HABARI ZINAZOHUSU AFYA YA UZAZI KWA WANAWAKE NA WASICHANA YAJA NA SURA MPYA PEMBA NI BAADA TAMWA-ZNZ KUTAFUTA 40 JUU YA UTOLEWAJI MDOGO WA TAARIFA HIZI.

Na - AMINA AHMED MOH’D , PEMBA. 


ZAIDI ya Waandishi wa Habari  15 Kutoka vyombo  mbali mbali Kisiwani Pemba wamepatiwa  Mafunzo ya  siku tatu juu ya Afya ya Uzazi  ambayo  yamelenga   kuongeza uelewa  juu ya kuandika kwa Ubora  na kuelimisha kupitia kalamu zao na   kuondosha Changamoto  zinazoendelea kujitokeza kutokana na kukosekana kwa Afya  na Uzazi kwa  Makundi mbali mbali ya wanawake katika Jamii.
 

Akifunga Mafunzo kwa Waandishi hao Afisa Mdhamini Wizara ya Afya Pemba  Khamis Bilali Ali   amewataka Waandishi hao  kuitumia Elimu hiyo  iliyotolewa  kwa  kuandika Habari  zitakazoisaidia  Kupunguza Vifo vya kina Mama na watoto . 


Amesema Miongoni mwa vipengele  Muhimu ambavyo vinahitaji kufanyiwa kazi na Waandishi wa Habari kufikisha Elimu na  Kusaidia Serikali  ni Afya ya Uzazi ambayo  Wanawake  na Wasichana   waliowengi wanaikosa Elimu hiyo  hiyo na kupelekea Kupata Changamoto mbali mbali za Kiafya.

"Afya ya Uzazi kwa  ni Taaluma  ambayo ni pana sana, hili ni Jambo Zuri  lililofanywa na Ndugu Zetu wa Tamwa  kwa sababu kupitia  Elimu hii Mliopatiwa Mtaweza kuandika Habari mbali mbali zinazohusu  Afya ya uzazi, kuna Mimba za Umri Mdogo, Uzazi wa Mpango,  kwaio taaluma hii itakuwa ni msaada wa kuondoa zile changamoto  zilizopo katika jamii zikiwemo Ndoa za Mapema na Watu kupata Uelewa wa Kutosha  na kujua Masuala Mazima ya Uzazi Salama" Alisema Khamis Bilali Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba. 
     Khamis Bilali Ali  - A/ Mdhamini Wizara ya Afya Pemba 

 Aidha Mdhamini Huyo Alisema kuwa Moja kati ya Vipaumbele vya Wizara ya Afya Zanzibar ni kupunguza Vifo  vya Mama na watoto   hivyo  kupitia Elimu hiyo  iliyotolea  kwa Waandishi Jamii itaweza kujikinga na Kuzuia   Upatikanaji wa mimba za Mapema kwa Wanawake pamoja na kuondosha Mimba za umri Mdogo kwa Wasichana  pamoja na kuongeza uelewa kwa Wananchi juu ya Kutumia Uzazi  salama  pamoja na utumiaji wa  Uzazi wa Mpango.

 Awali  Akizungumza kwa Niaba ya Mkurugenzi wa Chama  Cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar  Muhammed Khatib Muhammed  ambae ni Afisa Ufuatiliaji na Tathmini   kutoka Chama hicho amesema Mafunzo   hayo yalilenga   zaidi kuongeza   uelewa wa Kuripoti Habari zinazohusu Afya ya Uzazi kwa waandishi wa Habari  ikiwa ni Pamoja na kuzungumzia Elimu na Upatikanaji wa Huduma Mbali mbali katika Vituo vya Afya.
        Muhammed Khatib Muhammed- TAMWA-ZNZ 
"Tumeona kuna changamoto kubwa kwa Waandishi wa Habari ni  Kushindwa kuandika Habari zinazohusu Afya ya Uzazi na kabla ya haya Mafunzo Tulifanya utafiti tukagundua kama  tatizo kubwa ni Waandishi waliopo katika vyombo Vya Habari vingi Elimu juu ya Afya ya Uzazi  ni Ndogo  ndio mana tukaamua kutoa Elimu hii ili kuona wanatekeleza majukumu yao kwa Uweledi  katika Kutetea Haki za wanawake  katika Masuala hayo ya Afya ya Uzazi" Alisema.
       
Rahila  Salim Omar  Dakatari wa Magonjwa ya Uzazi Pemba  Amesema  Jamii inaweza kujiepusha  na Magonjwa ya Kujamiana, na kuweza kujifungua Salama, kujilinda pamoja na kujikinga  na  Magonjwa  Saratani   kwa Kufanya uchunguzi wa kitaalamu   juu ya Afya Ya Uzazi   kwa kupima Magonjwa mbali mbali ambayo hupelekea kuathiri Viungo  na Afya ya Uzazi na Kusababisha  Vifo. 

 Akitoa Elimu  juu ya Afya ya Uzazi Ali Mbarouk Omar  Mratibu wa Tume ya Ukimwi Pemba   ambae pia ni Mwandishi  wa Habari Mwandamizi,  alisema kuwa Miongoni mwa  njia Bora za kulinda Afya Kwa Wanawake na Wasichana ni vyema wazazi kujiwekea Utamaduni wa kuchunguza Watoto Afya  za watoto wakike  katika  Sehemu za Viungo vya Uzazi  ili kuweza  kubaini endapo kutakuwa  Mabadiliko  katika viungo vya uzazi  kwa Watoto wao na kuweza kupatiwa Matibabu Katika hatua Za Awali wanapobainika kuwa na Magonjwa ya Afya ya Uzazi. 
Nae  Sheik Abdalla  Nassor Abdalla  (Almaul)  kutoka Jumuia ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA )   Amesema  Afya ya Uzazi iliyo Salama  kwa Wanawake inahitaji  Maandalizi ya Mapema katika  Dini  Utamaduni na Mazingira ikiwemo Chakula Malazi Malezi na Makuzi kwa  watoto, Wanawake na wanaume. 
      Sheikh Abdalla Nassor Abdalla Maul -  JUMAZA 
Mafunzo hayo ya siku 3  yaliondaliwa na Tamwa Zanzibar kwa Kushirikiana na TAMWA Tanzania kwa Ufadhili wa  Shirika la Well Spring  juu ya  Haki ya Afya ya Uzazi kwa Wanawake na Wasichana Mjini  na Vijijini yamefanyika katika Ukumbi wa Ofisi za Chama hicho Mkanjuni Chake Chake Ambapo Waandishi hao walijengewa Uelewa juu ya Elimu ya Afya ya Uzazi, Hedhi salama, Saratani ya Matiti, Saratani ya Shingo ya Mlango wa Kizazi, Uzazi Wa Mpango, Mazingira ya Kidini  kiutamaduni juu ya Afya ya Uzazi, Maradhi ya kujamiiana, Mimba za Umri Mdogo, Ndoa za Mapema Pamoja na   Lishe  bora kwa mama wajawazito na watoto. 

Mwisho. 







 








.

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI