Posts

Showing posts from July, 2023

HABARI ZINAZOHUSU AFYA YA UZAZI KWA WANAWAKE NA WASICHANA YAJA NA SURA MPYA PEMBA NI BAADA TAMWA-ZNZ KUTAFUTA 40 JUU YA UTOLEWAJI MDOGO WA TAARIFA HIZI.

Image
Na - AMINA AHMED MOH’D , PEMBA.  ZAIDI ya Waandishi wa Habari  15 Kutoka vyombo  mbali mbali Kisiwani Pemba wamepatiwa  Mafunzo ya  siku tatu juu ya Afya ya Uzazi  ambayo  yamelenga   kuongeza uelewa  juu ya kuandika kwa Ubora  na kuelimisha kupitia kalamu zao na   kuondosha Changamoto  zinazoendelea kujitokeza kutokana na kukosekana kwa Afya  na Uzazi kwa  Makundi mbali mbali ya wanawake katika Jamii.   Akifunga Mafunzo kwa Waandishi hao Afisa Mdhamini Wizara ya Afya Pemba  Khamis Bilali Ali   amewataka Waandishi hao  kuitumia Elimu hiyo  iliyotolewa  kwa  kuandika Habari  zitakazoisaidia  Kupunguza Vifo vya kina Mama na watoto .  Amesema Miongoni mwa vipengele  Muhimu ambavyo vinahitaji kufanyiwa kazi na Waandishi wa Habari kufikisha Elimu na  Kusaidia Serikali  ni Afya ya Uzazi ambayo  Wanawake  na Wasi...

MARADHI YASIOAMBUKIZA UGONJWA WA SINDIKIZO LA DAMU (PRESSURE).

Image
NA, ABDALLA  AMOUR MBAROUK - PEMBA.  PENDA  kujua usiyo yajua na usidharau usilo lijua , elewa uzima hauchoshi Wala haukinaishi lakini Sindikizo la Damu ni ugonjwa unaoweza kukatisha maisha kama hautakua muelewa wa ugonjwa huo . Sindikizo la Damu (hypertantion) ni matokezeo ya msukumo wa nguvu wa  wdamu unatoka kwenye moyo kuelekea sehemu nyengine za mwili ambao mskumo huo unakua sio wa kawaida . Moyo ni kiungo muhimu na chenyekubeba kazi nyingi mwilini hivo kinapo pata hitilafu kama kushindwa kusambaza Damu kwa kiwango kinacho hitajika kwenda sehemu nyengine za viungo vya mwili  kwa kuziba au kubana  kwa baadhi ya mishipa ya Damu (blood versels) kutokea kwa Hali kama hiyo ndio husababisha ugonjwa huo wa sindikizo la Damu. Kwa mujibu wa vipimo vya kitaalamu mwanadamu aliye katika Hali ya  uzima wa kawaida kiafya anatakiwa awe na kiwango Cha 110 Hadi 140/80-90 Cha Damu na kuzidi kuanzia 140 na kuendelea mtu huyo atahesabiwa kua ni mgonjwa wa...

TAMWA-ZANZIBAR YAWATAKA WANAWAKE KUJITAYARISHA 2025 KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI BILA KUOGOPA VITISHO NA CHANGAMOTO.

Image
CHAMA cha waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) kinawataka Wanawake kuwa wajasiri na kujitayarisha kiuongozi bila kuogopa changamoto zinazowakabili wanawake wanapoingia katika uongozi ili kuongeza ushiriki wao kwenye vyombo vya maamuzi. Idadi ndogo ya wanawake katika vyombo vya maamuzi na michakato ya kidemokrasia umekuwa ukijidhihirisha katika chaguzi zinazofanyika nchini kila baada ya miaka mitano ambapo wanawake hupata nafasi chache na ndogo jambo ambalo linaweza kuwa kikwazo kwa Tanzania kutokomeza umaskini na kuimarisha demokrasia inayowapa wananchi haki ya kuchagua kiongozi wamtakae.  Hivi karibuni TAMWA ZNZ kimeendesha mafunzo kwa wanawake wenye dhamira ya kugombea nafasi za uongozi Zanzibar na kubaini kwepo kwa hofu miongoni mwa wanawake kushiriki katika nafasi hizo kutokana na sababu mbalimbali. Miongoni mwa sababu zilizobainika kukwamisha ushiriki wa wanawake katika vyombo hivyo ni vitisho, hofu dhidi ya rushwa ya Ngono, pamoja kukosekana...

AKINA MAMA WINGWI MTEMANI WAOMBA MSAADA WAKUTULIWA NA NDOO KICHWANI

Image
  Na Amina Ahmed Moh’d Pemba.( minnah1202@gmail. com)  BAADHI ya akina mama  Katika kijiji cha  jambo nia kilichopo Shehia ya Wingwi Mtemani Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini wanalazimika kuchota Maji kwajili ya Matumizi huku wengine wakiwa katika Hali ya Ujauzito ni kutokana na kukosa huduma ya Maji ya Bomba ndani ya kijiji chao.   Wakizungumza baadhi ya kina mama  hao mara baada ya kuonekana na kamera hizi wakiwa katika kisima  cha ndoo Akina Mama hao Wamesema kuwa hulazimika kufanya hivyo ili kujipatia Maji kwajili ya kuendesha shughuli za majumbani ambazo kwa Asilimia kubwa zinahitaji maji ili kukamilika kwake.  Wamesema kukosa huduma hiyo  kwa mufa mrefu kijijini kwao  ndiko kunakosababisha kutumia visima hivyo kuchota maji   na kuhatarisha hali za Afya zao ikiwemo kupata  maradhi ya kichwa.    Akina mama hao wameiomba serikali pamoja na viongozi wao wa jimbo  kuwasaidia kulipa...

MWENYEKITI WA TAASISI YA MAISHA BORA FAUNDATION MARYAM MWINYI AWAHIMIZA WANANCHI KUSINI PEMBA UMUHIMU WA KUFANYA MAZOEZI KUIMARISHA AFYA KUEPUKANA NA MARADHI YASIOAMBUKIZA.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA  MWENYEKITI wa Zanzibar Maisha Bora Faundation ambae pia ni Mke wa Rais wa Zanzibar mama   Maryam Mwinyi Ameongoza   matembembezi  maalum ya kuhamasisha umuhimu wa kufanya mazoezi   kwa Wananchi Mkoa  wa Kusini Pemba  yalioanza  eneo la  Kiwanda cha Makonyo wawi  Chake Chake na Kumalizia katika Viwanja vya Gombani ya kale wilaya hiyo.  Akizungumza na Wananchi mara baada ya  kumalizika kwa Matembezi hayo Mwenyekiti huyo  Amewataka wananchi Wa kusini Pemba Kuendelea kufanya mazoezi ili kuimarisha  afya zao na kuepukana na Maradhi mbali mbali. "Tunafahamu kuwa Mazoezi yanaimarisha Afya yanatukinga na Maradhi, Yasioambukiza  kama vile Pressure ambayo ni sindikizo la Damu ,  Kisukari, Uzitowa Kupindukia, Magonjwa  ya Moyo  haya yote tukiwa na tabia ya kufanya mazoezi tutaondokana nayo na kuepuka kuenda hospitali mara kwa mara na kuisaidia kupunguza m...

ZAPDO, ZALHO WAFIKA WINGWI KUZUNGUMZA NA WANANCHI JUU YA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI.

Image
Wananchi Shehia ya  Wingwi Mtemani Wilaya ya Micheweni Mkoa wa kasakzini Pemba Wameiomba Jumuia ya watu wenye Ulemavu wa Akili Pamoja na Shirika la Msaada wa kisheria kuwasaidia kulipatia ufumbuzi suala la  kupatikana Hospitali maalum kwa wagonjwa wa  Akili sambamba na hi kuwawekea  Madakatari maalumu ambao Watakuwa na  Utaratibu Wa kuwatembelea na kuwapatia Huduma za afya na  Matibabu wagonjwa Wa Akili waliopo katika Maeneo mbali mbali kisiwani Pemba.   Wametoa Ombi hilo leo  Walipokuwa  wakizungumza Katika Mkutano Maalum  ulioandaliwa na Jumuia ya Watu wenye Ulemavu wa Akili Zanzibar pamoja Shirika la Msaada wa kisheria    huko Wingi Jambo nia. Wamesema Licha ya Kuwepo kwa Idadi kubwa ya Watu wenye Ulemavu wa Akili  wanaozurura na kuzagaa katika Maeneo mbali mbali kisiwani Pemba Lakini bado  kumekuwa na Changamoto ya Kukosekana na Hospitali hiyo pamoja Madakatari wanaotembelea majumbani ...

MHADHIRI CHUO KIKUU CHA ZANZIBAR SUZA WANAWAKE WASHINDE UONGOZI LAZIMA WAZIELEWE MBINU ZA KUJENGA USHAWISHI USHAWISHI KISIASA.

Image
  NA MWANDISHI WETU   ZANZIBAR WANAWAKE wenye nia ya kugombea nafasi za uongozi wametakiwa kuelewa mbinu sahihi za kufanya ushawishi katika siasa na uongozi ili kukabiliana na vikwazo vinavyoweza kuwakwaza kushika nafasi hizo katika ngazi mbalimbali. Wito huo umetolewa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar -SUZA, Dkt. Salum Suleiman Ali, wakati wa mafunzo maalum kwa wanawake kutoka vyamba mbalimbali vya siasa Pemba kuwajengea uwezo kutambua haki zao na kushiriki katika mchakato wa kugombea nafasi za uongozi kwenye vyombo vya maamuzi.         DK  SALUM  SLEIMAN ALI - MHADHIRI SUZA.  Akizungumza katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway Tanzania, alieleza suala la kushiriki kugombea nafasi za uongozi ni mchakato endelevu unaohitaji maadalizi ya muda mrefu ili kujenga Imani kwa jamii juu ya uwezo wa kiongozi katika kute...

WANANCHI PEMBA WAIOMBA SERIKALI KUWASAIDIA HOSPITALI YA WAGONJWA WA AKILI PAMOJA NA MADAKATARI MAALUM

    AMINA  AHMED MOH’D - PEMBA  ,   (  0719859184.). WANANCHI Shehia ya  Wingwi Mtemani  Wilaya ya Micheweni Mkoa Wa kaskazini Pemba  wameiomba Serikali na wadau  kuwasaidia kulipatia ufumbuzi suala  la kujengewa Hospitali maalum kwajili ya  wagonjwa wa  Akili  ili kuwaepushia kuzurura na Kuzagaa mitaani  sambamba na kuwawekea  Madakatari Maalumu ambao Watakuwa na  Utaratibu wa kuwatembelea na kuwapatia Huduma za matibabu Wagonjwa hao Wanapokuwa Majumbani.   Wametoa Ombi hilo leo  Walipokuwa  wakizungumza na kutoa maoni yao juu ya   habari hizi  kuhusu haki ya kulindwa dhidi ya Udhalilishaji wa Kijinsia   kwa Watu wenye Ulemavu wa Akili  katika Maeneo mbali mbali kisiwani Pemba.  Wamesema Licha ya Kuwepo kwa Idadi kubwa ya Watu wenye Ulemavu wa Akili  wanaozurura na kuzagaa katika Maeneo mbali mbali kisiwani Pemba Lakini bado  kumekuw...

MRADI WA VIUNGO PEMBA WALETA MAGEUZI KWA WAKULIMA, WASEMA NI CHACHU YA KUKOMBOKA KIUCHUMI.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA  :0719859184  WAKULIMA  wa viungo mboga mboga na matunda kisiwani Pemba wamewataka wananchi kuzitumia fursa  kujiinua  kiuchumi  kupitia fursa za kilimo hicho ambacho kitawaletea  tija.  Ushauri huo umetolewa na Wakulima kwa nyakati tofauti huko katika Mashamba yao walipokuwa wakizungumza na waandishi  wa habari ikiwa ni ziara maalum ya kuangalia mafanikio  kwa  wakulima   wa mradi wa viungo  unaofadhiliwa na  umoja wa wa ulaya EU  kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya kilimo na kutekelezwa  na TAMWA-Zanzibar, PDF pamoja na Community forest Pemba CFP ikiwa ni mpango Maalum Wa kukuza kilimo "  Agri conect".   Wamesema Kilimo Cha Viungo mbga mboga na matunda Ni Fursa Pekee inayoweza kuwakomboa wananchi kiuchumi na kuwawezesha kuwainua Kiuchumi  Na kuacha utegemezi.  "    Awali kabla  sijapata fur...

MKURUGENZI BARAZA LA MJI WETE "NITASIMIA UJENZI SOKO MZAMBARAUNI KUSOGEZA KARIBU HUDUMA KWA WANANCHI

Image
  Na AMINA AHMED MOH’D,   PEMBA.  KUFUATIA Maombi na kilio cha Muda Mrefu  kwa   Wakaazi Mzambarauni takao   Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba juu ya kujengewa Soko katika Kijiji  chao Hatimae  Uongozi wa  Baraza la Mji wete Umepitisha Azimio  la kujengwa  soko  kijijini Hapo.  SALMA ABUU HAMAD MKURUGENZI BARAZA LA MJI WETE  Adhimio hilo limepitishwa na Mkurugenzi wa Baraza la Mji  Wilaya ya Wete  Salma Abuu Hamad  kwa kushirikiana na Madiwani wa wilaya ya Wete  Ambapo  amesema adhimio hilo limelenga kuwaondoshea Usumbufu Wananchi.    Aidha Mkurugenzi huyo alisema  kuwa Kupitishwa kwa Adhimio hilo kumetokana  na Maombi ya Muda Mrefu kutoka kwa wananchi wa Mzambaruni  Kuhitaji soko karibu na Maeneo yao ambalo litawasaidia kurahisisha upatikanaji wa bidha na kuwaondoshea usumbufu wa kufata bidhaa maeneo ya mbali.  "Mlikuwa mnaleta san...

WADAU WAHIMIZA UTEKELEZAJI WA SERA NA SHERIA ZINAZOSIMAMIA MASUALA YA UDHALILISHAJI

Image
Na Asha Ahmed, Unguja. Katika muendelezo wa harakati za Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA ZNZ kupambana na kesi za udhalilishaji Zanzibar, kimekuwakutanisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa sera na sheria zinazosimamia masuala ya udhalilishaji Zanzibar. Wadau hao ni pamoja na mahakimu kutoka mahakama maalum ya udhalilishaji, maafisa kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka, wanasheria, Jeshi la Polisi, msaidizi kamishna kutoka chuo cha mafunzo, watoa msaada wa kisheria, maafisa kutoka asasi mbalimbali za kiraia na serikali pamoja na waandishi wa habari. Lengo kuu la mkutano huo lilikua ni kujadili sera na sheria na kuangalia ni kwa namna gani zinatekelezwa katika kupambana na vita ya udhalilishaji hapa visiwani Zanzibar, ambapo wadau hao walisikitishwa sana kwa kuwepo na sera na sheria nyingi na madhubuti lakini zisizotekelezwa jambo ambalo linachangia kuongezeka kwa vitendo vya udhalilishaji. Mratibu wa TAMWA ZNZ kwa upande wa Pemba F...