MICHE 10000 YA MIKOKO YAPANDWA KAMBINI PPC WAUNGANA NA WANANCHI KUDHIBITI UHARIBIFU WA MAZINGIRA.
Na,Amina Ahmed Moh'd Pemba.
WANACHAMA wa Club ya waandishi wa habari Pemba ( PPC ) wakishirikiana na Wanakijiji wa Kambini Kichokochwe pamoja na jumuia ya Community Forest Pemba ( CFP ) wameshiriki zoezi la upandaji wa miche aina ya mikoko ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo habari duniani.
Zoezi la upandaji wa miche hiyo limefanyika mapema leo katika bahari ya Kambini Kichokochwe Mchanga Mdogo wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba ambayo ni moja kati ya maeneo 200 kisiwani humo yaliy𝕠𝕙𝕒𝕣𝕚𝕓𝕚𝕨𝕒 na mabadiliko ya tabia ya nchi kutokana na ukataji wa miti hiyo kiholela kwajili ya matumizi mbali mbali.
Awali akizungumza kwa niaba ya wanachama hao ambao ni waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali kutoka kisiwani humo mwenyekiti wa club hiyo Pemba Bakar Mussa Juma amesema lengo la kuadhimisha siku hiyo kwa kushiriki zoezi hilo la upandaji wa miche ya mikoko ni kusaidia kuendeleza kukabiliana na athari za kimazingira zinazopelekea kuleta mabadiliko ya tabia ya nchi.
Aidha Mwenyekiti huyo ameishukuru CFP kwa kukubali kuwaunga mkono katika kufanikisha zoezi hilo la upandaji wa miche ya mikoko katika bahari hiyo ya kichokochwe ambapo amesema itakapokuwa itasaidia kudhibiti kupanda kwa maji ya bahari katika maeneo ya makazi ya watu .
Kwa upande wake mwenyekiti wa CFP Kombo Seif Khamis ameishukuru club ya waandishi wa habari Pemba PPC kwa kutambua umuhimu wa kutunza mazingira ambapo amewataka kuendelea kuelimisha jamii kupitia vyombo vya habari vyao umuhimu wa kutunza mazingira na kupanda miti huku akizitaka club wananchi na wadau wengine mbali mbali kuiga mfano huo uliotolewa na PPC.
Nao baadhi ya wanakijiji wa Kambini kichokochwe wameishukuru Club hiyo kwa kwa kujitolea juu ya suala hilo katika kijiji chao ambapo amesema licha ya juhudi mbali mbali wanazoendelea kuzichukua ikiwemo kupiga matuta kudhibiti maji ya chumvi kusogea katika maeneo ya wananchi lakini bado yamekuwa yakiwaletea athari mbali mbali hivyo upandaji wa miche hiyo kutasaidia kukabiliana na athari zinazojitokeza ikiwemo kuharibika kwa mashamba yao kutokana maji ya bahari yanayoendelea kusogea siku hadi siku katika maeneo yao.
Akitoa ufafanuzi juu ya athari za mabadiliko ya tabia ya nchi Mbarouk Mussa kutoka CFP amesema ni vyema jamii ikaendelea na utaratibu wa upandaji wa miti kwani kutasaidia kupunguza athari mbali mbali ikiwemo kuongezeka kwa joto sambamba na kuhuisha urithi wa kijani kama ambavyo serikali inataka .
Katika Zoezi hilo Jumla ya miche ya Mikoko elfu 10000 imepandwa katika eneo la bahari hiyo ya Kichokochwe ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali ya Mapinduzi ya zanzibar pamoja na wadau mbali mbali wa mazingira dunianin katika kukabiliana na athari zinazotokana na mabadiliko ya tabia ya nchi .
Mwisho.
Comments
Post a Comment