Posts

Showing posts from September, 2022

MFUMO WA BENKI KUTUMIKA KULIPA VIBALI VYA NGOMA ZA UTAMADUNI MASHEHA WAPEWA AGIZO.

Image
Na AMINA AHMED  Masheha wa Shehia Wa mkoa wa kusini Pemba Wametakiwa Kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato kupitia utowaji wa vibali vya ngoma mbali mbali ili za utamaduni kwa kutumia mfumo wa ulipiaji wa benki na kusaidia serikali kuongeza na kukusanya mapato yake bila kupotea .  Akizungumza katika mkutano maalum na masheha mkoa wa kusini Pemba Katibu Mtendaji baraza la sanaa sensa filamu na utamaduni Zanzibar Dk Omar Abdalla Adam Amesema iwapo vibali hivyo vitatolewa kupitia mfumo huo wa ulipiaji ambao ni mfumo mpya wa kidigitali fedha zinazotolewa zitasaidia kutumika katika kupanga mambo mbali mbali ya serikali ambayo yatasaidia kuleta maendeleo kwa Wananchi.            Dk OMAR ABDALLA ADAM      KATIBU MTENDAJI BARAZA L BARAZA LA SANAA  SENSA SENSA NA UTAMADUNI  ZANZIBAR.   Aidha Katibu Adam amewataka Masheha hao kuendela kuhifadhi mila silka na tamaduni za kizanziba...

JUMUIA YA WAZAZI CHAMA CHA MAPINDUZI YAASWA KUWA WABUNIFU.

Image
Na AMINA AHMED.  Katibu wa Chama Cha Mapinduzi  CCM wilaya ya Chake Chake  Hassan Khatib Hassan amewasa  viongozi  Wlwatakaochaguliwa kungoza Jumuia  ya  wazazi  kuwa wabunifu  kubuni miradi ya maendeleo itakayosaidia kuendesha Jumuia hiyo mbele kimaendeleo .   Hassan Khatib Hassan. Katibu CCM wilaya ya Chake Chake.  Katibu Hassan Aliyasema hayo Alipokuwa akizungumza  na wajumbe wa  Jumuia ya wazazi  wilaya ya Chake Chake katika ghafla ya uchaguzi  wa Jumuia hiyo uliofanyik katika ukumbi wa Makonyo  Wawi Chake Chake.   Alisema Iwapo viongozi hao watakuwa wabunifu  katika Suala la miradi  ya maendeleo Chama kitaendelea kuwaunga mkono katika kufikisha mbali kimaendeleo Jumuia hiyo .  Aidha alisema kuwa matarajio ya viongozi watakaopata nafasi ya kuongoza Jumuia hiyo kwa miaka mitano katika nafasi mbali mbali ni kusimamia Jumuia hiyo na kuona Inafika mbali katika ushindani w...

UMOJA WA WANAWAKE TANZANIA UWT WILAYA YA CHAKE CHAKE WAPATA VIONGOZI WAPYA.

Image
Na AMINA AHMED  Umoja wa Wanawake Tanzania  wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya ya Chake Chake Mkoa  kusini Pemba umefanya uchaguzi   ambapo umemchagua  Bi Halima Juma Khamis Kuwa mwenyekiti mpya atakaeongoza umoja huo.   Akizungumza mara baada ya kumalizika uchaguzi huo mwenyekiti wa uchaguzi huo mafunda Hamad Rubea  amewataka waliochaguliwa kufanya kazi kwa uadilifu kutumikia jumuia hiyo.  Awali  Wakizungumza na Habari  hizi baadhi ya wajumbe   wa  mkutano mkuu Umoja wa wanawake wilaya  hiyo   Akiwemo Zuhura Mgeni othman , Aziza Yussuf  Salum   pamoja na Mwajuma Hija kipenda wamesema  Uchaguzi huo  utasaidisa kuleta maendeleo  kwa wanawake  wa umoja huo katika kutetea maslahi mbali mbali  katika ngazi za juu za Chama huku wakiwataka watakaochaguliwa kutumikia kwa uadilifu nafasi walizoziomba.  Uchaguzi  wa kupata viongozi watakaoongoza umoja ...

MSAADA WA CHAKULA WAWANUIFAISHA WANANCHI WENYE HALI DUNI KISIWANI PEMBA.

Image
Na Fatma Abrahman.  Mkuu wa mkoa WA kusini Pemba Matar Zahor masoud Ameipongeza taasisi the future life  foundation katika hatua wanazozichukua za kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum pamoja na  kuwafariji kwa kuwapatia mahijaji muhimu Ili nao kuishi kwa amani .  Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa huyo   mkuu wa wilya ya chake chake Abdalah Rashid Ali amesema kuwa kujitoa katika kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum ni jambo jema hivyo ni vyema kuniwekea hakiba ya baadae.    Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa hafla hio ya ugawaji wa msaada huo raisi wa taasisi ya the future life foundation sheikh Mbarouk Seif Salim amesema wametoa sadaka hio kwa mayatima wasiopungua 320 ambapo  lengo  ni kutoa zaidi ya kiwango hicho Ili kuwasaidia na kuwafanya wajione  kua nao ni sawa na walio na wazazi  licha ya kuondokewa na wazazi wao . Kwa upande wa wa wazazi na walezi wa mayatima hao wameishuku...

JESHI LA POLISI ZANZIBAR LATOA NENO Hili.

Image
Na AMINA AHMED.  Nawaombea aibu Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya jinai wa jeshi la Polisi Zanzibar, Kamishna Msaidizi Zubeiri Seif Chembera amesema mashirikiano makubwa wanayoyapata kutoka kwa viongozi wa ngazi mbali mbali wa serikali ya Mapinduzi kumerahisisha kazi za kuzuia matendo ya uhalifu na maskosa ya jinai kudhibitiwa kwa kiasi kikubwa katika visiwa vya Unguja na Pemba.   ACP Chembera ameyasema hao huko Makao Makuu ya jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, wakati akizungumza na waandishi wa habari kufuatia ziara yake ya siku tatu ya ukaguzi na kuagalia utendaji kazi wa jeshi hilo katika mikoa ya Kusini na Kaskazini Pemba na kueleza kuridhishwa kwake na uwajibika wa askari wa jeshi hilo katika ngazi mbali mbali.   Amesema Jeshi la Polisi Zanzibar litaendelea kushirikiana na viongozi hao ikiwemo kuifanyia kazi michango yao mbali mbali wanayoitoa katika kuboresha kazi zao za kuweza kupambana na vitendo vya uhalifu na makosa mbali mbali katika ...

WAANDISHI WASUKWA UANDISHI WA HABARI ZA MAENDELEO KWENYE JAMII

Image
  Habari zenye kuleta mabadiliko katika jamii ni chachu ya maendeleo   nchini kuhamasisha wanawake kutumia haki ya kidemokrasia na uongozi hali itakayosaidia kushiriki na kushinda kwenye ngazi za maamuzi.

DC Mjaja afungua kongamano la Amani lililoandaliwa na Taasisi ya Roots & Shoots kwa wanafunzi

Image
  Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja amesema maendeleo yakiwemo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii katika taifa lolote hutegemea kuwepo na kuimarika amani, umoja na mshikamano. Amesema wajibu kwa wananchi wote bila ya kujali dini, rangi, kabila na tofauti zao katika mitazamo ya kisiasa hivyo kila mmoja anao umuhimu wake katika kujenga misingi imara ya amani. Mjaja ameyasema hao huko katika Skuli ya Sekondari ya Moh`d Juma Pindua Mkanyageni Wilaya ya Mkoani wakati akifungua kongamano la umuhimu wa amani lililoandaliwa na Taasisi ya Roots & Shoots kwa wanafunzi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya amani duniani.   Aidha mjaja ameipongeza taasisi ya Roots & Shoots kwa shughuli zao mbali mbali wanazozifanya katika jamii ikiwemo kuwajenga wanafunzi kuwa wabunifu. Akizungumza kwenye Kongamano hilo Mratibu wa Roots & Shoots Mkoa wa Kusini Pemba Matti Ali Matti ameeleza umehimu wa kuwepo wa amani, umoja na mshikamano. Akisoma risala kwa niaba ya Taasisi hiyo Huss...