JUMUIA YA WAZAZI CHAMA CHA MAPINDUZI YAASWA KUWA WABUNIFU.

Na AMINA AHMED. 

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi  CCM wilaya ya Chake Chake  Hassan Khatib Hassan amewasa  viongozi  Wlwatakaochaguliwa kungoza Jumuia  ya  wazazi  kuwa wabunifu  kubuni miradi ya maendeleo itakayosaidia kuendesha Jumuia hiyo mbele kimaendeleo . 
Hassan Khatib Hassan. Katibu CCM wilaya ya Chake Chake. 
Katibu Hassan Aliyasema hayo Alipokuwa akizungumza  na wajumbe wa  Jumuia ya wazazi  wilaya ya Chake Chake katika ghafla ya uchaguzi  wa Jumuia hiyo uliofanyik katika ukumbi wa Makonyo  Wawi Chake Chake. 

 Alisema Iwapo viongozi hao watakuwa wabunifu  katika Suala la miradi  ya maendeleo Chama kitaendelea kuwaunga mkono katika kufikisha mbali kimaendeleo Jumuia hiyo . 

Aidha alisema kuwa matarajio ya viongozi watakaopata nafasi ya kuongoza Jumuia hiyo kwa miaka mitano katika nafasi mbali mbali ni kusimamia Jumuia hiyo na kuona Inafika mbali katika ushindani wa vyama vingi mwaka 2025. 

Awali kwa  upande wake Katibu wa Jumuia ya wazazi wilaya ya Chake Chake kupitia Chama Cha Mapinduzi  Fatma Ramadhan Khamis  Aliwaasa wajumbe wa mkutano mkuu Jumuia ya wazazi wilaya ya Chake Chake  kutoa mashirikiano kwa viongozi watakaoteuliwa kuongoza Jumuia hiyo ili kuzidisha uimara   katika Chama na Jumuia hiyo ambayo  ni Jumuia mama kwa Chama hicho.
Fatma Ramadhan Khamis. 
Katibu Jumuia ya wazazi ya Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya ya Chake Chake. 
Wakizungumza baadhi ya wajumbe wa  Jumuia ya wazazi   akiwemo Hadija Henoc pamoja na  Khamis Ali khamis wamewaomba  viongozi hao Kusaidia kuongeza wananchama katika Jumuia hiyo   pamoja kuimarisha  utendaji katika Jumuia na  Chama Cha Mapinduzi pamoja na  kuwezesha sambamba na kuondosha makundi ambayo  ya nakuwa yanajitokeza katika  kipindi  Cha uchaguzi . 
 Khamis Ali Khamis Mjumbe Jumuia ya wazazi wilaya  ya Chake Chake. 
Hadija Henock Mjumbe Jumuia ya wazazi Chake Chake. 
Jumuia hiyo umefanya uchaguzi wa nafasi mbali mbali ambapo viongozi watakaoteuliwa wataongoza Jumuia hiyo kwa kipindi Cha miaka mitano IJAYO.
Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

BARABARA 19 KUJENGWA KWA KIWANGO CHA LAMI PEMBA KUKAMILIKA DISEMBA 2024.

WAZAZI ZIDISHENI KUFUATILIA NYENENDO ZA WATOTO HUSUSAN NI VIJANA .

UONGOZI WA WILAYA CHAKE CHAKE KFHI WAPONGEZA JUHUDI