MRAJIS ASASI ZA KIRAIA ZANZIBAR AWAPONGEZA WANAVIKUNDI SHIRIKISHI

 NA , AMINA AHMED MOH'D.

MRAJIS  wa asasi za kiraia Zanzibar  Ahmed Khalid amewaasa wana vikundi jumuishi  vya ushirika wa kukopa na kuweka  kisiwani Pemba  kuendeleza  umoja na mashirikiano katika kutatua changamoto mbali mbali na kusaidia kutimiza malengo yao waliyojiwekea  katika kujiendeleza kiuchumi bila kuwa na utegemezi .


Ametoa wito huo leo alipokuwa akizungumza na wana vikundi  wa aina mbali mbali Ole, Mvumoni pamoja na Mbuzini wilaya ya Chake chake katika ziara maalum ya kukagua  vikundi vya uwezeshaji kiuchumi kwa watu wenye ulemavu  (Kijaluba isave  )  ikiwa ni utekelezaji wa  mradi jumuishi wa kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchumi ambayo imeandaliwa na  shirikisho la jumuia za watu wenye ulemavu zanzibar Shijuwaza.
Amesema  changamoto zinazojitokeza katika vikundi hivyo zinaweza kupata ufumbuzi iwapo wanavikundi hao watakuwa na mashirikiano ya pamoja katika kuzalisha fikra  za pamoja  zitakazobadilisha changamoto kuwa fursa za kimaendeleo.


Aidha mrajis  huyo amewapongeza wanavikundi hao kwa  kuendelea kufikia malengo ya  mradi wa kijaluba isave  kujiwezesha kiuchumi bila utegemezi kwa watu wenye ulemavu  .

 Hata hivyo amesema kuwa wataendelea kuzisemea changamoto mbali mbali zinazowakabili katika kuendesha vikundi hivyo ikiwemo kukosa  fedha ili kupatiwa ufumbuzi.

Wakizungumza  na wanaushirika hao mwenyekiti wa shijuwaza Mwan - dawa  Khamis  pamoja na  mjumbe wa bodi shijuwaza  Joseph  Abdalla  Meza wamesema kuwa  Jumuia hiyo i5a3ndelea kuwa mstari wa mbele katika kuona watu wenye ulemavu wanapewa kipaumbele katika shughuli za maendeleo.

Akitoa taarifa kuhusu mafanikio ya  mradi huo Msaidizi afisa mradi kijaluba isave  Upande wa Pemba Aisha Abdalla Juma  amesema kuwa mwaka mmoja wa majaribio katika mradi huo wa majaribio umefanikiwa kufikia malengo yaliokusudiwa ya kuweza kujisimamia wenyewe katika shughuli mbali mbali  za kimaendeleo.

Amesema miongoni mwa mafanikio yaliyofikiwa katika mradi huo ni kuwaweka pamoja watu wenye ulemavu na wasio na ulemavu   kushirikiana pamoja katika  kujiwekea hakiba  na kuweza kupata mikopo ya kuweza kufanya shughuli zao  za kujitegemea kiuchumi.

Nao baadhi ya wanavikundi hao  akiwemo said Omar Said wameishukuru  shijuwaza na Tamwa  kwa kusimamia mradi huo  wa Kijaluba isave ambao umewaletea mabadiliko   katika kujikomboa kiuchumi ikiwemo kubadilika kiakili katika kujitegemea wenyewe watu wenye ulemavu kiakili.

Mradi huo wa majaribio  kwa wanaushirika  umekusanya jumla ya shilingi milioni 54 laki moja  elfu tisini  800 ambapo  vikundi    21   katika maeneo mbali mbali  ya shehia hizo tatu vimefanikiwa kuendesha shughuli zao  ikiwemo kukopeshana fedha  na kuanzisha biashara mbali mbali ambapo asilimia 60 ya wanachama  wa vikundi hivyo ni watu wenye ulemavu  .

 

Comments

Popular posts from this blog

BAJAJI WAMLILIA RAIS DK MWINYI PEMBA ,WAOMBA MSAADA KWAKWE WASEMA WAMECHOSHWA NA HILI KUTOKA MAWASILIANO

Masheha wanawake wa Wilaya ya Magharib B walivyoleta mabadiliko na maendeleo kwenye shehia zao.

MPANG0 MKAKATI JUMUISHI WA JINSIA KATIKA MICHEZO UTEKELEZAJI WAKE UZINGATIWE.