EPA YAADHIMISHA SIKU YA ZIPASO KWA BONANZA LA AINA YAKE PEMBA TIMU YA WANAFUNZI YAIBUKA NA USHINDI .
Na - AMINA AHMED MOH'D,PEMBA.
TIMU ya chuo cha utawala wa umma EPA epa student imeibuka kidedea katika mchezo wa fainali ya mpira wa miguu uliofanyika katika viunga vya uwanja wa Gombani kongwe Chake Chake Pemba ikiwa ni bonanza maalum la maadhimisho ya siku ya serikali za wanafunzi ZIPASO day .
Fainali hiyo iliyochezwa kati ya wanafunzi wa chuo hicho pamoja na vijana kutoka timu ya mpira pesa Chake chake ambapo kabla ya fainali hiyo jumla ya timu 4 ziliumana kuutafuta ushindi katika viwanja hivyo hapo jana majira ya saa 10 jioni ambazo ni Epa student,Transfoma,Epa Staff pamoja na timu ya mpira Pesa.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa fainali na michezo mbali mbali katika bonanza hilo Wakili wa Serikali Kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Pemba Jecha Vuai Jecha ameipongeza zipaso kwa kuandaa boananza hilo kisiwani Pemba ambapo amesema kuwa litasaidia kuongeza hamasa kwa vijana na jamii katika kujiunga na chuo hicho ambacho kinarudisha shukurana kwa kufanya kazi na kushiriki shughuli mbali mbali kwa wananjamii.
Akizungumza kwa upande wake mara baada ya kumalizika kwa fainali hiyo iliyotanguliwa na michezo na burudani mbali mbali rais wa serikali ya wanafunzi kutoka chuo cha utawala wa umma Epa Najla Abdalla Mussa amesema kuwa lengo la kuadhimisha siku hiyo ni kuleta mashirikiano ya pamoja kupitia michezo kwa wanafunzi wa chuo hicho matawi mbali mbali unguja na Pemba .
Aidha Najla amesema kuwa kupitia bonanza hilo ni kuionesha jamii uimara wa elimu zinazotolewa na chuo hicho katika kuisadia na kuhamasisha wanafunzi ambao wameshindwa kuendelea na masomo pamoja ushiriki wa shughuli mbali mbali ikiwemo michezo.
Kwa upande wake Afisa uhusiano wa chuo hicho amewataka vijana wenye sifa za kujiunga na chuo hicho kuwahamasisha vijana walioshiriki bonanza hilo pamoja na walioko katika maeneo mbali mbali kujiunga na chuo hicho kwajili ya kupata kozi mbali mbali zitakazowasaidia kujiendeleza kiuchumi ambapo kwa sasa tayari udahili wa wanafunzi wapya umeanza.
Zawadi ya pesa taslim pamoja ja flana kwa washindi wa mpira wa miguu ambao ni timu ya Epa student zimetolewa huku washiriki wengine walioshiriki michezo kama vile mbio za magunia,kufukuza kuku,mashindano ya kukuna nazi, pamoja na kukimbia zilitolewa uwanjani hapo ambapo kabla ya maadhimisho hayo ziposa kutoka Epa pia waliwatembelea na kuwafariji wazee katika nyumba ya wazee Wete mkoa wa Kaskazini Pemba.
Mwisho .
Comments
Post a Comment