UMOJA WA WANAWAKE TANZANIA UWT WILAYA YA CHAKE CHAKE WAPATA VIONGOZI WAPYA.

Na AMINA AHMED 

Umoja wa Wanawake Tanzania  wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya ya Chake Chake Mkoa  kusini Pemba umefanya uchaguzi   ambapo umemchagua  Bi Halima Juma Khamis Kuwa mwenyekiti mpya atakaeongoza umoja huo.

  Akizungumza mara baada ya kumalizika uchaguzi huo mwenyekiti wa uchaguzi huo mafunda Hamad Rubea  amewataka waliochaguliwa kufanya kazi kwa uadilifu kutumikia jumuia hiyo. 

Awali  Wakizungumza na Habari  hizi baadhi ya wajumbe   wa  mkutano mkuu Umoja wa wanawake wilaya  hiyo   Akiwemo Zuhura Mgeni othman , Aziza Yussuf  Salum   pamoja na Mwajuma Hija kipenda wamesema  Uchaguzi huo  utasaidisa kuleta maendeleo  kwa wanawake  wa umoja huo katika kutetea maslahi mbali mbali  katika ngazi za juu za Chama huku wakiwataka watakaochaguliwa kutumikia kwa uadilifu nafasi walizoziomba. 

Uchaguzi  wa kupata viongozi watakaoongoza umoja huo wilaya ya Chake Chake   umefanyika Leo katika ukumbi wa makonyo Wawi. 
 Ambapo  jumla ya nafasi Sita zilpigiwa kura  ikiwa ni pamoja na nafasi ya mwenyekiti wa umoja wa wanawake  Tanzania UWT wilaya Chake Chake, Mjumbe mmoja wa UWT  halamashauri kuu CCM  wilaya  ya Chake Chake, Wajumbe 8   baraza  umoja wa wanawake  wilaya  ya Chake Chake, Mjumbe mmoja mkutano mkuu taifa wilaya ya Chake Chake, Mjumbe 1  wa kuwakilisha jumuia ya  wazazi UWT wilaya  ya Chake, pamoja na Mjumbe mmoja kuwakikisha vijana UWT  wilaya ya Chake Chake. 

 Katika uchaguzi huo   ulichagua  kamati tekelezaji ya UWT wilaya hiyo. 

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI