ZSTC YAWAONYA WAUZAJI NA WANUNUAJI KARAFUU KINYUME NA UTARATIBU ULIOWEKWA .

Na,Amina Ahmed Moh'd Pemba.

SHIRIKA la biashara la taifa Zanzibar ZSTC  limewataka wakulima wa zao la karafuu kisiwani Pemba kuacha mara moja suala la uuzwaji wa karafuu kinyume na utaratubu uliowekwa  na shirika hilo ili kuepusha  hasara  na kudhulimiwa na matapeli wanaoingia mitaani kwa njia tofauti kununua zao hilo.
SUDI  SAID ALI,MKURUGENZI MTENDAJI  ZSTC .


Kauli hiyo kwenda  kwa wakulima wa zao hilo kisiwani humo imetolewa na Sudi Said Ali mkurugenzi  mwendeshaji shirika la biashara la taifa Zanzibar ZSTC   usiku wa kuamkia leo alipokuwa akitoa taarifa kwa   waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali huko Makonyo  Wawi kufuatia doria maalum ya ukaguzi na kuwatembelea wakulima wa zao la karafuu  kwajili ya maandalizi ya uuzaji wa zao hilo kwa msimu   maeneo mbali mbali  ambayo imebaini   changamoto ikiwemo kuuza zao hilo kinyume na utaratibu uliowekwa .

Amesema ununuwaji wa karafuu umewekewa utaratibu  sambamba na maeneo maalum hivyo mkulima  kuuza zao hilo kwa watu wasio rasmi  ni kinyume na  sheria huku ikiwasababishia atahari zaidi wakulima hao kutokanana kudhulimwa  kwa mbinu mbali mbali na wanunuaji hao wasio rasmi.

 Sudi amezitaja mbinu hizo zinazo wasababishia hasara wakulima walizozibani kufuatia doria hiyo ni pamoja na wanunuaji hao kutumia pishi  kubwa zisizosahihi, mizani isiyostahili  pamoja na mapolo huku wakinunua kwa baei ya chini  kwa njia ya udanganyifu  ukilinganisha na bei ya shirika iliyowekwa.

"Tumefanya ziara  na doria hii katika maeneo mbali mbali ya kambi za karafuu lakini kwa bahati mbaya kuna wimbi kubwa la   ununuzi wa karafuu ambao wa wanapita katika kambi hizo wakiwadhulumu wakulima kwa njia ya udanganyifu kwa kununua karafuu kwa pishi na tumekuta pishi tofauti tofauti  wanazitumia kuwadhulumu wakulima".

"Wanunuaji hawa ambao sio rasmi wanatumia udanganyifi  kuwadhulumu wakulima  kwanza wanatumia pishi ambazo ni kubwa huku wakiwadanganya wakulima kuwa pishi hii ni sawa na pishi rasmi inayotumiwa, na wanunuaji ndio wanaopata faida mara mbili kwa mtindo huu huku wakulima wakidhulumiwa".

Aidha   kufuatia doria hiyo shirika hilo limefanikiwa kukamata vifaa vya udanganyifu kama vile pishi,shazia mizani pamoja na karafuu kutoka kwa wanunuaji ambao walilazimika kukumbia baada ya kuwaona watendaji wa shirika hilo na kuwacha vifaa vyao huko Mtambile .
Hata   hivyo mkurugenzi huyo amewataka wakulima kuhifadhi vyema karafuu zao ili kusubiri tamko rasmi juu ya ununuzi wa zao hilo kwa msimu huu itangazwe.

Ambapo kupitia mkutano  huo mkurugenzi huyo akawatahadharisha wanunuaji wa zao hilo bila utaratibu uliowekwa kisheria kutokakwa wakulima kuwacha mara moja suala hilo ambapo amesema shirika halitomvumilia yeyote atakaebainika kuenda kinyume na utaratibu katika ununuaji wa karafuu.
Vifaa vilivyo kamatwa katika doria  hiyo ni pamoja na pishi zenyw ujazo tofauti,shazia,mizani pamoja na karafuu kavu.

Mwisho.

 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.