DC Mjaja afungua kongamano la Amani lililoandaliwa na Taasisi ya Roots & Shoots kwa wanafunzi
Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja amesema maendeleo yakiwemo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii katika taifa lolote hutegemea kuwepo na kuimarika amani, umoja na mshikamano.
Amesema wajibu kwa
wananchi wote bila ya kujali dini, rangi, kabila na tofauti zao katika mitazamo
ya kisiasa hivyo kila mmoja anao umuhimu wake katika kujenga misingi imara ya
amani.
Mjaja ameyasema hao
huko katika Skuli ya Sekondari ya Moh`d Juma Pindua Mkanyageni Wilaya ya Mkoani
wakati akifungua kongamano la umuhimu wa amani lililoandaliwa na Taasisi ya
Roots & Shoots kwa wanafunzi ikiwa ni maadhimisho ya siku ya amani duniani.
Akizungumza kwenye
Kongamano hilo Mratibu wa Roots & Shoots Mkoa wa Kusini Pemba Matti Ali
Matti ameeleza umehimu wa kuwepo wa amani, umoja na mshikamano.
Akisoma risala kwa niaba ya Taasisi hiyo Hussein Abdalla Bakar amesema kufuatia dunia kupotenza misingi yake ya amani ni vyema kuitumia siku hii kuamsha ufahamu juu ya athari za kutokuwepo kwa amani.
Maadhimisho ya siku ya
Amani duniani huanzimishwa kila ifikapo tarehe 21 septemba ya kila mwaka na
haya ni maadhimisho ya 21 tokea kupitishwa azimio la siku ya amani duniani na
umoja wa mataifa.
Comments
Post a Comment