UHAKIKI ANUANI ZA MAKAZI MASHEHA WATAKIWA KUFANYA HAYA PEMBA



Na,AMINA AHMED MOH'D- PEMBA.


AFISA mdhamini wizara ya ujenzi mawasiliano na uchukuzi  Zanzibar Ibrahim Saleh Juma amewataka viongozi wa shehia kuwashirikisha  wananchi katika vijiji na maeneo yao kuweza  kupata maoni ya utowaji wa majina  ya mitaa  iliyokosewa na ambayo bado haijatambuliwa  katika mfumo rasmi wa anuani  za makazi (post code)  ili kuweza kutambuliwa rasmi kwa ridhaa na mapendekezo ya wakazi wa maeneo husika  wna  kuepusha mivutano  isoyo na ulazima mara baada ya kukamilika zoezi la uhakiki wa anuani za makazi kwa awamu ya pili. 

Ametoa wito huo kwa nyakati tofauti alipokuwa akizungumza nao, kufuatia ziara maalum ya kuangalia zoezi la  uhakiki wa anuani za makazi linaloendelea katika shehia na maeneo mbali mbali  ya mikoa miwili ya Pemba wenye lengo la kuboresha  na kutambua mfumo rasmi wa  makazi ya wananchi.
            IBRAHIM SALEH - JUMA,A/MDHAMINI                               W.U.M.U  -PEMBA
Amesema wapo baadhi ya wananchi wamekuwa wakiendelea kulalamika juu ya kuwekwa majina wasiyoyatambua katika vibao na nguzo za utambuzi wa  mitaa na maeneo yao ambayo imewekwa kwa ridhaa za  viongozi wa shehia  ,na kuendelea kutambuliwa  majina hayo katika mifumo hiyo bila ridhaa za wanajamii husika jambo ambalo lilitokana na kukosa kushirikishwa ipasavyo wakati wa utambuzi wa awali wa uwekwaji wa vibango hivyo.

Akizungumza  katika ziara hiyo  mwakilishi kutoka   timu ya kitaifa ya kuratibu anuani za makazi kutoka wizara ya Habari mawasiliano na teknologia ya Habari Tanzania Habari Arnold Mkude amesema lengo la uhakiki huo  ni kurekebisha baadhi ya changamoto za mfumo  huo zilizotolewa na wananchi  ,kutokuhakikiwa kwa baadhi ya nyumba,sambamba na kuziingiza katika mfumo nyumba,mitaa na barabara  ambazo hazikuwepo wakati wa uhakiki wa mwaka 2022.
        ARNOLD  MKUDE-  MRATIBU TIMU YA ANUANI ZA MAKAZI TANZANIA  .

Wakizungumza juu ya  zoezi hilo  mratibu wa  anuani za makazi mkoa wa kusini Pemba Mussa Alawi Muhamed , Zena Juma Shamte sheha wa shehia ya   Mtangani, Dodo,ukutini Kinowe  Pamoja na baadhi ya wananchi wamesema kuwa wananchi wanaendelea  kutoa mashirikiano  katika kufanikisha  mpango huo  licha ya kuwepo kwa baadhi ya changamo tofauti,ikiwemo  wananchi kutokuelewa  umuhimu wa zoezi hilo linaloendelea jambo ambalo hulazimika kutumia muda mwingi  kuelimisha kabla ya kufanya uhakiki huo.
   MUSSA ALAWI MUHAMED , MRATIBU P.CODE KUSINI PEMBA .

 Ziara hiyo ya timu ya kitaifa ya kuratibu anuani za makazi kutoka  wizara ya Habari mawasiliano na teknologia ya Habari Tanzania, pamoja na vongozi kutoka wizara zinazohusika na mpango huo Zanzibar zilikagua zoezi hilo katika shehia  mitaa barabara maeneo mbali mbali ikiwemo ukutini mtangani, dodo,kinowe,  katika mikoa miwili ya Pemba.
Mwisho,
 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.