MRADI WA VIUNGO PEMBA WALETA MAGEUZI KWA WAKULIMA, WASEMA NI CHACHU YA KUKOMBOKA KIUCHUMI.

NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA  :0719859184 

WAKULIMA  wa viungo mboga mboga na matunda kisiwani Pemba wamewataka wananchi kuzitumia fursa  kujiinua  kiuchumi  kupitia fursa za kilimo hicho ambacho kitawaletea  tija. 

Ushauri huo umetolewa na Wakulima kwa nyakati tofauti huko katika Mashamba yao walipokuwa wakizungumza na waandishi  wa habari ikiwa ni ziara maalum ya kuangalia mafanikio  kwa  wakulima   wa mradi wa viungo  unaofadhiliwa na  umoja wa wa ulaya EU  kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya kilimo na kutekelezwa  na TAMWA-Zanzibar, PDF pamoja na Community forest Pemba CFP ikiwa ni mpango Maalum Wa kukuza kilimo "  Agri conect". 

 Wamesema Kilimo Cha Viungo mbga mboga na matunda Ni Fursa Pekee inayoweza kuwakomboa wananchi kiuchumi na kuwawezesha kuwainua Kiuchumi  Na kuacha utegemezi. 

"    Awali kabla  sijapata fursa hii ya kuwa mnufaika kulima kilimo hichi cha Viungo, Vanilla na Mdalasini nilikuwa nashindwa kujikimu vizuri kimaisha, lakini sasa naendesha shuguli zangu bila wasi wasi wowote,  Kilimo ndio Imekuwa Mafanikio yangu  mradi wa viungo  umenikomboa, Alisema Salma Hamad Ali  Mkulima wa Mdalasini Gando Mkoa wa Kaskazini. 

" Mradi wa viungo Umenikomboa na umabadilisha maisha yangu kwa kipindi kifupi sana, Mimi ni mmoja kati ya wakulima wanufaika katika   mradi wa Viungo, Nimeongeza uzalishaji wa midalasini  zaidi ya  10000, wakati mwanzoni nilikuwa na  midalasini miamoja tu ambayo hiyo naishughulikia bila kupata faida wala kujua kudhibiti mabadiliko ya Tabia ya nchi. 

"Nina zaidi ya Eka 6  za Midalasini tu, wakati mwanzoni hata kabla ya kuja kwa mradi nilikuwa sijui kuhusu  zao la vanilla pia Nimehamasika kulima vanilla na saivi Ninayo mivanilla Zaidi ya elf 5 Shambani kwangu  ". 

" Nilikuwa sina Elimu sina Taaluma wala sijui jinsi gani nitaendeleza zao la  vanilla mradi wa viungo  umenitoa  kutoka kilimo ambacho sielewi chochote mpka kufika kwenye kilimo cha kitaalamu chenye Tija  kwangu, Naendesha Familia yangu, najiptia kipato, naweka hakiba ya kiendeleza shuguli zangu ". 

 "Tulikuwa Tunapata shida sana kuwafikia wakulima kuwapatia pembejeo za kilimo, kuwapa  Elimu  lakini mara tu baada ya kuja mradi huu wa viungo Taasisi ambazo zinashughulikia Na kusimamia huu mradi    kumerahisisha kuwafikia wakulima  wote  Waliomo ndani ya jumia  mbao ni zaidi ya 800 wanaojishughulisha na upandaji wa viungo  kuwapa elimu na mbinu za ulimaji wa kisasa pembejeo pamoja na mbegu " Alisema Sleiman Ali Mfaki  mkulima wa Vanilla na Mdalasini ambae pia ni mwenyekiti wa   Jumuia ya wakulima wa viungo na  mazao  (Pemba Spice  producer coorperative). 


Asha Ali Omar Anasmea kuwa  kupitia mradi wa viungo  kwa upande wake Hakuwahi kujua nini haswa faida ya Kulima Mazao ya viungo licha ya kulima kwa muda mrefu. 


"Nilikuwa naona tu watu wanalima  wanapanda na mimi nikawa najitia tu kundini nafanya kama ni mazoea ya kawaida tu napanda pembeni mwa nyumba zetu , lakini Mradi huu ulipokuja tukapewa Elimu tukahamasika na kuanza kutafuta mashamba kwa vile nilikuwa nayo nalima tu Mihogo  tukaanza kupanda  Midalasini,  nimepanda eka kama moja, Na ndani ya hiyo eka nimepanda pia vanilla Miche 150 Faida nimeiyona  nasomeshea wanangu, baada ya kuvuna mara ya kwanza, Mara ya pili Nimepata pesa ya Kumlupia mwanagu kusomea udereva, nakata nauza napata kipato  nimeanza kujenga  nyumba  na nafanya shughuli nyengine kupitia kilimo pia ninayo hakiba ambayo naendeleza shughuli za kilimo.

 
Subira Mkubwa Muhammed  pamoja na   Ali Khamis Abdalla Ambao wamekuwa wakijishughulisha na kilimo cha Matunda,  na Mboga mboga ikiwemo Mananasi, Mapensheni  Matikiti,Pili pili boga na  matikiti  kutoka kijiji cha Kwale Mpona  Wamesema kuwa mradi mara baada ya kuwa wanufaika wa mrafi huo Kasi ya maendeleo ya kiuchumi na uzalishaji imeongezeka mara mbili zaidi ya ilivyokuwa awali kabla ya kuja kwa mradi huo. 

 Tulikuwa tunaanika Mdalasini baada ya kuchuna  kwenye barabara unaingia michanga mavumbi,  siku nyengine unaroa Lakini kupitia  Mradi huu tunatumiaSolara draya  kukaushia  Kwa haraka na rahisi Zaidi  . ni mafanikio makubwa kwa upande wetu. 

"Nimetia umeme tumeuvuta mbali sana ushawishi kwa serikali umeongezeka Tumekuwa tukitumia fursa ya mikopo inayotolewa na serikali  bila kipingamizi, Kilimo chetu kwa sasa tunatumia umwagiliaji wa dripu, Tumeajiri vijana ajira za Msimu na wao kutusaidia wanajipatia kipato Tumekuwa shamba darasa kwa wakulima wengine mbali mbali  kupitia Mradi wa viungo watu wanaiga kutoka kwetu namna ya kulima  kilimo hichi . 


"  Tayari kupitia Mradi huu wa viungo Tumeanza kujenga Nyumba fondesheni ile mnayoiona, Soko leru la bidhaa ni la kila siku tunaingiza na faida inapatikama kubwa sitaki kuitaja hapa lakini inajitosheleza   Tunapata  kuweka kuendesha gharama  za kilimo,  na nyengine inabakia kiasi ambacho hata mradi umalizike kesho b hihasi hatutorudi nyuma kuendeleza kilimo. 
  
Nae Kwa Upande wake Mkunga Hamad Sadala Mkulima mnufaika Mradi wa Viungo  Vitongoji Wilaya ya Chake Chake  Ambae anajishugulisha na kilimo cha Matunda na mboga mboga Ameseeleza kuwa Faida mbali mbali amabzo amezipata kupitia kilimo cha  mboga mboga kupitia  mradi wa viungo Amefanikiwa kuhamasisha  vijana kuwekeza katika Kilimo, sambamba na kujipatia mtaji mwengine wa kuendeleza shughuli zake ikiwemo Mifugo Ikiwemo mbuzi pamoja na kuku. 

    Akizungumza  kuhusu  Maendeleo kwa wakulima hao Afisa Viungo Kupitia Mradi  wa  Viungo unaosimamiwa na Agri Conect  upande wa Pemba  Haziel Gilbert Sezero  amesema lengo la kushughulika na wakulima wa mazao ya viungo matunfa na mboga mboga , ni kusaidia kupunguza  changamoto   mbali mbali ambazo zilikuwa zinawakabili na kupelekea kurudi nyuma kimaendeleo. 

"Mradi huu umekuja kusaidia kupunguza changmoto za wakulima wa mazao ya viungo, walikuwa wakikabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo eneo la kukaushia Mazao yao kipindi cha mvua, ambayo yalikuwa yakiharibika kutokana na kupata Sumu Kuvu, Kwaio baad ya kuona hivyo Mradi ulisadia upatikanaji wa Solar  Draya  ambayo , Lakini pia Changamoto ya Mbegu lengo ni kuoma wakulima Wetu wanapata tija na kipato kupitia kilimo jambo ambalo limefanikiwa kwa kiasi kikubwa. 

  Ziara  hiyo ya waandishi wa habari  kutembelea wakulima wanaufaika Mradi wa viungo pemba Imeandaliwa na Chama cha  Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar, ikiwa ni utekelezaji wa Mradi wa Viungo     ambao unatekelezwa kwa mashirikiano kati ya Tamwa Zanzibar, PDf, CFP kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya EU kulitia mpango wa Agri conect  ambapo zaidi ya Mashamba  ya wakulima   5 kutoka maeneo mbali mbali ya kisiwa hicho yametembelewa na Waandishi hao
Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI