KIJANA OMAR ALIEBADILI MUELEKEO KUTOKA KUWA DEREVA WA GARI HADI MKULIMA WA MBOGA MBOGA NA MATUNDA AELEZA SABABAU ZILIZOMSHAWISHI KUFANYA HHIVYO MAAFANIKIO NI MOJA KAATI YA SABABU HIZO.

NA, AMINA AHMED MOH’D - PEMBA. 0776859184 

KUPITIA Siku ya Wakulima Duniani Leo Maalum Tumekuandalia Simulizi  Fupi inayomuhusu  Omar Salum Mbarouk Mkaazi wa Vitongoji Chake Chake Kijana  Alieamua   Kuacha Gari na Kushika Jembe   kuzifata Fursa Zinazopatikana kupitia Kilimo na Kupata Mafanikio. 


 Kijana Huyo Ambae Kwa Zaidi ya Miaka 4 Alikuwa Anajishughulisha na Udereva Wa Gari   ndogo Za kubebea  Mizigo  Amesema kuwa  katika Kipindi chote hicho Hakuna Mafanikio ya kujivunia  Ambayo ameyapata kupitia Shughuli ua Udereva. 

 Ni kipindi cha  Muda Mfupi Tangia Omar kuanza Rasmi shuguli za Kilimo Cha Matunda na Mboga mboga Vitongoji ambapo Kwa Sasa Ameamua Rasmi Kuwekeza nguvu Zake zote katika  shuguli za Kilimo. 
 
 Miongoni mwa Kilimoambacho Anaendelea kulima Omar ni Pamoja  Migomba, Pilipili, Matikiti, Mahindi, mipensheni pamoja na Ufugaji wa Kuku.
              Omar Salum Mbarouk - Mkulima. 

 Anasema  Mvuno wa kwanza  wa Zao la Matikiti Alisema Tayari  Zimempatia Matunda kwani Tayari Amenunua  Matofali  Pamoja na mawe kwajili ya kuanza  shughuli za Ujenzi wa nyumba Yake.
 
 Kilimo kikiwa kinaendelea  kwa kijana Omar anasema Matarajio ya mafanikio  ni makubwa baada ya  Mavuno kuputia zao la Migomba kukamilika. 

 Anasema Ndizi ni Miongoni mwa Biashara yenye uhitaji mkubwa katika soko la Ndani ya Kisiwa cha Pemba lakini hata nje ya kisiwa Hicho.
 
 "Msimu wa mavuno ya Ndizi utakapowadia  Ninamatarajio makubwa kujipatia kipato cha kuendesha harakati hizi za kilimo lakini Pia  kuendeleza shughuli za Ujenzi".

 Omar amabe Amehamisha Makaazi yake  na kuamua Kupiga kambi nje  kidogo na Kijijini  kwao  Kufanya shughuli hizo  za Kilimo kwa Ufanisi Anasema Licha ya kulima Kilimo hicho lakini Pia  Ufugaji wa kuku wa kienyeji Umeanza kuimarika  kutoka kuku 5 Aluokuwa nao kabla hadi kufikia 20 ambao wote hao wanaendelea na uzakishaji wa vifaranga ambavyo muda mfupi baadae vitaweza kuwa Tija kwa uoande wake.

 Aliemshawishi Omar kujiunga na Kilimo ni Mama yake Mzazi Ambae kwa Muda mrefu anafanya shuvhuli hizo. 

"Nilihamasika kupitia Mama yangu Mzazi  bi Mkunga  anapata fursa mbali mbali  kuputia kilimo, Hamasa  ilizidi baada ya kuona   Amenunua mbuzi wawili 2 kama faida licha ya vitu vyengine mbali mbali zilizitokana na kilimo. 

Napata Mafunzo mbali mbali knamna na mbinu bora za kilimo kutoka kwa mama yangu ambae nae alichowezeshwa   na MRADI WA VIUNGO unaotekelezwa na TAMWA-Zanzibar  kwa mashirikiano kati ya , PDF, CFP kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya EU kupitia Mpango wa Agri conect. "

 Omar amewataka Vijana wenzake Kutopuuza Fursa za kilimo  na badala yake kujikita na kuwekeza katika kilimo ili kujikomboa kimaisha. 

Anasema  Kilimo kinaweza kutimiza ndoto ya kijana yeyote ambae ataamua kulivalia njuga suala hilo katika kujikomboa. 

Omar Pamoja na Mambo mengine hakusita Kuiomba Serikali  na wadau kumtembelea katika shamba lake  ili kumpatia Zaidi Elimu Ambayo itazidisha Hamasa katika kukiendeleza Kilimo. 

 Mwisho. 




Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI