Posts

Showing posts from March, 2023

WANANCHI :VIONGOZI WANAWAKE WANAO UWEZI KUSHIKA NAFASI ZA JUU.

Na Khadija Rashid Nassor Pemba WANANCHI kisiwani Pemba wamesema ipo haja kwa wanawake kujitoa kushiriki katika ngazi za maamuzi ipaswavyo kwani ni wachangiaji wazuri wa maendeleo nchini. Wakiz ungumza na mwaandishi wa habari wakaazi wa wadi ya Michenzani wamesema kuboreka kwa miundombinu ya barabara kijiji cha shangini ambayo imetataliwa na juhudi za diwani mwanamke Mashavu Juma Mbarouk kupitia mfuko wa jimbo imekua chachu kwa mama wajawazito na wazee kufikia huduma ya afya kwa urahisi. Mwanajamii Fatma Mohd amesema kadhia hiyo imedumu kwa miaka kadhaa hali iliyopelekea kwa wanawake wajawazito kujifungua njiani na hata kupoteza maisha ya watoto wao. Kwa upande wao Rehema Omar Salim Ali wamepongeza juhudi za diwani huyo kutakana na hatua anazozichukua kutatua changamoto hiyo ya muda mrefu kwani imewasaidia wanajamiia kufika kwa urahaka katika vituo vya afya. Mashavu Juma Mbarouk Diwani wa wadi ya Michenzani amesema juhudi hiyo imekuja baada ya kuguswa na changamoto hiyo na kusimama kwa ...

WANANCHI PEMBA WAFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA VIONGOZI WANAWAKE.

NA AMINA MASSOUD JABIR.  Pemba.  WANAJAMII Wilaya ya Mkoani wamewapongeza madiwani wanawakew wilayani humo kwa umoja wao na utendaji wa kazi zao lengo kuletea maendeleo endelevu.Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema viongozi wanawake ni chachu ya maendeleo kwani wapo mstari wa mbele kutatua changamoto zinazowakabili ndani ya jamii. Rehema Juma Othman na Maimuna Haroub Sheha, kutoka kijiji cha kizungu shehia ya Michenzani wamesema kupitia jitihada za diwani wa wadi ya michenzani mashavu juma mabrouk zimepunguza tatizo la barabara kutoka michenzani kwenda kijijini kwao jambo linaloashiria maendeleo kupitia kiongozi huyu. Nao, Salim Kombo na Tabia Makame wanajamii shehia ya kangani wamesema kupitia diwani mwanamke wa Wadi hiyo Mayasa changamoto ya maji imekuwa hostiria kijijini hapoSheha wa Shehia ya Michenzani Juma Nassor amesema juhudi za viongozi hao ni za kupigiwa mfano kwani zimekua hamasa ya kubadilisha mitazamo kwa jamii wanaopi...

WANAJAMII MTENG’OMBE,MIAMBONI WAMPATANO MWAKILISHI JIMBO LA CHAMBANI.

Na Khadija Rashid Nassor Pemba Wanajamii kijiji cha Mtengombe na Miamboni Wilya ya mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba, wameshukuru juhudi zinzochukuliwa na Mwakilishi wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo katika kuwaletea maendeleo. Hayo yamezungumzwa na mwanajamii, Kaije Faki na Rajab Said Mohd wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao Mteng’ombe wamesema, hawajawahi kufikiwa na huduma ya umeme tangu Mapinduzi ya mwaka 1964 lakini  kupitia  kiongozi mwnmke Bahati Khamis  imekuwa faraja kwao kwani amekua nao bega kwa bega hadi huduma hiyo ilipopatikana. Bahati Khamis Kombo Mwakilishi Jimbo la Chambani amesema, ameamua kulivalianjuga suala hilo la umeme  kutokana na umuhimu wa umeme katika jamii. Miza Hasan Faki katibu tawala Wilaya ya Mkoani ambae pia ni mwanaharakati Wilayani humo amesema kiongozi Bahati Khamis Kombo amekua na jicho la kuona mbali hivyo ni vyema kwa jamii kuthamini juhudi zake ili kupata maendeleo zaidi. Sheha wa shehiya ya Ngw...

WANANCHI MKOA WA KASKAZINI PEMBA WAVUTIWA NA MBUNGE MAIDA

Na Khadija Rashid Nassor Pemba Wananchi Mkoa wa Kaskazini Pemba wamepongewza juhudi zinazochukuliwa na Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Kaskazini Pemba Maida Hamad Abdalla Katika kuwaletea maendeleo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi Saumu Moh’d Said Diwani wa kuteuliwa Jimbo la Wingwi na  moh’d haji mwanajamii shehiya ya micheweni wamesema, kiongozi huyu amekua akijitoa kwa moyo mmoja katika kusaidia jamii bila kujali itikadi za dini wala siasa jambo limechangia chachu ya maendeleo Mkoani wa Kaskazini Pemba. Wameongeza kuwa, juudi zake ni nyingi kwani amekua akiwafikia hadi wanajamii wa tabaka la chini kujua changamoto zinazowakabili na kuwapatia suluhisho muafaka na kwa muda hitajika kwani hivi karibuni wamepatiwa vyarahani 14 lengo kubwa wanawake wilaya y micheweni kujikwamua . Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahaya amesema anapata mashirikiano ya kila hatua na kiongozi kutoka kwa bi Maida ili kuwapatia maendeleo wanajamii jambo linalomuongezea hamasa na ari kwenye...

MWAKILISHI BAHATI AWEZESHA ELIMU YA UJASIRIAMALI KWA WANAWAKE.

Na Amina Massoud Jabir Pemba.  WANAWAKE Jimbo la chambani wamesema juhudi zinazochukuliwa na Mwakilishi wa jimbo hilo za  kuwajengea uwezo wa kujiajiari ambapo ni moja ya mambo muhimu yakupigiwa mfano katika harakati za kuleta maendeleo nchini. Wakizungumza kwa nyakati tofauti Hadia Ismail na Nuwaira Karim wamesema elimu ya utengenezaji wa Medera ya batiki imebadilisha maisha yao kwani kwa sasa wameweza kujiajiri. Wanasema Nuwaira na Karim na Hadia Ismil,   “ jitihada zinazochukuliwa na kiongozi  mwanamke Bahati Khamis ya kuwapatia elimu ya ujasiriamali imewatoa mashimoni kwani wamejikomboa na umasikini na hata kuachana na utegemezi kwa wenza wao”. Kwa upande wake Mwakilishi Bahati Khamis Kombo amesema hatua hiyo imekuja baada ya kuona fursa ya ujasiriamali na jinsi inavyokomboa wanawake na vijana na hatimae kuondokana na utegemezi, pia ni chanzo cha kushiriki kwenye ngazi za maamuzi sambamba na kuchangia kwenye pato la taifa. “Nikiwa napitia video kwenye mitandao ya...

WANAWAKE WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUTUMIA VIZURI TEKNOLOJIA ILI KUJINUFAISHA KATIKA BIASHARA ZAO.

Image
NA  MASSOUD JUMA , UNGUJA. Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mheshmiwa Mgeni Hassan Juma amewataka wajasiriamali wanawake kutumia vizuri teknolojia na mitandao ya kijamii  na kuangalia ni kwa namna gani teknolojia hiyo inaweza kuwasaidia kukuza biashara zao na ustawi wa jamii kwa ujumla. Mheshmiwa Mgeni alitoa wito huo wakati  akifungua rasmi Jukwaa la pili la wajasiriamali Zanzibar lililoandaliwa na taasisi ya The Warrior Women Foundation lililofanyika siku ya Jumamosi ya tarehe 11 mwezi wa 3 mwaka 2023  huko katika ukumbi wa Bolilo Bwawani Mjini Unguja. Katika shughuli hiyo Mheshmiwa Mgeni aliwaasa wajasirimali kujiamini na kusimama imara katika kutekeleza majukumu yao na shughuli mbalimbali za ujasiriamali. Katika jukwaa hilo Mheshmiwa Mgeni alisema kuwa kuna changamoto kubwa ya masoko kwa wajasiriamali wa zanzibar ambalo linasababishwa na vitu mbali ikiwemo namna ya kuhifadhi bidhaa,utafutaji wa rasilimali na nyenginezo , hivyo aliwataka w...

AFYA YATILIWA MKAZO KWA WANAWAKE

NA ASIA MWALIM  UNGUJA.  KATIBU Mkuu Wizara ya Kazi na Uwezeshaji, masuala ya kazi na Uwezeshaji Zanzibar, Maryam Juma Abdallah, amesema bila ya wanawakwe kuwa na afya nzuri, hawawezi kujenga uchumi imara wa nchi. Aliyasema hayo wakati akikabidhi taula za kike, nguo za ndani na sabuni kwa wanafunzi 145, kutoka kituo cha kinamama cha umeme wa jua (Barefoot College) na Taasisi ya Dnata, ikiwa ni miongoni mwa harakati za kuadhimisha siku ya wanawakwe duniani, huko skuli ya Matemwe Kijini, Mkoa wa Kaskazini Unguja.  Alisema wanawake ni viongozi na walezi wa familia wanapaswa kutunza na kuimarisha afya zao kwa lengo la  kufikia maendeleo yao na taifa kiujumla. Naibu alisema, Zanzibar kama zilivyo nchi nyengine duniani inasherehekea siku ya wanawakwe, kutokana na umuhimu wake wa kumuwezesha mwanamke kupiga hatua muhimu za kimaisha na kukumbusha jamii juu ya haki za wanawake. Alieleza kuwa hatua ya kugawa vifaa na kutoa elimu ya afya skulini hapo, ita wawezesha wanafunzi wa...

Shamra Shamra Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani Yaleta Faraja kwa Wanafunzi 300 Wakike Pemba.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA.  JUMLA  Ya wanafunzi Wakike  300  Wa Skuli Za Sekondari Msuka Na Chamabani Kisiwani Pemba  Wamepatiwa  Elimu Juu ya  Mafunzo ya Hedhi Salama, Ukatili wa kijinsia, Pamoja na Haki ya Hedhi salama  kwa Mwanafunzi wa Kike, ambapo 233 kati ya Hao wamepatiwa  Taulo za Kike  Zenye uwezo wa kudumu Miaka Miwili Kutoka   ikiwa ni  Shamra shamra Za kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani inayoadhimishwa Kila ifikapo  Tarehe 8  Mwezi wa 3 Duniani Kote. Elimu  pamoja na Msaada wa Taulo hizo kwa Wanafunzi hao umetolewa Na Shirika lisilo la Kiserikali La Smile for Community  ikiwa ni katika utekelezaji wa Mradi wake wa Run for Binti Marathon, ambao Umefadhiliwa na Shirika la Msaada  wa Kisheria Legal Services Facility unatekelezwa kwa  LSF na kyfanya kazi kwa kushirikana na  Kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia wizara ya  Maendeleo ya Jamii ...

Wizara ya Kilimo Zanzibar yaridhishwa Utekelezaji wa AGRI-CONNECT kuwainua Wakulima

Image
Na GASPARY CHARLES   PEMBA  WIZARA ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar imepongeza hatua zinazochukuliwa na wadau wa maendeleo katika kukuza na kuimarisha thamani ya kilimo cha Viungo, Mboga na Matunda Zanzibar kupitia miradi inayotekelezwa nchini. Hayo yamebainika kufuatia ziara ya kutembelea wakulima wanufaika wa miradi inayotekelezwa na programu ya AGRI-CONNECT Tanzania kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) iliyofanyika Kisiwani Pemba kwa lengo la kutathimini hali ya utekelezaji wa programu hiyo katika kukuza uzalishaji wa mazao hayo kwa wakulima. Katika ziara hiyo iliyoongozwa na Dkt. Suleiman Shehe, afisa mkuu wa Utafiti wa wizara hiyo, alisema juhudi kubwa zinazochukuliwa na watekelezaji wa miradi hiyo inasaidia kuongeza thamani ya mazao hayo ambayo kwa muda mrefu yamekuwa hayapewi kipaumbele kama sehemu ya shughuli muhimu za kiuchumi kwa wananchi na taifa. Alifahamisha kuwa wananchi wengi walikuwa bado hawaoni umuhimu wa kujiingiza katika ...