WAHAMASISHAJI JAMII WAPEWA MAFUNZO PEMBA

Na Fatma Suleiman

Wahamasishaji jamii kisiwani Pemba wametakiwa kutumia fursa ya mafunzo ya uongozi waliyopatiwa Ili kusaidia wanawake kushiriki kwenye demokrasia siasa na uongozi.

Hayo yameelezwa na Afisa kutoka Afisi ya mrajisi asasi zisizo za kiserekali Pemba Sada Abubakar Khamis  wakati akifungua mafunzo ya  siku mbili Kwa wahamasishaji jamii, watu wa dini na watu  wenye ulemavu.

Aidha ameongeza kuwa serekali ya muungano wa Tanzania na serekali ya mapinduzi ya Zanzibar zimetoa vipaumbele kwa mwanamke kushika nafasi mbali mbali hivyo ni wajibu wao  kuzichangamkia fursa hizi katika kusonga mbele.

Alizungumza afisa ufuatiliaji na tathmini kutoka chama Cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa _ Zanzibar amesema kupitia mradi huu wanatarajia kufikia watu million Moja na laki Tano wanawake wakiwa zaidi ya elfu kumi na Tano, wanaume elfu kumi na sita, waandishi wahabari mia mbili, wasichana  kutoka vyuo vikuu na skuli mia sita, wanaasasi za kiraiya mia Moja hamsini.

Hafidh Abdi Said mkurugrnzi PEGAO
 amesema mbali na juhudi zinazochukuliwa  ila Bado ushiriki wa wanawake ni ndogo hivyo, ni vyema kushirikiana kwa pamoja kuhamasisha  Ili wanawake kufaidika na kujitoa kushika nafasi za Uongozi ambapo ndio lengo la mradi.

Akiwasilisha mada ya demokrasia mkufunzi wa mafunzo hayo ambae pia ni mwanaharakati Fat_hiya Mussa Said amesema  muda umefika kwa wanawake kutumia haki Yao kidemokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa kama Katiba inavyoelekeza bila ya kubugudhiwa.

Wakitoa maoni yao baadhi ya wahasishaji jamii

Jumla ya wahamasishaji jamii  40  wamepewa mafunzo Kupitia mradi wa SWIL  unaofadhiliwa na ubalozi wa Norway Tanzania unaotekelezwa na taasisi nne ya PEGAO, TAMWA ZAFELA na  huko katika ukumbi wa maktaba ChakeChake Pemba.

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.