RC KASKAZINI PEMBA " NAAPA WAZAZI MTALALA RUMANDE " TUNATAKA MABADILIKO KWA WANAFUNZI WA SKULI HII HARAKA.

NA AMINA AHMED MOH'D PEMBA

MKUU  wa mkoa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib amewataka wazazi na waalimu  wa wanafunzi skuli ya Sekondari Mchanga mdogo  kusimamia na kutoa mashirikiano katika kuziondosha changamoto zinazokwamisha ufaulu mzuri kwa wanafunzi wa kidato cha nne ndani ya skuli hiyo.

Akizungumza katika mkutano maalum  wa  waalimu wazazi,kamati ya ulinzi na usalama, pamoja  wanafunzi  mkuu huyo amesema kuwa bado kuna changamoto  kwa wazazi na waalimu  ikiwemo  suala la ufuatiliaji  wa mienendo ya watoto ,ukosefu wa maadili na nidhamu kwa  wanafunzi wanaosoma katika skuli  hiyo  ambazo zinapelekea kukosa utayari wa kuongeza bidii katika masomo yao jambo ambalo husababisha matokeo mabaya kwa wanafunzi wa kudato cha 4.

Amesema uongozi wa mkoa utaendelea kufuatilia kwa ukaribu mahudhurio ya wanafunzi wa  skuli hiyo na  kuchukua hatua ikiwemo kuwalaza rumande   wazazi wa wanafunzi watoro,pamoja na watakaofanya  vibaya katika mitihani ya majaribio itakayofanywa ili kuleta  mabadiliko na matokeo  chanya kwa wanafunzi  kwa wanafunzi wa kidato cha 4 .

 
Aidha mkuu huyo ameagiza uongozi  wa skuli hiyo kusimamia na kuchukua hatua za kinidhamu kwa wanafunzi watakaovaa mavazi yasiostahiki ikiwemo suruali za kubana ,  kukata mikato isiyo rasmi kufuga ndevu,kutoingia madarasani,kusuka  misuko , hina pamoja  na kuvaa mapambo huku akiwataka wanafunzi wote wa kiume kukata kipara  kuanzia kesho.


 Katika hatua nyengine mkuu huyo ameliagiza jeshi la polisi Mchanga mdogo pamoja na uongozi wa shehia  kuzifuatailia na kuzifungia tv za usiku zinazooneshwa katika vibanda  mbali mbali ndani ya shehia hiyo .

Sambamba na hayo Salama amewataka wazazi kuacha tabia ya kuwatumikisha watoto shughuli za kuuza biashara katika mitaa na maeneo mbali mbali na kuwakosesha muda wa masomo.

Nao baadhi ya wazazi na waalimu  wa wanafunzi wa skuli hiyo  wameushukuru uongozi wa mkoa huo kwa kufanya mkutano  wa kujadili maendeleo ya wanafunzi ambapo wameahidi kutoa mashirikiano katika suala hilo litakalosaidia kuleta mabadiliko kwa watoto wao.

Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi wameuomba uongozi wa wizara ya elimu Pemba kuwasaidia kuwawekea bweni litakalowasaidia kujisomea kwa pamoja  muda wote wote

Mwisho.
  

 



 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.