MASHEHA MICHEWENI WAASWA HAYA NI BAADA YA KUKABIDHIWA VIFAA VYA KUTUMIA KWAJILI YA UTAMBUZI WA WANANCHI KUPITIA MFUMO RASMI WA ANUANI ZA MAKAZI KWA NJIA YA KIDIGITALI.
NA, AMINA AHMED -PEMBA.
UONGOZI WA wilaya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba umesema utaendelea kushirikiana na wananchi pamoja na kutoa elimu zaidi katika maeneo ya miji na vijiji ndani ya shehia zote wilayani humo ili waweze kuongeza uelewa juu ya kutumia mfumo rasmi wa anuani za makazi kwa njia za kidigitali na waweze kuitumia katika shughuli zao za kila siku
MGENI KHATIB YAHYA, DC - WILAYA MICHEWENI
Kauli hiyo imetolewa leo na mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya alipokuwa akizungumza mara baada ya kumaliza kukagua vifaa kazi , vilivyokabdihiwa na serikali kwa viongozi wa shehia mbili zilizoanza majaribio ( Pilot area ) ya mfumo huo wa kurahisisha shughuli za utambuzi wa anuani za makazi kwa njia ya kidigitali ghafla iliyoandaliwa na wizara ya ujenzi mawasilino na uchukuzi Pemba.
Amesema mafunzo yaliyotolewa na waratibu wa shehia hizo juu ya matumizi ya mfumo huo ambao unafaida nyingi katika kurahisisha upatikanaji wa huduma za maendeleo itakuwa chachu ya kukuza uelewa kwa wananchi wa shehia za wilaya hiyo kwa kutumia mfumo huo kama ulivyokusudiwana serikali.
"Tutahakikisha elimu inawafikia wananchi na wanaitumia katikashugjuli zao zote ambazo zinahitaji utambuzi kila siku shehia zote 25 zilizopo katimawilaya hii tutakuwa
tukipita kutowa elimu hii i kuongeza uelewa wa matumizi haya ya mfumo"
Hata hivyo Mgeni amewataka masheha hao kutoutumia vibaya mfumo huo na kuwanyima wananchi haki zao mbali mbali sambamba na kuwaasa kuutumia vyema vifaa hivyo katika kuwasaidia kuondoa mivutano inayowakabili na kuwatambua vyema wananchi wao waliowazunguka kwa mujibu wa shehia zao.
"Sisi wilaya hatutokuwa tayari kuona vifaa hivi havitumiki kwa malengo yaliokusudiwa niwaatake masheha kuwa makini na matumizi ya hii mifumo ili mizozo na mivutano isyo ya ulazima kwa wananchi isiweze kujitokeza kila sheha anatakiwa ajuwe wananchi wake kwa umakini mkubwa".
Aidha mkuu wa wilaya huyo ameushukuru uongozi wa wizara ya ujenzi mawasiliano na uchukuzi Pemba kwa kuendelea kujitolea kusimamia kufanikisha utekelezaji wa zoezi hilo la utolewaji wa huduma za utambuzi kwa mifumo ya kidigitali lilotokana na dhamira njema za viongozi wa serikali zote mbili Tanzania za kuwarahisishia mifumo ya upatikanaji wa huduma kwa njia urahisi wananchi wake.
"Tuvitumie vifaa hivi kuweza kuielimisha jamii ,lakini pia kuweza kuwatambua waliotuzunguka katika shehia zetu,vifaa hivi komputer na printer pia zitumike kwa malengo yalikusudiwa"Alisema .
Akizungumza afisa mdhamini wizara ya ujenzi mawasiliano na uchukuzi Pemba Ibrahim Saleh Juma amewataka wasimamizi wa mfumo huo katika shehia kuendelea kuwahakiki na kuwatambua wahamiaji, wageni, wanaojenga katika maeneo yao na kuwaingiza katika mfumo huo
Aliongeza kuwa wizara ya habari mawasiliano na teknlogia ya habari Tanzania kwa kushirikiana na wizara ya ujenzi mawasiliano na uchukuzi Zanzibar itarudi katika shehia zilizobaki kuendeleza zoezi hilo la kuwakabidhi vifaa kama hivyo ili kuogeza maboresho zaidi katika suala hilo la anuani za makazi
"Wapo waliodhani kuwa suala hili la anuani za makazi lilitumika katika kipindi kilecha sensa tu ,lakini wapo ambao wameshaanza kujiuliza mbona mawasiliano wanapita tena katika suala la anuani lakini niwatoe hofu hili ni sualatu la kutqka mfumo kuwatambua kuzitambua shehia zina watu wangapinyumba ngapibarabara ngapina menginyo kwa nia ile ile ya viongozi wetu Dk Samia na Dk Mwinyi kupanga na kuboresha zaidi maendeleo ".
Nao waratibu wa shehia waliopatiwa mafunzo na vifaa hivyo wamesema kuwa wataendelea kushirikiana na viongozi hao katika kutimiza malengo yaliyokusudiwa na serikali juu ya matumizi ya mfumo huo kwa wananchi.
Vifaa hivyo ambavyo ni Komputer,Printer pamoja na Vish kwambi vimetolewa kwa hatua za awali katika shehia ya Konde ,sambamba na Kinowe ambapo shehia hizo mbili za majaribio kwa upande wa kisiwani Pemba zimeanza kutumia mfumo huo.
Mwisho
Comments
Post a Comment