MWENYEKITI WA TAASISI YA MAISHA BORA FAUNDATION MARYAM MWINYI AWAHIMIZA WANANCHI KUSINI PEMBA UMUHIMU WA KUFANYA MAZOEZI KUIMARISHA AFYA KUEPUKANA NA MARADHI YASIOAMBUKIZA.

NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA 

MWENYEKITI wa Zanzibar Maisha Bora Faundation ambae pia ni Mke wa Rais wa Zanzibar mama   Maryam Mwinyi Ameongoza   matembembezi  maalum ya kuhamasisha umuhimu wa kufanya mazoezi   kwa Wananchi Mkoa  wa Kusini Pemba  yalioanza  eneo la  Kiwanda cha Makonyo wawi  Chake Chake na Kumalizia katika Viwanja vya Gombani ya kale wilaya hiyo.

 Akizungumza na Wananchi mara baada ya  kumalizika kwa Matembezi hayo Mwenyekiti huyo  Amewataka wananchi Wa kusini Pemba Kuendelea kufanya mazoezi ili kuimarisha  afya zao na kuepukana na Maradhi mbali mbali.

"Tunafahamu kuwa Mazoezi yanaimarisha Afya yanatukinga na Maradhi, Yasioambukiza  kama vile Pressure ambayo ni sindikizo la Damu ,  Kisukari, Uzitowa Kupindukia, Magonjwa  ya Moyo  haya yote tukiwa na tabia ya kufanya mazoezi tutaondokana nayo na kuepuka kuenda hospitali mara kwa mara na kuisaidia kupunguza mzigo  kwa Serikali yetu wa kuagiza dawa za  magonjwa haya yasioambukiza  " Alisema . 

Amesema Taasisi hiyo  imeweka Mpango huo maalum wa kuhamisha umuhimu wa kufanya  Mazoezi kwa Wazanzibari wote ili kuenda sambamba na Kasi ya Maendeleo iliyopo  ambayo inahitaji Wananchi wenye Afya Imara. 

"Kwa Kasi ya 5G iliyopo inayoletwa na Rais wetu Dk Hussein Mwinyi ni lazima inahitaji Afya imara ya wananchi wake na ndio sababu ambayo Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Faundation ikaweka kipaumbele  muhimu suala hili la Kufanya mazoezi kwa Wananchi".

 Aidha Maryam amesema licha ya kuimarisha Afya pia Ufanyaji wa mazoezi  Unasaidia kukuza Umoja na  amani  na kuimarisha zaidi Mshikamano uliopo.

"Michezo inatuletea  amani na furaha kama ambavyo tunajiona hapa leo  kupitia mazoezi haya ya pamoja Tumefurahi  tumekusanyika  tumejuana watu kutoka meneo na itikafi mbali mbali  kwa pamoja mumeitikia kwa hamasa jambo hili kwa pamoja Nasema Ahsanteni na nikiri muitikio huu nimefurahi hivyo tuzidishe umoja na mshikamano  huu ili kuzidisha Amani iliyopo". 

  Akizungumzia kuhusu Taasisi hiyo ya Zanzibar Maisha Bora Faundation iliyoanzishwa mwaka 20121 na kuanza Rasmi kazi zake Mwaka 2022  Mama Mwinyi Amesema  kuwa lengo la kuanzishwa  kwa Taasisi hiyo  imeundwa maalum kwa lengola kuisaida Serikali  Kuleta Maendeleo kwa Wananchi Wake.
 
 "Lengo la kuanzisha taasisi  ni kuunga mkono Serikali hususan ni kwa akina Mama, Vijana na watoto ambapo Zanzibar Maishabora Faundation inasaidia zaidi katika maeneo manne Ambayo ni uwezeshaji kwa Akina mama wakulima wa  Mwani, Masuala ya Afya ya Mama na Mtoto,  Ushajihishaji wa Uchanjaji chanjo ya Uviko 19 katika maeneo ambayo yako nyuma Vile vile kutoa Elimu  Afya ya Uzazi na Hedhi salama kwa Vijana Sambamba na kupinga ukatili na Udhalilishaji wa akina mama na Watoto. 

Awali Akizungumza  Mku wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud Amemshukuru Mwenyekiti huyo  kwa Kutimiza Ahadi yake ya kuungana pamoja na wananchi wa Mkoa wa kusini Pemba katika Matemebezi  hayo  ya kuhamasisha Suala hilo la kuimarisha Afya .

" Tunakushukuru Mwenyekiti  Ambae pia ni Mke wa Rais wa Zanzibar kwa kutimiza Adhma hii ya kujumuika na Wananchi  Wa Kusini Pemba , tunakuombea heri katika Kumsidia Rais  kutimiza majukumu yake ya Kuleta Maendeleo kwa Taifa tunakuomba uendelee na moyo huo wa kumsaidia Kuleta Maendeleo Kwa Wananchi". 

Awali akitoa Salamu za wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo kwa Niaba ya Waziri wa wizara hiyo Tabia Maulid Mwita, Kamishna Idara ya Michezo Pemba Ameir Muhamed Makame  Amesema  kuwa wizara itaendelea kushirikiana  na Taasisi hiyo katika kuona Suala la kuhamaisha michezo linakiwa Endelevu Kwa Wananchi wa Zanzibar pamoja na kuongeza hamasa juu ya Suala hilo .

 Pamoja na Mambo Mengine Mwenyekiti huyo Pia Amekabidhi Taulo za Kike 200 kwa Wanafunzi wa Skuli ya Skuli ya Sekondari Dk Philip Mpango na  Skuli ya Msingi Uzalendo ikiwa lengo ni kuimarisha Afya ya Uzazi kwa Watoto wakike. 
 Matembezi hayo ambayo yalianza mapema katika Eneo la kiwanda cha Makonyo Wawi na Kumalizia katika Viwanja vya Gombani ya kale  yamewashirikisha wananchi, viongozi wa Serikali za Wilaya zote Mbili Chake Chake na Mkoani, Viongozi wa vyama vya siasa  Taasisi  mbali mbali pamoja na Vikundi vya Mazoezi  vilivyomo katika Mkoa huo.


Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI