ZCRF YATOA MAFUNZO YA SIKU 2 KWA WATETEZI WA HAKI ZA WATOTO PEMBA
Jukwaa la haki za Watoto Zanzibar (ZCRF) ,imetoa mafunzo kwa jumuia zalinazohusiana na watetezi wa haki za watoto Pemba yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kisheria katika utendaji kazi wa kusimamia haki za watoto yaliofanyika katika ukumbi wa Skuli ya Madungu Sekondari leo July 6 .
Akifungua mafunzo kwa wawakilishi wa jumuia 20 ambazo shughuli zake zinawagusa na kuwatetea watoto zaidi kisiwani humo Mratibu wa jukwaa hilo Saphia Lengali amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kusaidia watoto ambao bila utetezi hawawezi kusimamia upatikanaji wa haki zao wenyewe .
Amesema suala la haki za watoto ni suala linalotambulikana kwa mikataba ya kimataifa sheria Tanzania na Zanzibar hivyo wajibu wa kulinda haki zao ni suala linalohitaji ulinzi madhubuti katika sera na sheria hizo kwa kuimarisha zaidi ulinzi na makuzi ya mtoto.
Katika mafunzo hayo mada na maoni mbali mbali yalitolewa katoka kuboresha na kuimarisha ulinzi wa mtoto kwa mujibu wa sheria .
Comments
Post a Comment