MWAMUZI WA KIKE PEMBA ALILIA KUKOSA FURSA KATIKA MICHEZO PAMOJA KUBAGULIWA .


Na AMINA AHMED MOH'D PEMBA.
"SISI  waamuzi Pemba tunabaguliwa,hatushirikishwi, hatupewi fursa licha ya kuwa  zipo ,tunakosa  kujifunza, hatulipwi, vitendea kazi  hatuna  ,serikali kama imetuwacha nyuma haituangalii,,tunatukanwa,  vifaa vya mazoezi  hatuna,   mtu  ile flana anavaa mpka dakika za mchezo zinakwisha habadilishi,Ligi zile za serikali silipwi  Kuna siku nauli nakosa kuja mazoezi nadandia tu lifti".

"Nikifika uwanjani nafanya majukumu  ambayo sio yangu sionekani kama mwamuzi naonekana mtu wa kawaida tu,mara niokote mipira mara niwapelekee  watu maji ilimradi sionekani wa hadhi kama waamuzi wengine hususan ni huku kwetu Pemba,ingawa sivunjiki moyo ilani vitu ambavyo natamani vipatiwe ufumbuzi  ".


Yote hayo  ni  maneno  kutoka kwa  Safia Khamis Ali  mwamuzi  wa kati ( centa refa ree )  katika mchezo wa mpira wa miguu  kisiwani Pemba ambae licha ya changamoto hizo na nyengine mbali mbali  hajawahi kuchoshwa na kazi yake hiyo akiamini siku moja Changamoto hizo  zitabaki kuwa hadithi  .
    SAFIA  KHAMIS ALI - MWAMUZI MPIRA WA                                  MIGUU , PEMBA.
Safia, mkaazi wa Kianga Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa kusini Pemba  ambae kwa mapenzi yake aliamua kuipigania nafasi hii katika michezo, ambapo kwa sasa ana zaidi ya miaka 2, ni baada ya kujiona anauthubutu ,ujasiri na utayari   wa kuitendea kazi hiyo  huku michezo ikiwa kwenye damu  akiianza  akiwa skuli.

Alianza kujifunza uamauzi  kwa kuangalia  wengine katika uwanja  Gombani, kwenye runinga kupitia ligi mbali mbali zinaoneshwa  na baadae kupata mafunzo ya vitendo katika uwanja wa Polisi Madungu huku mwalimu wake Akiwa  Muhamed Amour Mwalim (  MD )  .

Safari ya kujifunza uamuzi  haikuishia  hapo Safia pia alilazimika kusafiri  kutoka Pemba kwenda Unguja  na huko pia alipata mafunzo kupitia  baadhi ya waamuzi wa michezo  wa kisiwa hicho  akiwemo Ali Kibo, pamoja na mwalimu Issa. 

Baada ya kurejea tena kisiwani Pemba kazi ya kujifunza iliendelea  ambapo mwalimu wa awali pamoja na mwalimu mwengine waliendelea kumjenga Safia kwa kumfundisha Safia aliekuwa  na dhamira ya kuwa muamuzi .

 Mafunzo ya  vitendo  na mazoezi kwa muda mrefu kutoka kwa walimu wenye uzoefu  waliomfunidisha Safia yaliweza kuzaa matunda ni baada ya  mama huyo kufanya mtihani ambao   ili kutambulika rasmi kama mwamuzi ni suala la lazima kuufanya.

Mtihani huo wa Coper test  haukumuwia ugumu Safia na alifanya vizuri na yeye kuwa mwanamke peke yake kisiwani Pemba aliyeweza  kupata nafasi hiyo ya kuwa mwamuzi wa kati kati wote waliofanya mtihani ambao wote walikuwa ni wa kiume.

Harakati za kuchezesha mechi ndogo ndogo za cen central  zilianza  ambapo hatoweza kuisahau  mechi zake 4 za kwanza kuziamua akiwa  mwamuzi wa kati katika viwanja vya Tibirinzi,Fufuni ,Kangani, huku mechi kubwa ligi daraja la kwanza na daraja la pili akiamua katika   kisiwa cha Unguja  Uwanja wa Mau A na B   nilipata pongezi  nyingi licha ya kuwa ni mara ya kwanza.

Safia  ambae umri wake ni miaka 34   mama mwenye mtoto mmoja,mlezi wa baba mama na familia yake kupitia harakati hizo za michezo na nyengine anazozifanya anahudumia  vyema  familia yake  katika harakati za kila siku  .

Jamii inayomzunguka  Safia  imempokea kwa mitazamo tofauti  ikiwa wapo ambao wanaamini  uamuzi  na michezo kwa mwanamke ni jambo ambalo sio sahihi   huku wengine wakilichukulia suala hilo ni  kuwa la kawaida huku yeye mwenyewe akiamini kuwa maamuzi yake  ya maisha juu ya kile anachokipenda yana muhusu mwenyewe  sio mtu mwengine .

Zulfa Shaame Ali anasema kuwa  mara nyingi anamuona Safia  akijishughulisha na harakati za michezo ambapokwa upande wake anachukulia suala hilo analolifanya  mwamuzi huyo kuwa ni kujitoa ufahamu   ili kutimiza mahitajio yake.

" Naamini anajichetua na kujifaya chakaramau   tu  ili kujipatia kipato cha kuendesha  familiayake lakini sio kazi mbaya kama anapata kipato ,na muhimu anajistiri bhasi  lakini mimi kama mimi sitaki hata siku moja kusema nikaachanganyike na kundi la wanaume eti nachezesha mpira watu wote wananiangalia mimi".

Kwa upande wa familia yake ambayo ni mama,kaka pamoja  na baba mzazi  wa Safia wanamuunga mkono kwa vile mama huyo  anakidhi mahitaji yake ya  mtoto na familia yake    ingawa awali baba yake mzazi hakuonesha kupendezewa na  suala hili kwa kilealichokihofia kuwa anaweza kubadilika  tabia.

"Awali baba yangu alikuwa hataki   nijichanganye na masuala ya michezo nikiwa skuli  mama yangu ndio alikuwa ananiibia kuniagia naenda kushiriki ,lakini kadri siku zilivyozidi   ilw hamasa  ya kupenda michezo kwangu  haijawahi kupungua nilikuwa naenda Gombani kuangalia mpira kila jioni   na ndipo aliponiunga mkono  nashukuru hajawahi tena kuacha kunisapoti  kwa lolote lile".

Mimi ni mama ambae najichumia mwenyewe na nina mtoto mgonjwa  wazazi wangu pia wananitegemea kwa vile na wao ni watu wazima   natofautisha muda wa michezo na majukumi yangu ya nyumbani,ikiwemo kumpeleka mwanangu skuli, kupika na kufanya shughuli nyengine za nyumbani na wala hakuna amabacho kinaharibika na michezo kwangu mara nyingi ni jioni.

Mpambanaji  huyu ambae  licha ya kuwa ni mwamuzi wa mchezo wa mpira  wa miguu ,lakini pia nje ya michezo anajishughulisha na kazi mbali mbali ikiwemo kushona ,pamoja na kufanya biashara ndogo ndogo .

Muhamed Amour Mwalim (MD) ni mwamuzi wa mpira wa miguu kanda ya Zanzibar  ambae pia ni mkufunzi  wa uamuazi kwa wanafunzi mbali mbali anasema kuwa alimfahamu Safia viwanjani  kwa kuwa mwanamke ambae aliiona nia yake ya michezo jambo balo halikumuia ugumu  kumfundisha  Uamuzi  wa soka alipomuomba kumsaidia suala hilo.
       MOHAMED AMOUR MWALIM (MD )                        MWAMUZI, MPIRA WA MIGUU KANDA YA       ZANZIBAR.
" Niko  na wanafunzi wengi  rika  tofauti na kwa sasa niko na wanafunzi sita ambao wote wako katika standad nzuri  ya kuhakikisha wanafanya maamuzi   sahihi ya kuzitafsiri sheria 17 za mpira wa miguu,na actual safia ni mwanafunzi wangu kweli  na mara nyingi nilikutana nae humu humu viwanjani  kuna siku tunakimbia nakumbuka akanifata akaniomba nimfundishe uamuzi kwa vitendo nikamfundisha na wezake ambao ni wanaume huku mwanamke akiwa yeye peke yake tangia nimeanza kuwafundisha wanafunzi na alikuwa na utayari".

 Anafanya vizuri na mimi niwaambie wazazi fursa zipo wasiwanyime watoto wakike uhuru  kwa sababu zisizoeleweka  mpira ni ajira mpira ni fursa kama mavazi ndio tatizo  hakuna sheria inayo muamuru mwanamke kuvaa nusu uchi nimaamuzi ya mtu mwenyewe"

Ni kweli bado wanawake huku kwetu wapo nyuma katika michezo na mfano ni huyu safi mimi nishafadisha wengi lakini kwa mwanamke ni yeye peke yake Na mimi sitosita kumfundisha yeyote ambae atakuwa na utayari nipo tayari mda wote nawakaribisha katika kuona tunaongeza usawa na ushiriki  wa kijinsia katika michezo "

Kassim Juma Salum ni katibu wa  mpira wa miguu kwa  vijana ( central  ) wilaya  ya Chake chake  anasema anamuona mbali Safia  endapo  changamoto anazokumbana nazo  katika viwanja  na  kujengewa uwezo  zitapatiwa ufumbuzi  na wadau wa soka.

" Tunamtumia sana  katika  michezo yetu  na kiukweli ni mwamuzi  mzuri, anauwezo wa kukimbia na kuzitafsiri sheria 17 za mpira ipasavyo ni mwamuzi hana utofauti na hao wanaume  katika kutekeleza jukumu lake  hilo ,kuhusu  changamoto  ni za kawaida   endapo atawezeshwa ipasavyo ataweza kufika mbali zaidi "

Safia anasema kuwa  michezo haiondoi  stara na heshima  ya mtu  ambayo mwenyewe ataamuwa kujiwekea  huku akiamini kuwa mavazi pia ni maamuzi mabaya ni   mtu mwenyewe  binafsi mimi navaa stoking refu,  tight,kilemba  na suruali refu bodi suti na wala hakuna anaeona mwili wangu .  

" Ukweli ni kwamba  changamoto ni nyingi  kwanza tunatukanwa  bado hakuna elimu ya michezo timu ikifungwa mashabiki wanakutukana matusi ambayo hata wazazi wao hawawezi kukubali endapo watatukanwa bila hata kupimwa.

" Uamuzi kwetu bado hauonekani wa thamani sio kwa mwanaume  wala wanawake  sisi wanawake  ndio tumezidi  hatushirikishwi tunazisikia tu fursa za michezo wanapelekewa watu ambao hata hawastahiki mifano mingi ipo".


"Muamuzi unaweza ukachezesha mechi ambayo unajipa matumaini  hii utapata walau pesa ya daladala lakini wapi mpka leo kuna mechi tumechezesha hatujalipwa  tena za serikali  kombe la mapinduzi, na hata yale maji hatujapewa tumedai mpaka tumesamehe "

Vifaa  kama jezi  hatuna pia ,sishirikishwi  nadra sana kupewa  fursa niamue  mechi , nathubutu kujiita muamuzi kwa vile nimepata elimu na nina ule utayari lakini  hata vile kupewa kujaza fomu  bhasi sipewi  nakata tamaa lakini najipa moyo lakini mambo magumu ndio mana  najikeep  bussy na mambo mengine huku tunalegeza kamba kwa sababu  hakuna maslahi  fursa wanakula wengine"
Vifaa kama becon,Jezi,mipira,suruali,viatu, mafunzo kushirikishwa vyoote tunakosa  yaani tupo nya sana michezo haionekani kama ni ajira kwa upande wetu"

Nina ndoto za kufika mbali  sana kimichezo natamani siku moja niamue mechi zenye  ushindani ,kimataifa na kitaifa kwa sababu uwezo ninao wadauwa michezo serikali na wapenda maendeleo  kwa wanawake msiache kuniunga mkono uwezo ninao na uthubutu pia ".

 Safia anasema kuwa  si tu  uamuzi wa mchezo  wa  mpira lakini pia utayari wake upo hata kwa kufundisha wengine  michezo ,na kushiriki yeye mwenyewe ni miongoni mwa vitu alivyo na uthubutu navyo.

Mwisho.


 


Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.