WAANDISHI ,WAMILIKI WA VYOMBO WAHIMIZWA KUANDIKA HABARI ZA MICHEZO KWA WANAWAKE HUKU VIONGOZI WA SERIKALI WAKIASWA KUTEKELEZA KWA VITENDO SERA YA MICHEZO KWA WOTE ILIYOWEKWA NA SERIKALI ZANZIBAR.
.
Na, AMINA AHMED
PEMBA.
WAMILIKI na waandishi wa vyombo mbali mbali vya habari wametakiwa kutoa kipaumbele katika kuandika na kutangaza habari zinazo gusa maendeleo na changamoto katika sekta ya michezo kwa wanawake ili kukuza ushiriki wa kundi hilo katika michezo kisiwani Pemba.
Kauli hiyo imetolewa na Mwandishi mwandamizi Zanzibar Hawra Shamte,alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali kisiwani humo wanaoendelea kushiriki katika mafunzo ya siku 5 ya kujengewa uwezo juu ya kuandika habari za ushiriki wa michezo kwa wanawake yaliondaliwa na TamwaZanzibar katika ukumbi wa ofisi za chama hicho Mkanjuni Chake Chake .
Amesema bado mchango wa waandishi na vyombo vya habari Zanzibar umekuwa hauridhishi katika suala la utoaji wa habari zinazogusa michezo kwa wanawake jambo ambalo linaendelea kurudisha nyuma na kupelekea kukosekana hakasa kwa wanawake kujiingiza katika michezo visiwani humo.
Aidha Hawra ameitaka jamii kuendeleza uwezeshaji wa wanawake na wasichana, katika michezo mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuwacha mila potofu na mitazamo hasi juu ya ushiriki wao katika michezo .
Mwandishi huyo mwandamizi akatumia fursa hiyo kuwaomba viongozi na watendaji wa sekta za Michezo kuifanyia kazi sera ya Michezo iliyowekwa na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Michezo kwa wote ( "Sport for All " )yenye lengo la kuweka usawa wa kijinsia katika michezo.
Kwa Upande wake Mratibu wa chama cha waandishi wa habari Tamwa Zanzibar Ofisi ya Pemba Fat hiya Mussa Said amewataka waandishi hao kuwa waandishi wa mabadiliko katika kuwasaidia wanawake visiwani humo kuitumia haki hiyo ya ushiriki wao katika michezo mbali mbali ili kuweza kujipatia maendeleo wanayoyakosa kutokana na kutokushiriki ipasavyo katika michezo mbali mbali.
Mafunzo hayo ya siku Tano kwa waandishi hao kisiwani humo ni katika utekelezaji wa mradi wa kukuza usawa wa Kijinsia katika Michezo (Cohort Gender and Sports) ambao umeanza mwezi March mwaka 2024 na kutarajiwa kukamilika February 2025 ambapo zaidi ya waandishi wa habari 20 Unguja na Pemba wamepatiwa mafunzo hayo ya kujengewa uwezo katika uandishi wa habari za michezo kwa wanawake .
Mwisho.
Comments
Post a Comment