MAGUMU YA WAGOMBEA WANAWAKE WAKATI WA UCHAGUZI
I
NA, AMINA AHMED MOH’D PEMBA.
IKIWA imebaki miezi michache Tanzania yenye idadi ya watu 61,741,120 wanawake 31,687,990 na wanaume 30,053130 kuufikia uchaguzi mkuu wa nchi mwaka 2025 ,tusiyasahau magumu waliyopitia wagombea wanawake wakati wa uchaguzi.
Uchaguzi ambao kikawaida hufanyika kila baada ya miaka 5 na kutoa fursa kwa watu wote waliotimiza sifa na mashrti yaliyowekwa kwa mujibu wa sheria kuwania nafasi za kuwakilisha wananchi katika vyombo vya maamuzi ikiwemo bunge baraza la wawakilishi pamoja Na baraza la Madiwani .
Changamoto hizo zilizojitokeza 2020 kwa baadhi ya wagombea wanawake ambazo huenda zisiposemewa bhasi ushiriki wa wao katika mchakato wa uchaguzi unaweza ukaendelea kubaki nyuma bila kufikia malengo ya usawa wa kijinsia asilimia 50 kwa 50 katika vyombo vya kutolea maamuzi .
Chanagamoto hizo ambazo ni kutokuwepo kwa maafisa wasiyokuwa waaminifu kutoka Tume ya uchaguzi , Vikwazo,Vitisho,Dharau,Kukosa Fedha za kuendeshea Kampeni, Kukosa na kuondolewa Mawakala kutokuwepo kwa Tume huru kukosa ulinzi pamoja na udanganyifu.
Wanawake wengi ambao baada ya kupata ridhaa ya chama chochote kati ya vyama 19 vya siasa vinavyotambuliwa na msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania na kupata ,fursa ya kuingia katika mchakato wa kuwakilisha moja kati ya majimbo 264 ya uchaguzi yaliopo Tanzania ambayo 214 yapo na mengine 50 yapo Zanzibar .
Makala hii maalum imezungumza na baadhi ya wanawake waliowahi kugombea nafasi ya ubunge katika uchaguzi mkuu uliopita wa mwaka 2020 na kukumbana na kadhia hizo ambapo wanaamini iwapo zitadhibitiwa ushiriki wao utaweza kuongezeka kuelekea 2025 na kufikia usawa wa kijinsia katika vyombo vya maamuzi.
Rukia Abuu bakar Muhammed mwenye umri wa Miaka 34 Mzaliwa wa Chake Chake ambayo ina jumla ya wakaazi 136,298 Wanawake 70,912 na wanaume 65,386 Aliyepata taaluma yake ya ualimu katika chuo kukuu cha Taifa Zanzibar SUZA , Mama wa watoto wa 5 mkaazi wa mtaa wa Chachani wenye idadai ya wakazi 990 wanaume 509 na wanawake 481 wadi ya Tibirinzi yenye idadi ya wakazi 11,089 wanaume 5304 na wanawake 5785 Mkoa wa kusini pemba ambao una jumla ya wakazi 271,350 wanaume 131,373 na wanawake 139,977.
Rukia Abuu ni mwanasiasa aliyezianza harakati hizo mnamo mwaka 2014 ni baada ya kupenda siasa,utayari na sera za Chama cha Democrasia na Maendeleo CHADEMA chama ambacho anaendelea kukitumikia hadi sasa huku akishika nafasi mbali mbali kabla ya kuwania ubunge kwa miongo miwili mfululizo bila mafanikio ambapo nje ya ulingo wa siasa Mwanamke huyo ni mwalimu katika skuli ya Msingi Michakaeni .
‘’Niligombea ubunge jimbo la Chake Chake kupitia Chadema mwaka 2020 lakini niseme tu Uchaguzi kwa sisi Wanawake bado mfumo Dume haujaondoka tunabezwa’’
Licha ya kuwa bado vijana utaskia wengine wanasema aaah !! vijana awa bado hawajui siasa bila kujuwa kuwa siasa haihitaji umri inahitaji utayari na uwajibikaji katika kuleta maendeleo’’
‘’ Bado wanaamini wanaume ambao age- go ndio wana maendeleo , muitikio unakuwa sio mzuri na tunakosa izo fursa kwa sababu za hovyo kama hizo watu hawasikilizi kile ambacho tunakizungumza wala kukichambua na hizo ndizo siasa zetu wazanzibari takriban sote.‘’ Alimaliza Rukia
Licha ya kutokata tamaa kwa sababu hizo za ubaguzi wa kijinsia na umri kutoka kwa aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Chake chake kwa tiket ya Chadema Rukia anasema kuwa ukosefu wa fedha za kuendeshea kampeni pia zilikuwa changamoto kubwa .
‘’kwa upande wetu chadema mwaka 2020 hatukuwa na ruzuku asilimia ndogo tuliyopewa na chama haikukidhi na tulilazmika kufanya kampeni katika mazingira magumu’' .
Kwa sababu nilikuwa natembea maeneo mbali mbali kwa miguu kuomba ridhaa Wapo vijana waliwahi kuniambia wakati napita kuomba kura tukikupa na sisi utatupa nini mtoto mzuri nia yao sio njema Ilikuwa’’
‘’Naamini ningelikuwa mwanaume wasingeweza kuniambia ivo ,lakini pia ingelikuwa nimeenda kwa usafiri wa heshima pia wangeniheshimu kwaio ni changamoto ambazo tunatamani ziangaliwe kuelekea 2025 zisije kujitokeza zikarudisha nyuma ‘’
‘’Suala la Tume linahitaji kifua unakwenda Tume Chake chake pale maafisa wilaya maafisa wa jimbo hawakuitikii muitikio ule ambao wewe unaamini unapaswa kuitikiwa wanakubeza ‘’
Wanapokuja wagombea wanaume unaona wanaongea lugha moja kwa vile ni wanaume wenzao ndio mana wanawake wengine wanahofia kugombea kwa kukosa mashirikiano kwa taasisi inayohitaji itupe mashirikiano’’.
Hali pia haikuwa rafiki kwa Maryam Saleh Juma mzaliwa na mkaazi wa Vitongoji Umangani yenye wakaazi 13,044 wanaume 6,413 na wanawake 66,31 Wilaya ya Chake chake ambae ni mzoefu wa siasa tangia mwaka 1995 Aliegombea nafasi ya ubunge 2020 katika jimbo la Ole wilaya ya Chake chake kwa tiketi ya Chama cha Ukombozi wa Umma chama ambacho kwa uchaguzi wa mwaka 2020 kiliungwa mkono na wana chama wa ACT wazalendo.
‘’Saa nane za usiku bado tulikuwa njiani tunarudi sehemu kituo cha kuhesabiwa kura,huku magari ya doria ya ulinzi na usalama tu ndio yanayozunguruka mitaani atuna hata walinzi sisi wagombea ’’
‘’Hofu zilitutawala hatukuwa na utulivu , Maafisa wa tume wanaubaguzi,Ubabaifu hakukuwa na uwazi wala uhuru ,wanawake hatuheshimiki tunapofika kipindi cha Uchaguzi,tunakosa ulinzi tulilala chini ya msheli sheli ‘’
‘’kituo cha kuhesabiwa kura haki haikuwepo , dhulma za wazi wazi nilizishuhudia mimi mwenyewe zikitendeka nilikuwa na uhakika ndio mshindi wa kiti cha uchaguzi kwa jimbo la Ole’’
‘’Mawakala wangu walibadilishwa na kuwekwa wengine ,na usiku wakati kura zikaesabiwa Madungu wakati tuliambiwa Gombani udanganyifu tunatoka gombani kuja Madungu kura zimeshamaliza kuhesabiwa na wakala wangu alikuwa sie tume haikuwa huru hata kidogo’’ Alimaliza Maryam.
‘’Kuna ulazima haswa wa kupatiwa ulinzi kwa viongozi wote wanaogombea nafasi mbali mbali ili kulinda usalama wao dhidi ya hatari zinazoweza kuwakumba isiwe wanapewa wale wanaogombea nafasi zaa juu tu za urais’’ .
‘’Jitihada zinahitajika kutoka kwa serikali kuona sasa huu ni wakati wa kuwaunga mkono wanawake kushika nafasi za uongozi wasiwawezeshe kwa vyama bali wawawezeshe kwa kundi lao la wanawake tutafanikisha usawa wa kijinsia kuongezeka 2025’’ .
alisema Fat hiya Mussa Said mwanaharakati mwasuala ya wanawake Aliyewezeshwa na TAMWA ZNZ ambao ni miongoni mwa wadau wakubwa wa maswala ya usawa wa kijinsia kwa wanawake .
Rukia anaamini kuwa endapo changamoto hizi zitadhibitiwa kuelekea uchaguzi 2025 hakutokuwa na pingamizi ya wanawake kushindwa kuwa viongozi ndani ya majimbo kwa vile baadhi a vyama vyao vinawaamini katika utendaji.
‘’ Maryam nae akiiomba serikali kutowapa uhuru bila kuisimamia kisheria maafisa wa Tume kwani ni miongoni mwa wavunjaji wa haki za wanawake hususan ni wakati wa Uchaguzi’’
MWISHO.
Comments
Post a Comment