ZMBF YAFUNGA KAMBI SIKU 5 MICHEWENI KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU NA UCHUNGUZI WA MAGONJWA MBALI MBALI .

NA AMINA AHMED MO'HD.
 PEMBA.

Taasisi ya zanzibar maisha bora faundation imesema itaendelea kuunga mkono upatikanaji wa huduma bora za matibabu kwa wananchi  visiwani zanzibar ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya nane katika uboreshwaji wa huduma za matibabu  kwa wananchi wake. 
Kauli ya mweneyekiti wa taasisi hiyo Maryam Mwinyi  imetolewa kwa  niaba na mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib Alipokuwa akizungumza na wananchi mbali mbali mara baada ya kumaliza bonanza maalum lililoanzia katika eneo la kilindini na kumalizika katika viwanja vya Shaame  mata ikiwa ni  uzinduzi wa kambi ya  maisha bora afya bora  iliyoandaliwa na taasisi hiyo .
Amewema licha ya taasisi hiyo kutoa huduma za uchunguzi wa magonjwa mbali mbali kwa wanachi 8000 upande wa kisiwani unguja lakini pia imelenga kutoa huduma ya uchunguzi kwa wagojwa 5000 kwa upande wa kisiwa cha Pemba kupitia kambi hiyo .
Amesema lengo la kambi hiyo nikuhakikisha wananachi  wanaishi katika maisha bora huku wakiwa na afya njema.

Nae afisa Mtendaji mkuu wa tasisi hio Fatma Fungo amasema tasisi yao chini nya program ya maisha bora afya bora imeshatoa huduma ya matibabu kwa wannachi zaidi ya elfu Nane kupitia kambi mablimbali  wanazoziweka ,huku kambi hio inatarajiwa kuhudumia zaidi ya Wananchi elfu 5.
Mapema Afisa Mdhamini Wizara ya Afya Wemba Khamis Bilali amesema wizara ya Afya imejipanga kutoa huduma mbalimbali za Afya kwa Wananchi wote watakaokuja katika kambi hio.
Uzinguzi wa kambi hio ya siku 5 ambayo imeandaliwa na tasisi  ya maisha bora foundation chini ya program ya maisha bora afya bora ilianzia na matembezi na  mazoezi ya viungo

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.