SERIKALI YA MKOA KUTOA UAMUZI WA MWISHO ENEO LA UJENZI WA SOKO KISIWA CHA KOJANI .
Na ,AMINA AHMED MOH'D
MKUU WA mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib amesema kuwa uamuzi wa mwisho utatolewa na serikali ya mkoa juu ya eneo litakalojengwa soko la wafanya biashara ndani ya wilaya ndogo ya Kojani .
Ameyasema hayo leo mara baada ya kumaliza kupokea maoni ya wananchi ndani ya kisiwa hicho ambayo yalishindwa kutoa maamuzi kufuatia mvutano baina ya wananchi wenyewe kwa wenyewe kutaka kujengwa soko maeneo manne tofauti ndani ya kisiwa hicho katika mkutano maalum uliofanyika katika uwanja wa Kojani mji mpya.
Amesema baada ya kupata maoni hayo ya wananchi serikali itatoa uamuzi utakaoendana na vipimo vya kitaalamu juu ya eneo litakalofaa kujengwa soko hilo litakalowasaidia wananchi kuuza biashara zao maeneo yalio rasmi .
Aidha mkuu huyo amewataka wananchi wa kisiwa hicho kuacha mivutano isiyo na tija yanapokuja masuala ya maendeleo kwa maslahi mapana ya wananchi wa kisiwa hicho.
Awali akizungumza kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Wete Mgeni Khatib Yahya ambae ni mkuu wa wilaya ya Micheweni amewataka Wananchi hao kuunga mkono juhudi za rais wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi katika kuleta maendeleo kwa wananchi wake maeneo mbali mbali.
Awali wakizungumza Baadhi ya wananchi wameiomba serikali kuzingatia maslahi mapana ya wananchi watakapochagua eneo la ujenzi huo .
Mkutano huo uliowajumuisha wananchi wa shehia za kojani ,kamati za ulinzi na uslama mkoa wa kaskazini,watendaji wa baraza la mji Wete , pamoja na viongozi wa jimbo hilo la kojani.
Comments
Post a Comment