WANANCHI PEMBA WAIOMBA SERIKALI KUWASAIDIA HOSPITALI YA WAGONJWA WA AKILI PAMOJA NA MADAKATARI MAALUM

    AMINA  AHMED MOH’D - PEMBA  ,  0719859184.).

WANANCHI Shehia ya  Wingwi Mtemani  Wilaya ya Micheweni Mkoa Wa kaskazini Pemba  wameiomba Serikali na wadau  kuwasaidia kulipatia ufumbuzi suala  la kujengewa Hospitali maalum kwajili ya  wagonjwa wa  Akili  ili kuwaepushia kuzurura na Kuzagaa mitaani sambamba na kuwawekea  Madakatari Maalumu ambao Watakuwa na  Utaratibu wa kuwatembelea na kuwapatia Huduma za matibabu Wagonjwa hao Wanapokuwa Majumbani. 

 Wametoa Ombi hilo leo  Walipokuwa  wakizungumza na kutoa maoni yao juu ya   habari hizi  kuhusu haki ya kulindwa dhidi ya Udhalilishaji wa Kijinsia   kwa Watu wenye Ulemavu wa Akili  katika Maeneo mbali mbali kisiwani Pemba. 

Wamesema Licha ya Kuwepo kwa Idadi kubwa ya Watu wenye Ulemavu wa Akili  wanaozurura na kuzagaa katika Maeneo mbali mbali kisiwani Pemba Lakini bado  kumekuwa na Changamoto ya Kukosekana na Hospitali hiyo pamoja kutokuwepo kwa  Madakatari wanaotembelea Majumbani kuwapatia huduma za Matibabu jambo ambalo linapelekea kuhatarisha Usalama wao, sambamba na Kukosa Haki zao mbali mbali ikiwemo Afya Bora . 

"Wagonjwa Wa Akili wapo kwa idadi Kubwa kisiwani Pemba, Hata Umtafute Daktari Umwambie mimi nina mgonjwa siwezi kumfikisha  Hospitali njoo mara moja Unisaidie Humpati,  Labda Unaweza ukampata ukimlipia Gari au nauli ndio akufate, Mimi ninae mgonjwa ndani mwangu mtu mzima Hajajapo Daktari kuja kumuona na Kila siku naenda Pale Hospitali kununua Dawa lakini hata ile hamu ya kutaka kujua tu anaendeleaje hawaulizi Tunaomba  wadau zaidi Wizara ya Afya Itusaidie hili " Alisema Shoka  Hamad Abeid Mkaazi wa Wingwi. 

"Kutokana na kukosa Uelewa  Tunalazimika  kuwaacha tu wazurure Mimi mwanangu ni  mgonjwa wa Akili ana miaka 10 nilimuandikisha Lakini alikuwa umo Darasani hakai mara anaingia madarasa mengine Hatulii niliamua nimkatishe, anazurura tunaomba wadau na wa watu wenye ulemavu, Haki za Binaadamu na wadau wa kupambana na Udhalilishaji, pamoja na  Serikali, watusaidie Kupata uelewa Huenda tunawakosesha haki zao kutokana na kushindwa kujua vipi tunawasaidia kisheria kuzipata izo haki hizo " Alisema Mkongwe Khamis Said Mama Mweye mtoto ambae anaulemavu wa Akili Wingwi Jambo Nia. 

Aidha Wananchi  wameziomba jumuia na Mshirika ya kusaidia Upatikanaji wa haki kwa Watu wenye ulemavu Kuzidisha ukaribu wao kwa jamii   ili kupata urahisi wa kufikisha  changamoto zinazowakabili watu wenye Ulemavu wa Akili  na nyengine mbali mbali zinazowakabili  zinazohitaji msaada wa kisheria 

  Wakizungumza Juu ya Suala hilo Mwenyekiti wa Jumuia ya watu wenye Ulemavu Pemba Halfan Amour Muhammed Pamoja Siti Habib Muhammed Kutoka Shirika La Msaada wa Kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba  Wamesema Wataendelea kusimamia , kushawishi, pamoja na kutetea Upatikanaji wa Haki za Msingi kwa Watu wenye Ulemavu wa Akili kwa Wadau wa Maendeleo pamoja na Serikali. 

Watu wenye ulemavu wa akili wamekuwa  wakizurura huku wengine wakiitwa majina mabaya wengine wakifanyiwa vitendo viovu lakini Haki juu yao haipatikani, kutokana na kukosa Watetezi Jumuia ya Watu wenye ulemavu wa Akili tutaendelea kuwa bega kwa bega  kuona haki wanapata haki sawa kama walivyo watu wengine" Alisema   Mwenyekiti huyo.

" Watu wenye Ulemavu wa Akili wanastahiki kua na haki sawa kama Walivyo binaadamu wengine, Haki ya Kuishi, kulindwa dhidi ya majanga ikiwemo udhalilishaji, Haki ya matibabu  kushirikishwa   Haki ya Kusoma  na nyengine nyingi Zote hizi haziwezi kupatikana iwapo wazazi na walezi  hatutokuwa tayari kuwasaidia". 

"Tunatakiwa tuzidishe Mara mbili Usimamizi wa Kuzitafuta haki za Watoto wenye ulemavu wa akili Shirika la Msaada wa kisheria tutaendelea  kutoa mashirikiano Muda na wakati wowote  hivyo wananchi muitumie fursa hii  katika kuona watu wenye ulemavu wa akili na wao hawaachwi nyuma katika kupata haki na Maendeleo . 

Harakati za Kumtafuta Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba juu ya Maoni hayo  yaliotolewa na wananchi yanaendelea.


Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI