AKINA MAMA WINGWI MTEMANI WAOMBA MSAADA WAKUTULIWA NA NDOO KICHWANI


 

Na Amina Ahmed Moh’d Pemba.( minnah1202@gmail. com) 

BAADHI ya akina mama  Katika kijiji cha  jambo nia kilichopo Shehia ya Wingwi Mtemani Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini wanalazimika kuchota Maji kwajili ya Matumizi huku wengine wakiwa katika Hali ya Ujauzito ni kutokana na kukosa huduma ya Maji ya Bomba ndani ya kijiji chao. 

 Wakizungumza baadhi ya kina mama  hao mara baada ya kuonekana na kamera hizi wakiwa katika kisima  cha ndoo Akina Mama hao Wamesema kuwa hulazimika kufanya hivyo ili kujipatia Maji kwajili ya kuendesha shughuli za majumbani ambazo kwa Asilimia kubwa zinahitaji maji ili kukamilika kwake. 

Wamesema kukosa huduma hiyo  kwa mufa mrefu kijijini kwao  ndiko kunakosababisha kutumia visima hivyo kuchota maji   na kuhatarisha hali za Afya zao ikiwemo kupata  maradhi ya kichwa.  

 Akina mama hao wameiomba serikali pamoja na viongozi wao wa jimbo  kuwasaidia kulipatia  ufumbuzi suala hilo  ili waweze kuondokana na usumbufu huo wa kubeba ndoo kichwani na kuepukana na kutumia maji ambayo uhakika  na usalama  wake   wa kiafya sio wa uhakika.

 "Maji ya  Mfereji Sijui ata Muda gani sijayaona apa jambo nia, tunachota haya tupikie, vichwa vinatuuma lakini hatuna lakufanya Maji ni lazima majumbani yaweko" Alisema Mkunga Khamis Said mkaazi wa Jambo Nia. 

" Kama iwezekano wa kuletewa maji ya mfereji upo bhasi tusaidiwe ndoo kichwani mudawote ni Tatizo si dogo na ivo visima vyenyewe wasi wasi mtupu  Watoto tunaogopa ata kuwatuma". Aliendelea Mkunga. 

 Maji  ya mfereji kwetu  siku ya kutoka itakuwa Tunu kama Lulu Mana hayapo siku nyingi  wenzetu maeneo mengine mifereji saa zote maji tele Na Sisi tunaiomba Serikali isitisahau tunaoteseka ni sisi akina Mama, Baba ata hawana muda uo" Biamu Khamis Said Alisema. 

Akizungumzia suala hili sheha wa shehia ya   Wingwi Mtemani  Muhammed  Ali Hamad amekiri kuwepo kwa tatizo hilo  katika badhi ya meneo ndani ya shehia yake ikiwemo kijiji cha Jambo nia  ambapo amesema uongozi wa shehia   umechukua jitihada mbali mbali ikiwemo kulipfikisha suala hili katika uongozi wa wilaya.

"Ni kweli  tatizo  la maji ya mfereji katika  baadhi ya vijiji ndani ya Shehia yangu lipo na uongozi wa Shehia tumeshalifikisha suala hili kwa wahusika ambao ni zawa pamoja na Uongozi wa Wilaya. 

" Taarifa za kukosekana kwa huduma ya maji safi na salama  Baadhi ya vijiji ndani ya shehia ya Wingwi mtemani tmeshalipeleka kwa uongozi wa wilaya  kupatiwa ufumbuzi zaidi". 

 Hata hivyo Harakati za kumtafuta Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji   pemba  juu ya  suala hili zinaendelea .


Mwisho
 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI