NAZAF KUNYAKUA UBINGWA MWINYI CUP

Na,Amina Ahmed   - Pemba.
HATIMAE  Timu ya Nazaf  kutoka wadi ya  Wambaa imeibuka mshindi  katika  tamati ya mashindano ya Mwinyi Cup iliyoandaliwa na Mbunge wa  jimbo la Chambani ,ushindi ambao ulitafutwa kwa ushindani mkali wa timu 32  kutoka wadi tofauti ndani ya jimbo hilo kwa zaidi ya mwezi mmoja tangia kuanza kwa  mtanange huo.

Mchuano huo wa aina yake  ambao ulipigwa katika viwanja vya Mpira Mapape Chambani jioni  ambapo timu hiyo ya Nazaf iliibuka ushindi wa Goli 3 kwa moja dhidi ya mpinzani na mwenyeji wake timu ya   Black Mamba  kutoka wadiya Dodo  ambayo hadi dakika 90 za mchezo zinakamilika  iliambulia goli 1 .

Timu hiyo ambayo imejinyakulia zawadi ya shilingi  laki sita na 50  kutoka kwa mbunge huyo sambamba  na jezi ambapo mshindi wa pili katika fainali hiyo Black mamba kukabidhiwa shilingi laki 3 na nusu  na jezi  huku mshindi wa tatu akipokea shilingi laki 2    na mshindi wa 4 shilingi laki 1 Taslim.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi   kwa wana michezo wa timu 32   walioshiriki mashindano hayo  mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib  Juma Mjaja amemshukuru mbunge wa jimbo hilo kwa kuandaa mashindano hayo ambayo yamewakusanya vijana kwa pamoja katika kuendeleza michezo ambayo ni mionhoni mwa sera zinazoendelezwa kukuzwa na serikali zote mbili.
 a
"Viongozi wetu wakuu wa nchi Daktari Samia Suluhu Hassan Sambamba na Dk Mwinyi wamekuwa wakituhamasisha siku hadi kufanya michezo,kitendo hichi kilichofanywa na mbunge wetu huyu wa jimbo la chambani  kinaonesha kuunga mkono juhudi za viogozi wetu wakuu katika michezo kwa kuanzisha  mashindano haya".

Aidha katika kuunga mkono juhudi za  viongozi wakuu wa serikali ya Tanzania na Zanzibar Mjaja amesema kuwa uongozi wa wilaya hiyo ya Mkoani umedhamiria kuweka mashindano  ya wilaya ambayo yatazikutanisha  timu za majimbo wilayani humo kuonesha uwezo wao  na kusaidia kupatikana timu moja itakayoiwakilisha wilaya  katika mchezo huo maeneo mbali mbali yaTanzania.

Hata hivyo amewataka wanachambani kuendelea kuunga mkono na kuthamini juhudi zinazofanywa na viongozi  wa jimbo hilo kwa kuwapa mashirikiano .
Nae Mwanzilishi wa Mashindano hayo ambae ni  Mbunge wa jimbo la Chambani Muhamed Abrahman Mwinyi  amesema kuwa lengo la kuanzisha michuano hiyo ndani ya jimbo hilo ni   kukuza  kuendeleza na na kuimarisha vipaji  ili kuzifikia fursa za ajira afya na maendeleo  zinazotokana na  michezo .Aidha amewataka wanamichezo ndani ya jimbo hilo kujiweka tayari kwajili ya mashindano mengine ambayo yataanzishwa  mwanzoni mwa mwezi wa 9 na mwezi wa 2  ambayo yataandaliwa na mbunge huyo mwakilishi  pamoja na madiwani  ambayo yatakuwa na zawadi bora zaidi .

Akizungumzia ushindi wa mchezo na mashindano hayo mfungaji  bora  katika mchezo  wa fainali hiyo ya Mwinyi cup  Abdalla Awesi Abdalla  "Venamass " alisema kuwa hamasa ya kuibua vipaji  vya mchezo wa mpira kwa vijana  ndani ya jimbo hilo iliyofanywa na mbunge huyo inahitaji kuendelezwa  ili viweze kufika  mbali zaidi kwa kuanzishwa ligi  na mashindano mbali mbali ndani ya jimbo hilo wilaya na mikoa  .

Michuano hiyo  ya Mwinyi cup ambayo hadi kukamilika kwake imegharimu jumla ya shilingi  10,636,000   ambapo  kupitia mashindano hayo huduma za matibabu kwa  wananchi waliojitokeza ikiwemo,kuchunguza afya zao kwa magonjwa yasiyowmbukiza ikiwemo,pressure,kisukari,kupata ushauri nasaha,  kupima  virusi vya ukimwi ,sambamba na kuchangia damu salama  ziliweza kutolewa bila malipo .

Katika michuano hiyo viongozi mbali mbali wa chama na serikali  walihuhudhuria kushuhudia burudani hiyo ya aina yake.

Mwisho


Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.