KAMBI YA MAISHA BORA AFYA BORA JUU YA UCHUNGUZI WA MAGONJWA MBALI MBALI KUANZA RASMI KESHO MICHEWENI .


Na, AMINA AHMED PEMBA.
WANANCHI  wenye matatizo ya kiafya Kutoka maeneo mbali mbali ya kisiwa cha Pemba wametakiwa kujitokeza kwa wingi  katika  kambi ya siku tano ya  uchunguzi wa  magonjwa mbali mbali  itakayoanza rasmi kesho tarehe 8  katika viwanja vya  Shaame Mata wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba  ili kuweza kuchunguza afya zao  bila malipo yeyote na kuweza kupatiwa matibabu   .
        SALAMA  MBAROUK KHATIB  -RC             KASKAZINI.

Wito huo  umetolewa na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib alipokuwa akizungumza na wananchi wa maeneo mbali mbali kupitia mkutano maalum na waandishi wa habari wa vyombo tofauti ulioandaliwa na Taasisi ya Zanzibar  Maisha Bora Faundation  (ZMBF) huko katika ukumbi wa Micheweni mapema leo kuelekea uzinduzi maalum wa kambi hiyo   itakayozinduliwa kwa bonanza maalum  la maisha bora afya bora mapema kesho asubuhi .

Amesema Taifa bora ni lile ambalo wananchi wake wanakuwa na afya hivyo lengo la  kambi hiyo   ya siku tano inayotarajia kuchunguza   afya za  watu elfu 5 imedhamiria kurahisisha  huduma ya uchunguzi wa magonjwa mbali mbali .
  

Aidha Salama amewatoa hofu wananchi  ambao wataweza kufika katika kambi hiyo amabao watabainika  kuwa  na magonjwa yeyote baada ya uchunguzi   na kusema kuwa  utaratibu wa rufaa kwajili ya matibabu  utatolewa .

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya  amesema kuwa tayari maandalizi kwajili ya bonanza na kambi hiyo ya maisha bora afya bora  ndani ya wilaya hiyo yamekamilika ikiwemo suala la kuimarisha ulinzi na usalama  zaidi katika kutimiza malengo ya kambi hiyo.
     MGENI KHATIB -DC ,MICHEWENI.

Akitoa ufafanuzi juu ya kambi hiyo ya uchunguzi  afisa mdhamini  wizara ya Afya Pemba  Khamis Bilali Ali amesema kuwa Madaktari bingwa  wa magonjwa mbali mbali wanatarajiwa kuungana pamoja katika kambi hiyo  ya siku tano .
     KHAMIS BILAL ALI - MDHAMINI AFYA PEMBA.

Hata hivyo amewataka wananchi pia kuunga mkono zoezi la uchangiaji damu katika bonanza hilo .

 Miongoni mwa  huduma za uchunguzi  zinazotarajiwa kutolewa katika kambi hiyo iliyoandaliwa na taasisi hiyo ya zanzibar  maisha bora faundation    
kwa lengo la kuondoa  changamoto ya maradhi mbali mbali   ni pamoja na  huduma za  uchunguzi wa X ray ,uchunguzi wa magonjwa ya  Moyo, uchunguzi wa  sitiscan, huduma uchunguzi meno,ngozi,macho na nyenginezo.
Mwisho.
 



WANANCHI  wenye matatizo ya kiafya Kutoka maeneo mbali mbali ya kisiwa cha Pemba wametakiwa kujitokeza kwa wingi  katika  kambi ya siku tano ya  uchunguzi wa  magonjwa mbali mbali  itakayoanza rasmi kesho tarehe 8  katika viwanja vya  Shaame Mata wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba  ili kuweza kuchunguza afya zao  bila malipo yeyote na kuweza kupatiwa matibabu   .

Wito huo  umetolewa na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib alipokuwa akizungumza na wananchi wa maeneo mbali mbali kupitia mkutano maalum na waandishi wa habari wa vyombo tofauti ulioandaliwa na Taasisi ya Zanzibar  Maisha Bora Faundation ( ZMBF ) huko katika ukumbi wa Micheweni mapema leo kuelekea uzinduzi maalum wa kambi hiyo   itakayozinduliwa kwa bonanza maalum  la maisha bora afya bora mapema kesho asubuhi .

Amesema Taifa bora ni taifa ambalo wananchi wake wanakuwa na afya hivyo lengo la  kambi hiyo   ya siku tano inayotarajia kuchunguza   afya za  watu elfu 5 imedhamiria kurahisisha  huduma ya uchunguzi wa magonjwa mbali mbali .
  

Aidha Salama amewatoa hofu wananchi  ambao wataweza kufika katika kambi hiyo amabao watabainika  kuwa  na magonjwa yeyote baada ya uchunguzi   na kusema kuwa  
utaratibu wa rufaa kwajili ya matibabu  utatolewa .

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya  amesema kuwa tayari maandalizi kwajili ya bonanza na kambi hiyo ya maisha bora afya bora  ndani ya wilaya hiyo yamekamilika ikiwemo suala la kuimarisha ulinzi na usalama  zaidi katika kutimiza malengo ya kambi hiyo.


Akitoa ufafanuzi juu ya kambi hiyo ya uchunguzi  afisa mdhamini  wizara ya Afya Pemba  Khamis Bilali Ali amesema kuwa Madaktari bingwa  wa magonjwa mbali mbaliwanatarajiwa kuungana pamoja katika kambi hiyo  ya siku tano .

Hata hivyo amewataka wananchi pia kuunga mkono zoezi la uchangiaji damu katika bonanza hilo .

 Miongoni mwa  huduma za uchunguzi  zinazotarajiwa kutolewa katika kambi hiyo iliyoandaliwa na taasisi hiyo ya zanzibar  maisha bora faundation    
kwa lengo la kuondoa  changamoto ya maradhi mbali mbali   ni pamoja na  huduma za  uchunguzi wa X ray ,uchunguzi wa magonjwa ya  Moyo, uchunguzi wa  sitiscan, huduma uchunguzi meno,ngozi,macho na nyenginezo.

Mwisho.
 





Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.