendo hivyo  utaratibu wa Afisa mmoja katika kila wilaya ni miongoni mwa changamoto  inayopelekea  kuongezeka kwa changamoto katika kesi za udhalilishaji.

"Wilaya  mfano wilaya ya mkoani ina  shehia 32 ambazo shehia zote hizo vitendo na kadhia za udhalilishaji kwa watoto zinajitokeza  Afisa mmoja tu ndie analazimika kushuhulika  haisaidii kuondoa changamoto", Fathiya Mussa Said. 

 Serikali iliangalie suala hili kuona kwamba ipo haja ya kuongeza idadi ya hawa watu katika wilaya ikiwezekana iwaweke kwa shehia ili kuondoa usumbufu katika kesi za udhalilishaji kwa watoto ".Siti Habibu Muhamed kutoka Shirika la msaada wa kiaheria 

Kutokana na umbali ambao wapo maafisa ustawi jamii waliowengi wamekuwa wakibadilisha maamuzi hivyo ni vyema kusogezwa kwa karibu ili Tuweze kupata mashirikiano katika kupambana na vita hii, Alisema Tatu Abdalla Msellem Wanaharakati masuala ya udhalilishaji. 

Aidha kwa Upande wake   Asha Massoud Salim kutoka kituo cha mkono kwa mkono Chake Chake ameiomba Serikali kuongeza vituo vya ushauri nasihi ili kuondoa athari kwa wahanga  kwa kuwashirikisha wadau ambao wataweza kuanzisha vituo hivyo.

Changamoto kubwa iliyopo sisi watu wa mkono kwa mkono ni lazima tufanye kazi na watu wa ustawi wa jamii, lakini kiukweli hawa watu wapo mbali inakuwa ni usumbufu kwa wahanga  kuwapeleka katika kitengo chao

Alisema licha ya kutolewa huduma hiyo kwa wahanga  wanaothirika lakini bado waliowengi wamekuwa wakishindwa kufika katika kituo hicho hususan n kwa wananchi wanaoishi mbali na kituo hicho. 

Maafisa ustawi ni moja kati ya wasimamia miongozo ya utekelezaji wa kutoa huduma za kisaikologia  kwa jamii kwa lengo la kupunguza  matatizi yanayotokea hususan ni vitendo vya  ukatili. 











 
 
 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI