Shamra Shamra Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani Yaleta Faraja kwa Wanafunzi 300 Wakike Pemba.

NA AMINA AHMED MOH’D PEMBA. 

JUMLA  Ya wanafunzi Wakike  300  Wa Skuli Za Sekondari Msuka Na Chamabani Kisiwani Pemba  Wamepatiwa  Elimu Juu ya  Mafunzo ya Hedhi Salama, Ukatili wa kijinsia, Pamoja na Haki ya Hedhi salama  kwa Mwanafunzi wa Kike, ambapo 233 kati ya Hao wamepatiwa  Taulo za Kike  Zenye uwezo wa kudumu Miaka Miwili Kutoka   ikiwa ni  Shamra shamra Za kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani inayoadhimishwa Kila ifikapo  Tarehe 8  Mwezi wa 3 Duniani Kote.

Elimu  pamoja na Msaada wa Taulo hizo kwa Wanafunzi hao umetolewa Na Shirika lisilo la Kiserikali La Smile for Community  ikiwa ni katika utekelezaji wa Mradi wake wa Run for Binti Marathon, ambao Umefadhiliwa na Shirika la Msaada  wa Kisheria Legal Services Facility unatekelezwa kwa  LSF na kyfanya kazi kwa kushirikana na  Kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia wizara ya  Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto ,   Maisha Bora Faundation ZMBF, Taasisi ya Weza, Pamojana Taasisi ya Waja Mama. 
 
 Akizungumza na  habari hizi mara baada ya kumaliza kutoa  Elimu kwa Wanafunzi hao  Afisa Mradi kutoka Shirika la Smile For Community  Anet Kiao  Alisema kuwa lengo la kutoa Elimu juu ya Suala hilo  ni  kuhakikisha Wanafunzi wakike waliopo Maskulini  wanakuwa Salama Wanapokuwa katika Kipindi Cha Hedhi  Na kiweza kuendelea vyema na Masomo bila kupata usumbufu na wasi wasi wowote utakaowapelekea kushindwa kufanya vizuri katika Masomo yao na badala yake waweze kuedelea kubaki skuli kuendelea na Masomo yao.
 
"Lengo la kugawa Taulo hizi kwa wanafunzi wakike ambao wameshafikia umri wa balehe ni kuona wanaondokana na usumbufu  wanaokumbana nao wakati wa Hedhi, wanapokuwa Shuleni  ambao kwa namna moja ama nyengine hupelekea kukatisha Masomo yao au kushindwa kufanya vizuri Darasani wanapokuwa katika hali hiyo kupitia Elimu hii tuliyoitoa kwa wanafunzi hawa watajua  sasa nini wafanye wanapokumbana Na suala hili. 


Akitoa Elimu ya  Kisheria kwa Wanafunzi hao Alphonce  Mbarambe Gura  Mwanasheria Kutoka  Taasisi ya Legal Service  Facility Zanzibar  Aliwataka Wanafunzi hao Kutokaa kimya Wanapokumbana changamoto yeyote inayotokana na Hedhi  kwa vile Suala hilo linatambulikana  kikatiba  kama ni haki ya Msingi kati ya  Haki za Binaadamu kwa vile Suala  hilo linagusa Moja kwa Moja utu wa Wanafunzi hao Wakike. 

"Lazima suala la Hedhi Salama liangaliwe kwa Upana wake Hivyo ni lazima Watoto wakike Wenyewe  muweze kujua ni jinsi gani suala la hedhi Salama Ni Muhimu kwenu, Mna haki ya kupata vifaa vya kujisitiri kwa gharama nafuu ambavyo ni salama , kupata Mazingira Wezeshi Skuli na Nyumbani ya kubadilishia nguo maji  ya  Salam vtite hivi Mnahaki ya kudai  Endapo mtakuwa Skuli  ama Majumbani. 

Nao Baadhi ya Wanafunzi waliopatiwa Elimu Juu ya Masuala hayo Akiwemo Fatma Abdalla Mbarouk  Kutoka Skuli ya Msuka Sekondari Pamoja  Ruwaida Salum Hamad  Wamewashukuru  Wafadhili hao waliojitolea kuwafikishia Elimu hiyo  ambapo wamesema itawasaidia katika kukabiliana na changamoti ambazo walikuwa wanakumbana  nazo awali kabla ya kupata Elimu hiyo. 

 Tunaahidi kuifanyia kazi Elimu hii ili isiwe kikwazo tena kwetu kupata
 Changamoto zinazopelekea kuwa watoro tunapokuwa katika Hedhi Alisema Fatma Abdalla Mbarouk. 
Tunawaomba na Mashirika Mengine pamoja na Taasisi waoge Mfano huu mzuri ambao utasaidia kufanikisha malengo ya Wanawake tuliyojiwekea Kwani bado Elimu hii na Taulo hizi Wapo wanafunzi wengi ambao wanazihitaji katika skuli nyengine Akaongeza Ruwaida. 

 Elimu iliyotolewa kwa wanafunzi hao ni Pamoja na na Namna ya kujikinga na kutambua Viashiria vya Ukatili wa kijinsia, Matumizi salama ya Taulo za kike za kufua, Pamoja na Haki ya Kisheria ya Afya ya Hedhi Salama kwa Wanafunzi wa kike Mskulini ikiwa ni shamra shamra za  kuelekea Siku ya Wanawake Duniani ambapo ugawaji wa Taulo hizo  Zimepatikana kupitia kupitia Kampeni ya Twende pamoja  Run for Binti  Marathon. 
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI