MKURUGENZI BARAZA LA MJI WETE "NITASIMIA UJENZI SOKO MZAMBARAUNI KUSOGEZA KARIBU HUDUMA KWA WANANCHI

  Na AMINA AHMED MOH’D,   PEMBA. 

KUFUATIA Maombi na kilio cha Muda Mrefu  kwa   Wakaazi Mzambarauni takao   Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba juu ya kujengewa Soko katika Kijiji  chao Hatimae  Uongozi wa  Baraza la Mji wete Umepitisha Azimio  la kujengwa  soko  kijijini Hapo. SALMA ABUU HAMAD MKURUGENZI BARAZA LA MJI WETE

 Adhimio hilo limepitishwa na Mkurugenzi wa Baraza la Mji  Wilaya ya Wete  Salma Abuu Hamad  kwa kushirikiana na Madiwani wa wilaya ya Wete  Ambapo  amesema adhimio hilo limelenga kuwaondoshea Usumbufu Wananchi. 
 

Aidha Mkurugenzi huyo alisema  kuwa Kupitishwa kwa Adhimio hilo kumetokana  na Maombi ya Muda Mrefu kutoka kwa wananchi wa Mzambaruni  Kuhitaji soko karibu na Maeneo yao ambalo litawasaidia kurahisisha upatikanaji wa bidha na kuwaondoshea usumbufu wa kufata bidhaa maeneo ya mbali. 

"Mlikuwa mnaleta sana Barua  nyengine  kabla hata mimi sijawa mkurigenzi, Ombi na kilio chenu mnahitaji Mjengewe soko,  Hapa Mzambarauni, lakini leo sisi kama uongozi tumeamua  kupitisha azimio la kujengwa meadi hapa mzambaraunitakao na tumepitisha uamuzi huo baada ya kuona  katika kijiji hichi na vijij jirani hakuna soko la karibu na lililopo halikidhi haja. " Alisema 

Katika hatua nyengine Mkurugenzi huyo M alieleza kuwa Kwa Baraza la Mji Wete linaendelea na shughuli  mbali mbali za kuimarisha huduma za  wananchi  ikiwa  ni pamoja na ujenzi wa sehemu za kukaa Abiria katika maeneo mbali mbali ya Wilaya ya hiyo ili Kuondosha usumbufu wanaoupata Abiria.

" Kwa Sasa baraza la Mji Wete limeweza Kujenga vibanda Kwa ajili ya kupumzikia abiria katika maeneo mbali mbali ya Wilaya ya Wete na hii imeweza kuleta faraja Kwa wananchi wetu kwani walikuwa wanahangaika sana wakati wakisubiri Usafi katika vituo vya gari na Tunazidi kuimarisha  na kuongeza vituo hivyo maeneo mbali mbali ," alisema Mkurugenzi.

  Mwenyekiti wa Baraza la Mji Wete Zulfa Abdalla Said alieleza kuwa endapo soko Hilo litajengwa na kukamilika litasaidia kutoa fursa za Ajira kwa  vijana walio wengi na kuwasaidia kujikimu  kimaisha. 

Ni kweli Uongozi wa Baraza umedhamiria na umeshapitisha Adhimio hilo na Tunatarajia kujenga soko la kisasa ambalo litakidhi mahitaji ya watu wote  na pia kuzalisha fursa za vijana kujiajiri na kujipatia kipato chao. 

Akizungumzia juu ya Suala hilo  Diwani wa wadi ya Pandani Khalid Hamad Ali alieleza kuwa mipango ya ujenzi wa soko Hilo umekamilika na hivyo uongozi hautorudi nyuma katika kutekeleza suala hilo ambapo amewataka wanachi kuwa tayari kutoa mashirikiano katika kulifanikisha suala hilo.
  Wakizungumza baadhi ya wananchi wa Shehia ya Mzambarauni  wameuomba uongozi huo wa baraza la mji Wete kutosikiliza kauli za baadhi ya wananchi wanaotufisha nyuma maenedeleo katika Wilaya hiyo. 

 "Ni faraja kwametu kuona Baraza la Mji Wete limedhamiria Kujenga soko la kisasa katika eneo  la mzambarauni takao jambo hili  litaweza kuinua Hali ya Uchumi katika eneo  letu kuna fursa zitapatikana , Alisema Said Mbarouk Ali mkaazi wa Mzambarauni. 

 Ali Abdalla Chande Alisema kuwa Wananchi wa kijiji hicho wanahitaji zaidi maendeleo ambayo yatawasaidia kuwapa fursa mbali mbali  za kujiendeleza kimaisha. 

"Hamu kubwa kijijini kwetu ni Maendeleo endelevu ambayo yatatusaidia   kutukomboa lakini kuacha Alama kwa vizazi katika Kujiendeleza kiuchumi  Soko ni jambo moja wapo la Maendeleo tunakupongeza Mkurugenzi kwa uamuzi huo wenye maslahi kwetu tunaahidi kukuunga mkono kwa nguvu zetu zote. 

"Niupongeze uongozi wa Baraza la Mji Wete Kwa kufikiria Kujenga soko katika Kijiji chetu, hii inaonesha dhahiri kuwa uongozi uliopo unajali wananchi wake kwani jambo hili ni njia moja wapo ya kupata maendeleo, hivyo Kwa Umoja wetu Wana Mzambarauni tunasema kuwa tuko tayari kujengewa soko na hili halina mjadala wowote. Alisema Salama Saidi Khamis . 

 Azimio hilo la kujengwa soko la  kisasa kijijini humo kwajili ya kurahisha upatikanaji wa huduma na uuzaji wa bidhaa  kwa wananchi wa Mzambarauni sambamba na maeneo jirani unatarajiwa Kutekelezwa  muda wowote ndani ya kipindi  hiki cha 2023/2024.

Mwisho.



Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI