TEEMO YALETA FARAJA KWA WANAFUNZI SKULI ZA MSINGI PEMBA YAAHIDI KUIENDELEZA TANZANIA NZIMA .

NA,AMINA AHMED MOH'D,  PEMBA.
SHIRIKA lisilo la kiserikali  Tanzania Environment  and Empowerment 
( TEEMO ) leo  limezindua  rasmi kampeni maalum ya ugawaji wa vifaa   kwa wanafunzi  wa skuli za Msingi nchini ijulikanayo kwa jina la  "School bag for Batter  Tomorrow"  kwa kugawa vifaa ikiwemo, mikoba,mabuku Penseli pamoja na raba  .

Akizungumza  na wanafunzi  wa Sizini msingi katika uzinduzi wa kampeni hiyo  iliyodhaminiwa na  Shirika la  CEAMSA  kutoka Spain pamoja na  CWEEDMWANI Tanzania  
Mkurugenzi  wa Teemo Winfrida Jackson Shonde amesema kuwa lengo la kampeni hiyo ni   kuwasaidia wanafunzi  wote wa Tanzania  kupata vifaa Muhimu na kuongeza ijasiri wa kufanya vyema katika masomo yao pamoja na kuongeza uelewa kutunza mazingira    .

Amesema  mikoba  hiyo itasaidia   kupunguza matumizi ya mifuko ya plastiki  ambayo kwa asilimia nyingi hutimiwa na wanafunzi kubebea vifaa vya skuli  na kuharibu mazingira hivyo TEEMO  kupitia kampeni hiyo itaendelea kushirikiana na serikali  zote mbili katika kutimiza malengo  yaliyowekewa  juu ya mazingira bora na wezeshi  kwa wanafunzi  .
  

Kwa upande wake  Meneja wa kampuni ya CWEED Mwani  Kanda ya Pemba GERRY SCANDER amesema zoezi  la ugawaji wa mikoba na vifaa hivyo linalofanywa na TEEMO kwa skuli za Pemba  litasaidia wanafunzi kupata mabegi bali litaongeza motisha na kufanya vyema wanapokua skuli.
Wakizungumza baadhi  ya wanafunzi waliopatiwa vifaa hivyo wameishukuru taasisi hiyo kwa kuwapatia msaada huo ambapo wamesema  awali walikuwa wakitumia mifuko kutilia vifaa vya skuli  huku mwalimu mkuu wa skuli  hiyo Sleiman Abdalla Khamis  ameipongeza taasisi hiyo kwa kuendelea kuzisadia jamii  katika harakati mbali mbali  za maendeleo .
TEEMO kwa Kushirikiana na CWEEDMWANI pamoja na CEAMSA imetekeleza  kampeni mbali mbali ikiwa ni  pamoja na kampeni ya   WEZESHA WASICHANA ,MKULIMA WA MWANI BALOZI WA MAZINGIRA  na nyengine mbali mbali ambapo Kampeni hii ya School bag for better tomorrow  iliyozinduliwa leo  inaendelea katika skuli mbali mbali kisiwani humo  .

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.