Posts

Showing posts from August, 2023

WANANCHI ZANZIBAR WAPONGEZA UONGOZI WA DK SAMIA.

Image
NA MWANDISHI WETU, UNGUJA. WANANCHI wa Zanzibar wamesema,Tanzania wamepata kiongozi ambae Taifa likimuenzi wataweza kuendelea kupiga hatua mbalimbali za kimaendeleo na hatua bora zaidi. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati mbalimbali, wananchi hao wamesema, uongozi wa Dk. Samia umekuwa ukiwashirikisha wananchi wote ambapo ni sifa pekee ya kiongozi aliyekuwa bora na anapaswa kuenziwa na taifa. Mmoja ya wananchi hao, ambae ni mzee wa maskani ya kachorora, Mohamed Mussa Seif (mkobani) alisema, endapo kiongozi huyo akiendelea kupewa ushirikiano maendeleo zaidi yatapatikana kwa wananchi ikiwemo kuwanufaisha mmoja mmoja. Alisema, Dk. Samia, amekuwa akitambua changamoto mbalimbali za wananchi kwani uongozi wake umetokea chini na alikuwa bega kwa bega na watu na ni mpenda maendeleo na hana ubaguzi wa dini, chama wala rangi ya mtu. Hivyo, alisema utendaji wa kazi wa Rais. Dk Samia hauna shaka kwani ni kiongozi mzoefu na mwanamapinduzi wa kweli na mpenda haki kwa watu...

HOSPITALI 10 ZA JENGWA UNGUJA NA PEMBA UONGOZI WA AWAMU YA SITA.

Image
NA MWANDISHI WETU, UNGUJA  SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Afya, imesema kupitia fedha za UVICO 19 zilizotolewa na serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wake Dk. Samia Suluhu Hassan zimejenga jumla ya hospital 10 katika wilaya ya Unguja na Pemba na hospitali ya mkoa moja iliyokuwepo Lumumba Mjini Unguja. Akizungumza na waandishi wa habari, Ofisini kwake Mombasa, Afisa kitengo kinachosimamia mradi wa ujenzi wa hospitali na miradi yote ya ujenzi wizara ya Afya Zanzibar, Amina Habibu, alisema, hospitali hizo zitakuwa zinatoa huduma mbalimbali ikiwemo za mama na watoto. Alisema, ujenzi wa hospitali hizo zimekuwa zinakwenda vizuri na nyengine zimeshafunguliwa na huduma zinaendelea katika hospitali jambo ambalo limewarahisishia wananchi upatikanaji wa huduma zilizokuwa bora na muhimu. Alisema, kupitia fedha hizo wizara zimenufaika ambapo hivi sasa wamekuwa wakitoa huduma nyingi ikiwemo za dharura. Aidha alisema kabla ya ujenzi wa hospitali hizo wananc...

CCM YAAHIDI KUIMRAISHA MAZINGIRA MAZURI KWA WANAFUNZI

Image
NA OMPR ZANZIBAR.  SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa Wanafunzi ili kurahisisha upatikanaji wa elimu bora nchini. Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Hemed Suleiman Abdulla ameyasema hayo wakati akizungumza na Viongozi , wana CCM na Wananchi wa Jimbo la Donge, Mahonda na Bumbwini katika ziara yake ya kukiimarisha Chama Mkoa wa Kaskazin Unguja. Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imedhamiria kuwawekea mazingira mazuri Wanafunzi ikiwemo ujenzi wa Skuli za ghorofa, Madarasa, na Vifaa vya kufundishia pamoja na kuzingatia maslahi ya Walimu. Amesema Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali itajenga Dakhalia kubwa katika Wilaya zote za Zanzibar pamoja na Dakhalia kwa skuli zenye uhitaji ili Wanafunzi waweze kusoma vizuri na kuweza kukuza ufaulu nchini.  Hemed ameeleza kuwa Mkoa wa Kaskazini Unguja umebahatika kupata Miradi mingi ya maendeleo inayopelekea kuzalisha ajira kwa Vijana pamoja na kukuza Uc...

MJUMBE KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM AWAASA KUACHA MAMBO HAYA WANACHAMA

Image
  Na Mwandiahi Wetu  (OMPR),  UNGUJA  MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amewataka wanachama wa Chama Cha Mapinduzi kuachana na watu ambao wanawabeza viongozi kwa kuwakashifu na kuwasema vibaya juu ya jitihada zao wanazozichukua za kuwaletea maendeleo wananchi . Ameyaeleza hayo wakati akizungumza na viongozi, wanachama wa CCM na wananchi wa Majimbo ya Chaani, Mkwajuni na  Tumbatu Wilaya ya Kaskazini A ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kuimarisha Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Unguja.  Amesema wapo baadhi ya Viongozi wa Vyama vya upinzani ambao wana malengo ya kukichafua chama na viongozi wake hivyo ni vyema kwa wana CCM kuwapuuza na kuendelea kuwa wamoja na kukiimarisha Chama kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo. Amesema majimbo yaliyomo ndani ya Mkoa wa Kaskazini Unguja yatabaki kuwa ni ngome ya CCM na hatotokea mpinzani yoyote kuongoza katika Majimbo hayo hivyo umoja, upendo na mshi...

UKOSEFU WA MALEZI YA BABA YAELEZWA KUCHANGIA NDOA ZA MAPEMA PAMOJA NA MIMBA ZA UMRI MDOGO KWA WATOTO WA KIKE.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA.  WAZAZI WENGI WAKIUME WAMEKUWA wakiwekeza nguvu zao zaidi kuwashughulikia Watoto wanapokuwa Wadogo  lakini  akifikia Kuanzia Miaka 13 na kiendelea tu bhasi nguvu za kuwashughulikia katika Malezi zinaanza kupungua wakati kuanzia Umri huo   ilipaswa Usimamizi Uongezeke Mara Mbili Zaidi  kwa Watoto wakike Na Wakiume mana Mabadiliko Ya Tabia huanzia Hapo".   Hayo Ni maneno ya Nadhira Khamis Iddi Ambae  Nadhira Khamis Iddi aliyezaliwa katika kijiji cha Mgogoni Konde  Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba, mwenye umri wa miaka 21 kwa sasa ni Mama na Mlezi wa Watoto wake wawili wa Kiume aliowapata katika Mwaka 2017/ 2019 Iliyopita baada ya kupewa ujauzito na kuozeshwa Mume  akiwa na umri wa miaka  16. Nadhira ambae alizaliwa mwaka 2003 kwa sasa anaishi Mjini Chake Chake akiwa na wanawe hao pamoja na wazazi wake wote wawili baba na mama ambao walihamia miaka mingi iliyopita. Nadhira ambaye alis...

VIONGOZI VYAMA MBALI MBALI VYA SIASA WAJENGEWA UWEZO JUU YA KUANZISHA SERA YA JINSIA KATIKA VYAMA VYAO AMBAYO ITATEKELEZWA KWA VITENDO.

Image
NA AMINA AHMED MOH’D, PEMBA.  ZAIDI  ya Viongozi 15 kutoka vyama mbali mbali vya Siasa  kisiwani  Pemba wamepatiwa Mafunzo maalum   kujengewa uwezo juu ya Kuanzisha na kuifanyia  kazi Sera ya jinsia Katika Vyama Vyao.  Mafunzo hayo ya Siku moja yaliondaliwa na Chama  cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar kwa kushirikiana na Jumuia ya Utetezi wa kijinsia  na Mazingira Pemba  PEGAO   yamefanyika Leo katika ukumbi wa Chama hicho Mkanjuni Chake Chake.  Akizungumza katika Mafunzo hayo Mratibu wa chama hicho Pemba Fat-hiya Mussa Said Amesema lengo la Mafunzo hayo kwa Viongozi wa vyama vya Siasa ni  kusaidia Kuongeza  ushiriki wa  wanawake Katika Democrasia kwa kufuata Utaratibu maalum utakaotambulika kisheria, kusimamiwa pamoja na kuweza kutekelezwa  kupitia  Sera ya Kijinsia  ndani ya Vyama. " Baada ya kuona Changamoto kubwa ndani ya Vyama vya Siasa ni kukosekana...

AFYA YA UZAZI SALAMA KWA WANAFUNZI WA KIKE HAIWEZI KUFIKIWA IWAPO CHANGAMOTO HIZI HAZITOANGALIWA KWA UMAKINI NA KUPATIWA UFUMBUZI WANAPOKUWA KATIKA KIPINDI CHA HEDHI.

Image
AMINA AHMED MOH’D, PEMBA. ( 0719859184)     Hedhi salama ni hali ya Mwanamke au msichana aliye katika hedhi kuwa na uwezo wa kupata kifaa salama na nafuu cha kuzuia Damu, kupata Maji Safi na salama ya kujisafishia, kuwa na maliwato yenye mlango kwa ajili ya kujisitiri na kubadilishia vifaa vyake pia kupata sehemu sahihi ya kutupa au kutunzia kifaa chake baada ya kukitumia     KAMA Hiyo ndio maana halisi ya Hedhi salama bila shaka Bado kuna mengi yanahitaji kuangaliwa na wadau Serikali na wote wanaopenda Maendeleo Bora ya Afya ya Uzazi na  Elimu kwa watoto wa kike.  Wadau wengi hujali  Afya ya mtoto wa kike kwa kutoa  Elimu  ya Afya ya Uzazi kwa baadhi ya wanafunzi waliofikia  Umri wa Kupata Hedhi kwa  kugawa Sabuni pamoja na Taulo zakike lakini bado kuna changamoto Nyingi ambapo zisipoangalia kwa jicho la Tatu na Wadau pamoja na Serikali kwakuwekewa mkakati Endelevu Kugawa Taulo kutoa Elimu na Sabuni hizo  hautokuwa Msaada...

ALIENUSURU MAISHA NA UHAI WAKE KWA KUFANYA MAZOEZI AISA JAMII KUWEKA KIPAUMBELE SUALA HILO KUONDOKANA NA MARADHI YASIOAMBUKIZA.

Image
NA - AMINA AHMED MOH’D, PEMBA  (0719859184)  . MAZOEZI NI AFYA" Ni Msemo ambao hutumika mara nyingi katika  Kuhamasisha  Mazoezi Ili Kuondokana na Maradhi Yasioambukiza Ikiwemo  Shinikizo la Damu Kwa Jina la kitaalamu (Pressure) Sukari, Ugonjwa Wa Moyo Kiharusi, Saratani na Mengi Mengineyo ambayo Yanaendelea kuchukua Roho za Watu Siku hadi Siku .  Inathibiti kwa Vitendo  Kauli hii Maarufu katika vinywa vya Watu wengi kufuatia kutengamaa kwa Afya ya Muhammed Ali Omar  Mkaazi Wa Gombani  Chake Chake ambae Amenusuru Maisha yake baada ya kuamua kufanya Mazoezi.  Mpendwa Msomaji leo Maalum  Mwandishi wa Makala hii Amezungumza na  Muhammed Ali Omar Umri  39 ambae Mkaazi wa Gombani Chake Chake  Kusini Pemba ambae Kutokana na kufanya Mazoezi ameweza  kuondokana na  Magonjwa Nyemelezi yasioambukiza  yaliokuwa Yakihatarisha Afya na Uhai wake.  " Mazoezi ndio Tiba Sahihi Kwa hali yangu ilivyokuwa mimi na Fami...

MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM AKABIDHI KADI KWA WANACHAMA WAPYA

Utekelezaji mzuri wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndio kunakowavutia wananchi na wapinzani kujiunga kwa wingi na Chama  Chama Cha Mapinduzi ili kuzidi kukiunga mkono chama hicho.   Akikabdhi kadi za CCM kwa wanachama wapya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amewataka viongozi na watendaji wote wa CCM kuhakikisha wanatengeneza mazingira mazuri ya kukiimarisha chama, kuwaweka wanachama pamoja na kuachana na makundi ndani ya chama ambapo kufanya hivyo kutasaidia idadi ya wanachama kuongezeka na CCM kupata ushindi katika ngazi zote ifikapo mwaka 2025.   Mhe Hemed ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema sifa kuu ya kiongozi bora ni kusimamia haki na usawa kwa anaowaongoza sambamba na kutatua changamoto zinazojitokeza majimboni mwao. Aidha ameeleza kuwa Amani na utulivu ndio nguzo kubwa ya maendeleo nchini ambapo katiba ya CCM imemtaka kila mwana CCM na mtanzania kusimamia jambo hilo. Amesisistiza suala la kulipa ad...

KUHESHIMU HAKI ZA BINAADAMU NI WAJIBU WA KISHERIA NA KIMAADILI KWA ASKARI..

Image
Kamishna wa Polisi Zanzibar HAMAD KHAMIS HAMAD amesema kuheshimu na kulinda haki za binaadamu na kulinda utu wa kila mtu kwa Askari Polisi sio tu ni wajibu wa kisheria bali ni sharti la kimaadili katika taaluma ya Polisi. Akifungua mafunzo ya haki za Binadamu kwa Askari wa Mikoa mitatu ya Unguja huko Ukumbi wa Chuo cha Polisi Zanzibar amesema lazima askari afanye kazi kwa karibu na raia kwa kuwa na huruma, kutonyanyasa, kulinda makundi yaliyo katika mazingira hatarishi na kuzingatia uadilifu. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jumuia ya kukabiliana na changamoto za vijana Zanzibar (ZAFAYCO) amesemema kuimarisha mfumo wa haki jinai na kupunguza vitendo vya uvunjifu wa haki za binaadamu kunaenda sambamba na kuimarisha uchumi.

WKAGUZI WA SHEHIA WAKUMBUSHWA WAJIBU WAO KWA JAMII

Image
NA OMAR HASSAN – ZANZIBAR                              07/08/2023 KAMISHNA wa Polisi Zanzibar  HAMAD KHAMIS HAMAD amesema uwajibikaji na utoaji wa haki kwa Wakaguzi wa Shehia kutaleta mabadiliko na kuunda jamii salama, imara na yenye mshikamano . Akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo Wakaguzi wa Shehia wa Mikoa mitatu ya Unguja huko Kambi ya Polisi Ziwani ameeleza kuwa uwepo wa Wakaguzi wa Shehia kunatoa matumaini kutatua matatizo ya jamii, kuzuwia na kupunguza uhalifu, kuimarisha uwajibikaji wa Polisi na kupunguza hofu ya uhalifu. Mratibu wa Mafunzo hayo Mrakibu wa Polisi Dkt. EZEKIEL KYOGO kutoka Kamisheni ya Polisi Jamii Makao Makuu ya Polisi Dodoma amesema mafunzo hayo yatawajenga uwezo Wakaguzi hao wa Shehia kuelewa vizuri Falsafa ya Polisi jamii na kuwa na uwezo wa kuifanyia kazi kwa ufanisi. Kwa upande wake VERONICA FUBILE kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP amesema shiri...

KIJANA OMAR ALIEBADILI MUELEKEO KUTOKA KUWA DEREVA WA GARI HADI MKULIMA WA MBOGA MBOGA NA MATUNDA AELEZA SABABAU ZILIZOMSHAWISHI KUFANYA HHIVYO MAAFANIKIO NI MOJA KAATI YA SABABU HIZO.

Image
NA, AMINA AHMED MOH’D - PEMBA. 0776859184  KUPITIA Siku ya Wakulima Duniani Leo Maalum Tumekuandalia Simulizi  Fupi inayomuhusu  Omar Salum Mbarouk Mkaazi wa Vitongoji Chake Chake Kijana  Alieamua   Kuacha Gari na Kushika Jembe   kuzifata Fursa Zinazopatikana kupitia Kilimo na Kupata Mafanikio.   Kijana Huyo Ambae Kwa Zaidi ya Miaka 4 Alikuwa Anajishughulisha na Udereva Wa Gari   ndogo Za kubebea  Mizigo  Amesema kuwa  katika Kipindi chote hicho Hakuna Mafanikio ya kujivunia  Ambayo ameyapata kupitia Shughuli ua Udereva.   Ni kipindi cha  Muda Mfupi Tangia Omar kuanza Rasmi shuguli za Kilimo Cha Matunda na Mboga mboga Vitongoji ambapo Kwa Sasa Ameamua Rasmi Kuwekeza nguvu Zake zote katika  shuguli za Kilimo.     Miongoni mwa Kilimoambacho Anaendelea kulima Omar ni Pamoja  Migomba, Pilipili, Matikiti, Mahindi, mipensheni pamoja na Ufugaji wa Kuku.   ...

RAIFFA ABDALLA MAKAME KIJANA ANAENDELEA KUTIMIZA MALENGO YAKE KUONESHA UTHUBUTU, SAMBAMBA NA KUJIVUNIA MAFANIKIO KUPITIA MATUMIZI SAHIHI YA MITANDAO YA KIJAMII AWAASA VIJANA KUTUMIA FURSA

Image
Na, Amina Ahmed Moh’d - Pemba     (0719859184) (minnah1202@gmail)  " SIKU ZOTE NAWAAMBIA   Vijana wenzangu Unaweza kuwa Yue ambae unataka kuwa Lakini Anza Sasa, Siri ya Mafanikio Peke  ambayo Duniani kote Ao mabilionea  namba moja   siri yao kubwa Nikuanza hakuna siri nyengine hawakuwa tu Mabilionea kwa kulala tu na kuamka". Ni Maneno ya Raiffa Abdalla Makame Mwanamke alietimiza ndoto zake  Kupitia fursa za Mitandao ya kijamii.  "Nikiwa kijana Ninandoto ambazo nimejiwekea  na furaha yangu kubwa ni kuona Zinaendelea kutimia siku hadi siku, Na zinatimia kwa Sababu Ya Utayari wangu katika kufikia Malengo niliyojiwekea, Umakini, Kujifunza kwa wengine sambamba na kutumia Fursa  zilizopo mbele yangu "Aliendelea Raiffa.  JEE RAIFFA NI NANI!  Jina Lake kamili ni kama ambavyo limesimuliwa huko juu, Ni Mtoto wa Pili kati ya watoto wa 5 wa Mzee Abdalla Makame Na Mke wake Bi Tatu Omar Juma,  Wakaazi wa Fuo...